Jumatatu, 15 Juni 2015

SAHIHI YA KIFO

 SEHEMU YA TATU


Bwana Helman alianza kunifanya nichelewe kurudi
nyumbani kwangu kwa kunipitisha sehemu nyingi
za anasa na kunikutanisha na marafiki zake
ambao
wengi walionekana ni wenyeji wa Arusha,.kila
walipo kaa walikuwa wanazungukwa na
wasichana

ambao nilikuwa nashindwa kuwaangalia kwa
mara
ya kwanza kutokana na nguo zao za anasa
walizo
kuwa wanavaa.
Hivyo sehemu hizo za starehe zilinifanya
kumgeuza mke wangu magrety kuwa mlinzi wa
nyumba na mtunza muda kwa kuangalia saa ya
ukutani ni saa ngapi narudi na alipo sikia honi ya
gari majukumu ya kufungua mlango pia aliyabeba
na alinivumilia sana hata nilipo amia dunia
nyingine yenye utembeaji wa kupepesuka( ya
ulevi)
Nakiri kuwa sikuwahi kumpiaga mke wangu hata
nilivyo kuwa katika hali hiyo. Ilifika kipindi nikawa
na kosa hata muda wa kuzungumza na watoto
wangu vipenzi japo kwa wakati huo David ndiye
aliye kuwa na akili ya kunijibu na kunielewa nini
na
zungumza pia kwa utoto wa Nisha wa kuzunguka
zunguka na kupiga kelele pale subuleni wakati wa
mazungumzo ya hapa na pale ili kuendelea
kujenga amani na upendo niliukumbuka pia;
Namshukuru sana mke wangu siku ya jumamosi
majira ya saa tatu usiku nikiwa tayari
nimejiandaa
kutoka ndipo alipo niweka chini na kunikumbusha
mateso niliyo yapitia wakati na soma shida ngapi
nili pata na leo na tumia fedha bila kujali kuwa
kuna watu wenye shida duniani pia hata upande
wa penzi lake, baba yake alikuwa na fedha kiasi
ambacho yeye aliweza kuniibia na kunipatia ili
niweze kuendeleza masomo yangu na kujikimu
kwa
mahitaji madogo madogo.
Hakika jambo hilo lili niingia kichwani na kuona
kuwa Helman sio rafiki mzuri kwangu
sikuchelewa
niliingiza mkono mfukoni na kutoa nokia yangu
kisha kubonyeza vitufe 0654000092 na kupiga
sekunde kadhaa simu ikaanza kuita na muda huo
huo ikapokelea nilicho anza kukisikia ni kelele
nyingi za mziki na sauti za wanawake
tofauti ,hivyo nilijua tayari wamesha wasili baa na
wenzie wanakunywa pombe tu, akanzaa
kuongea,,,
“hallo uko wapi wewe mbona tunakusubiri
hutokei”? Aliuliza Helman kwa sauti ya juu ili
aweze kusikika kutoka na eneo alilopo
“Helman naomba usogee sehemu yenye utulivu
kidogo ili tuzungumze”nilimwambia
“Eeh uko wapi sasa? maana huku warembo
wanakusubiri kwa hamu uje kuwa mwagia pesa”
sauti hiyo aliyo ongea Helman, Magrety aliweza
kuisikia alizidi kujua vitendo alivyo kuwa na
vifanya
mme wake,Alfredy, aibu ikamshika Alfred ndipo
alipo zungumza kwa ukali,,,,,
”Sikia Helman kuanzia sasa urafiki wetu mimi na
wewe umeisha siwezi kutelekeza familia yangu
sababu yako na hata ukija ofisini nita kuhudumia
kama wateja wengine na sio kama rafiki yangu
pia
nyumbani kwangu sikuhitaji”
kisha akakata simu. upande wa Helman akawa
anaendelea kulalamika,,,,,
“hallo?,hallo? Lakini bila mafanikio alipo itazama
simu yake akagundua kuwa ilisha katwa muda
mrefu , oooh shit!!! Ndio neno li lilo mtoka.Helman
Akaondoka kwa mwendo wa haraka kuelekea
walipo wenzie walio kuwa wanajiburudisha na
warembo alifika huku akihema na kuzungumza
kwa
jazba…
“Jamani mpango wetu unaanza kuharibika yani
kama huyu jamaa ameotea dili vile au kuna mtu
kamvujishia huyu eeh?
Wote walihamaki! Na mmoja wao kuuliza kwanza
kafanyaje kwasababu leo si ndio tumepanga akija
tumalize kila kitu na tujue mchongo tuna useti
vipi?
“Alfred amekataa kuja na kasema kuwa hataki
urafiki na mimi maana mimi sio rafiki mzuri kwa
maneno haya huoni kama kanishtukia? Helmani
alizungumza na kuendelea kusema kwa hasira
huku akipigapiga mikono yake kwenye meza.
wakataka kuharibiana wenyewe ndipo walipo
kubaliana wafanye jambo.
****************
Nilipo kuwa naomba radhi kwa mama David
ghafla
muito mfupi kwenye simu yangu uliita nilipo
angalia nikakuta ni namba ngeni imenitumia
ujumbe nilishikwa na woga nilipo ona ujumbe ulio
andikwa,,,
“KAZI YETU KWAKO HAIJAISHA MPAKA LENGO
LETU LITA KAPO TIMIA”
kisha mbele akaandika maneno yalio ashiria
kucheka,,,
”hahahaha!!!!!!!”
Nilipigwa na butwaa hali iliyo mfanya mke wangu
mama David kuwa na wasiwasi naye akaichukua
ile simu na kusoma ujumbe ule, kabla hajamaliza
ghafla hodi ikawa inagongwa kwa nguvu sana
wote
tulizidi kushikwa na woga kila mmoja aliwaza
huenda ni Yule aliye tuma ujumbe ule wa vitisho?
lakini hatukuwa na uhakika tukajikuta
tumesogeleana na bahati nzuri Nisha na David
kila
mmoja alikuwa chumbani kwake hivyo
hawakuweza kujua kile kilichoendelea pale
sebleni.
Ikabidi nijikaze na kumwambia mama David
alekee
chumbani maana hatujui nani anaye gonga majira
yale ya usiku na hatukuwa na mazoea ya ugeni
wa
usiku bila taarifa na getini amepita vipi mtu huyo
anaye gonga mlango nilitazama huku na kule
nikakuta mchi wa kinu kidogo nika uchukua
nakuelekea mlangoni hakika sikuamini nilicho
kiona
mbele ya macho yangu
Nguvu ziliniishia na ule mchi mdogo nilio ushika
ulianguka chini kisha nikashusha pumzi ndefu,
kumbe alikuwa ni Sagu kijana ambaye alikuwa
anasimamia ujenzi wa nyumba yangu hii ninayo
ishi sasa hapa gairo ambayo niliamua kuijenga
kwa siri na huku mbali kwa sababu kama
kampuni
ingejua najenga wangeanza kunifuatilia na kuhisi
huenda nikawa naihujumu.
Basi nilimkaribisha japo aliuliza maswali ya hapa
na pale mbona na hema kiasi kile na nimeshika
mchi kama navizia kitu fulani cha hatari lakini
nilimpa majibu yalio mlizisha na hakujua kilicho
kuwa kina endelea kwa muda huo, hivyo tuliketi
na
kuanza mazungumzo,,,,,
“Sagu mbona usiku na bila taarifa? Nilimuuliza
”aisee bosi samahani kwani nilijaribu kupiga simu
yako ila mtandao ulikuwa unasumbua” alinijibu
Nikamtazama kwa makini lakini kila nilipo taka
kumuliza swali getini aliingiaje mdomo wangu
ulikuwa mzito niliwaza mambo mengi kichwani
mwangu kwa muda mchache nilio kuwa na
mtazama mpaka sauti ya mke wangu Magrety
iliposikika kutokea chumbani ,,,,,
”Eeh shemeji umekuja saa ngapi? Alimuuliza Sagu
kwa kuzuga
“Muda mrefu shemeji yangu wazima hapa? sagu
Alijibu na kuuliza hali
“Sisi wazima mnatunyima nini huko?Magrety
aliuliza huku akiweka kisura cha kujichekesha
asishtukiwe kama alitoka kwenye hofu
“huko tuta wanyima nini zaidi ya mvua
zinazoendelea kunyesha na viazi kuzidi
kunawaili”?
Baada ya mazungumzo hayo mafupi Magrety
alinyanyuka na kwenda kumuandalia chakula
Sagu
nasi tukawa tunaendelea na mazungumzo,,,,
“Mmh Sagu niambie ujio wako kama unautofauti
na siku nyingine?nilimuuliza
“hapana bosi ni ulele tu vifaa vya ujenzi
vimepungua hivyo nime ona bora nije ili
nimalizane
na wewe ukabidhiwe nyumba yako baada ya
muda
mfupi”alinijibu
“basi hakuna shida kesho nitakupatia fedha ili
ukaendelee na ujenzi” nilipo mjibu nikanyanyuka
na
kumuaga na kumtakia usiku mwema wakati yeye
akielekea kula na kwenda kwenye chumba cha
kumpumzika maana alikuwa sio mgeni.
Usiku nilipata usingizi wa mang’amu ng’amu
sana
niliwaza kila neno ambalo mke wangu aliniambia
na kuufikiria zaidi ule ujumbe nilio tumiwa, mke
wangu alizidi kunionea huruma kwa hali ilivyo
badilika ghafla kutoka kwenye furaha mpaka
kufikia huzuni ambao hata yeye hakutegemea kwa
muda ule kama ungeweka makazi ndani ya mioyo
yetu, ila kinywa chake hakikusita kutamka
maneno
haya ambayo yalimpendeza mungu,,
“mme wangu kesho tukiamka salama tuelekee
kanisani tuka fanye maombi maana hali ina anza
kuwa tete”
Hakika nilijikuta nikimporomoshea mvua nyingi ya
mabusu usoni mwake kisha nikamueleza,,
“mke wangu wewe ni mwanamke ambaye
umetumwa kuja kunibadilisha mimi katika dunia
hii
na kunipa faraja ambayo wengine wanaikosa
nakushukuru sana mama David” nilizungumza
maneno hayo huku uso wangu ukionesha
masikitiko makubwa kwa yote niliyo yafanya
nyuma.
Mke wangu akanisogelea taratibu na kuniangalia
kwa sekunde kadhaa usoni kisha akaachia
tabasamu la kimahaba na kulaza kichwa chake
juu
ya kifua changu ,
kutoka kwenye tabasamu lile niliweza kuhisi
alichofikiria huenda hakuamini kama nimeamua
kubadilika kwa muda mfupi kiasi kile.
kule kumisi kulala mapema na mimi kulimfanya
apitiwe na usingizi mapema lakini kwangu ilikuwa
tofauti mpaka kulipo kucha baada ya kumshwa
na
jogoo la kwanza.
Tuliamka wote tukajiandaa na kuibeba familia
yangu kwenye gari yangu aina ya BMW230 safari
ikawa kuelekea kanisani kama mke wangu alivyo
nishauli lakini kabla hatuja fika nilimshua Sagu
njiani ambaye pia tuliongozana nae kutoka
nyumbani na kumpatia kiasi cha fedha kwa ajili
ya
vifaa vya ujenzi na nauli ya kurudi Morogoro.na
baada ya muda tukawa tumefika kanisani ibada
iliendelea vizuri ila tulikaa mabenchi tofauti mimi
na mke wangu, na watoto wetu walienda kukaa
na
watoto wenzao kwa kuwa tulikuwa tumechelewa
hivyo mabenchi mengi yalikuwa na nafasi chache.
Wakati ibada ikiendelea nilihisi kutekenywa na
kitu
mfukoni nilipo toa ilikuwa ni simu yangu ambayo
niliweka muito wa kimyakimya ili isipige kelele
tukiwa ibadani, macho yangu yalipigwa na
bumbuwazi kuona tena namba ngeni ikiwa
imetuma ujumbe ambao nilianza kuwa na
mashaka
nao, ujumbe wenyewe ulisomeka hivi,,
“TUKO NJE TUNA KUSUBIRI UKITOKA UJE
KUCHUKUA MZIGO WAKO”
Maneno hayo kwa kweli yalizidi kuniogopesha
maana nikagundua kuwa kuna watu wameanza
kunifuatilia kama ni swala la kwenda kanisani
mawazo tulipata usiku mimi na mke wangu ndipo
tukaamua kuwaanda na watoto wetu tukaja
kanisani sasa wamejuaje kama tupo kanisani
moyo
ukaanza kuingiwa na wasiwasi juu ya Sagu.
Nilishindwa kuvumilia kukaa ndani ya kanisa
hivyo
nikatoka kwa mwendo wa haraka hali iliyo
wafanya
walio karibu nami kunishangaa maana
nilionekana
kama mtu aliyechanganyikiwa huku nikiwa na
bonyeza vitufe kutafuta namba ya Sagu nilivyo
fika
tu nje ikawa tayari inaonekana mbele ya mboni
zangu hapo mkono wangu ukaanza kubonyeza
kile
kitufe cha kijani kumpigia sagu na kuweka simu
sikioni nilizidi kushikwa na hasira baada ya
kujibiwa,,,,
”Ndugu mteja namba unayopiga kwa sasa
haipatikani jaribu tena baadae”
Nilipiga zaidi ya mara nne na jibu likawa lile lile
na
mawazo ya ule ujumbe wa kwanza ukawa kama
umenitoka kwa muda kichwani baada ya
kuchanganywa na muhudumu aliye nijibu wakati
nikiwa na mpigia Sagu, sikuwa na jinsi ilinibidi
nichukue maamuzi ya kutaka kurudi tena ndani
ya
kanisa,nilivyo piga hatua tatu kabla sijaukalibia
mlango wa kanisa ujumbe mwinigine ukaingia
hapo ulinifanya nigeuke nyuma na kupepesa
macho
yangu pande zote kama nitamuona yoyote
ambaye
anafahamiana na mimi huenda nikamjua huyu
anaye nitumia ujumbe usio eleweka kama huu
uliongia na kunieleza kuwa……..
“VIPI IBADA IMEISHA MBONA UMEWAHI
KUTOKA?”
Hapo sikuchelewa tena nikapiga haraka namba
hiyo iliyo nitumia ujumbe bahati nzuri ikawa
imepokelewa mdomo ukawa na kihere here cha
kuongea,,,
”Hallo? Hallo?
Hallo?hallo?
nikajikuta naongea peke yangu, nilipo toa sikioni
kuingalia ilikuwa bado ipo hewani nilizidi
kuchanganyikiwa mpaka nikaanza kujuta kwanini
nilienda kanisani na familia yangu maana
imeshaonekana ni hatari inayo taka kunikumba
lakini ghafla nikasikia sauti kwa mbali ikiongea
ndipo nilipo weka tena simu sikioni,
Hallo? Nilizungumza na bahati nzuri muhusikia
naye alianza kuzungumza ila nilishtuka baada ya
kusikia ananza kutaja jina langu tena ilikuwa ni
sauti ya kike,,,
“Hallo mr.Alfred kazinge”? alizungumza nami
sikutaka kupoteza muda nikamjibu kwa sauti ya
ukali bila kujali eneo nililopo
“Wewe ni nani na unataka nini toka kwangu”?
Nilihamaki
”hahahahaha” alicheka kwa dharau kisha
akaendelea kujitambulisha
”haina haja ya kunijua jina maana haito saidia
cha
msingi toka hapo ulipo na sogea mbele utakuta
kuna gari aina ya range nyekundu imepaki uje
kuchukua mzigo wako.
Nami nilifanya kama walivyo niagiza ilinibidi
nielekee mahali nilipo elekezwa, mwendo wa
hatua
kadhaa tu ulinifanya niwe nimewasili eneo lile na
nilipokuwa nashanga shanga mara kioo cha gari
lile aina ya range kikashushwa na mkono
ukaonesha ishara ya kuniita nikasogea mpaka
kwenye dirisha lile lakini aliyetoa kichwa chake
nje
huku uso wake ukiwa umefichwa na miwani meusi
hakua mwanamke kama sauti niliyo isikia kwenye
simu, alikuwa mwanaume tena aliye kuwa
amekomaa sana kwa mtazamo.
Nilipotaka kujua kama kuna mwanamke mle ndani
iliniweze kumuuliza anashida gani na mimi, nafasi
hiyo nilinyimwa baada ya kukabidhiwa bahasha
kubwa ya kaki iliyo kuwa imetuna kiasi kisha gari
hilo kuondoka kwa mwendo kasi sana lakini nilipo
taka kuifungua bahasha hiyo ilinijue kuna nini
nilishtushwa na breki iliyo kuwa imebanwa ghafla
kama vile dereva anayetaka kukwepa ajali ya
kugonga, hivyo uso wangu ulibidi utazame
kwenye
gari lile ila nilicho kiona ni yule jamaa aliye
nikabidhi ule mzigo akitazama nyuma yangu huku
akitingisha kichwa chake kama amegundua kitu
fulani hivi.
ITAENDELEA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni