Jumatatu, 15 Juni 2015

SAHIHI YA KIFO

 SEHEMU YA NNE

Nilipotaka kujua kama kuna mwanamke mle ndani
iliniweze kumuuliza anashida gani na mimi, nafasi
hiyo nilinyimwa baada ya kukabidhiwa bahasha
kubwa ya kaki iliyo kuwa imetuna kiasi kisha gari
hilo kuondoka kwa mwendo kasi sana lakini nilipo
taka kuifungua bahasha hiyo ilinijue kuna nini
nilishtushwa na breki iliyo kuwa imebanwa ghafla
kama vile dereva anayetaka kukwepa ajali ya
kugonga, hivyo uso wangu ulibidi utazame
kwenye

gari lile ila nilicho kiona ni yule jamaa aliye
nikabidhi ule mzigo akitazama nyuma yangu huku
akitingisha kichwa chake kama amegundua kitu
fulani hivi. Nilipogeuka alikuwa
Ni mama David na David hapo akili yangu ikabidi
ichekeche kwa haraka na jibu nililo pata ni
kwamba
yule jamaa atakuwa amejua kuwa hii ni familia
yangu na nilipo mgeuzia shingo kwa mara ya pili
nilizidi kuogopa baada ya kumuona
ametengeneza
umbo la bastola kwa kutumia kiganja chake cha
kulia na kuonesha ishara kuwa atawashuti, kisha
gari hilo likaacha vumbi na kuishia zake,hata
hamu
ya kutaka kujua kilichopo kwenye ile bahasha
sikuwa nayo nilicho kifanya ni kwenda kumshika
mkono David na kumwambia Magrety
akamchukue
Nisha tuondoke nyumbani ila kwa hasira nilitaka
kumchapa vibao Magrety kwa maneno aliyo
niambia,,,,,,,,
”mume wangu tatizo nini mbona ibada haija
isha”?
“fanya kama nilivyo kuambia kamchukue nisha
haraka macho huna hata sauti husikii?
Niilizungumza kwa sauti ya ukali bila kujali kuwa
baadhi ya watu walikuwa wana tutazama
Magrety hakukaidi agizo hilo, walipo wasili tu
niliwasha gari safari ikawa kuelekea nyumbani
hakika mwendo nilio kuwa naenda nao kama
askari wa barabarani wangeniona wasingee sita
kunikamata niliwakosakosa kuwagonga watoto
wenye tabia za kucheza barabarani lakini
nilimshukuru mungu baada ya kufika salama.
Mimi na mke wangu tukaelekea chumbani huku
nikiwa nimeshika ile bahasha mkononi na kina
David kuwaacha sebuleni baada ya kuwa
nimemuonya David asithubutu hata kunyakua
mguu wake kuutoa nje pia amuangalie Nisha
asicheze mbali naye nilifikia kukaa juu ya kitanda
huku mama David akiwa ana lalamika mwenyewe
“maisha gani haya tunayoanza kuishi?
”Hatuna amani nayo kabisa au kuna mtu
umemkosea mme wangu? Aliniuliza .
”Hakuna mtu niliye mkosea wala kumdhulumu
haki
yake mimi mwenyewe na shangaa haya yanayo
tokea ghafla hivi!!! ila yote ni mitihani tu katika
maisha mke wangu inabidi tupambane nayo sio
wote watakao kupenda wengine ni wanafiki”
Ilibidi niwe mpole na kusimama kama mwanaume
kwenye nyumba maana mke wangu asije
kupoteza
dira kabisa hata ya kutoa mawazo kama na mimi
ningeamua kunyong’onyea.
Baada ya kumuona kidogo anaanza kutulia
nikaichukua ile bahasha na kuanza kutaka
kuifungua ila mke wangu akauliza,,
” kuna nini humo”?
”Ngoja tufungue kwanza ili tujue kuna nini”
nilimjibu
Nikatoa gundi iliyo kuwa imebandikwa kama
kufuli
ya bahasha na kilichokuwa ndani kila mmoja
alishika mdomo, tulitazamana kwa mshangao
kisha nikaingiza mkono ndani ya ile bahasha
nilicho anza kutoa yalikuwa ni maburungutu ma
tano ya fedha mpya na kila burungutu lilikuwa na
kiasi cha milioni tano hivyo jumla yalikuwa yana
thamani ya milioni ishirini na tano
”Nilijiuliza fedha hizi ni za nini? Wakati huo mke
wangu alizidi kupagawa na macho yalimtoka na
kuendelea kutazama ile bahasha.
Nilipo ingiza mkono mara ya pili nikatoa karatasi
iliyo kuwa imeviringisha kitu fulani kigumu na
nilipoikunjua mapigo ya moyo yaliongeza kasi na
mke wangu alinyanyuka pale kitandani tulipo
kuwa
tumeketi kwa mshtuko na kusema kwa sauti ya
mshangao,,,,
”aaah bastola”? Yesu kristu balaa gani hili mume
wangu? Aliuliza maswali yasiyo kuwa na majibu.
Niliishika bastola ile kisha kuigeuza geuza zaidi
ya
mara mbili baadae nikagundua kuwa karatasi ile
iliyoviringisha bastola ilikuwa na maandishi yalio
nipa maelekezo juu ya ile bahasha,,,,,,,,
”HIZO FEDHA NI KIASI CHA AWALI KABLA YA
KAZI
TUNAYO TAKA KUKUPA, NA KAZI ITAKAPO
KAMILIKA UTAMALIZIWA KIASI KAMA HICHO PIA
HIYO BASTOLA SIO KIFAA KITAKACHO TUMIKA
KATIKA KAZI YAKO ILA UTAKITUMIA KUIMALIZA
FAMILIA YAKO KWA MKONO WAKO MWENYEWE
KAMA UTAKAIDI AGIZO LETU.
ITAKAPO FIKA SAA 4:30 USIKU NJOO TUKUTANE
PALE LANDMARK HOTELI YA RIVERSIDE
UBUNGO.KWA MAZUNGUMZO ZAIDI BILA
KUSAHAU
HIYO BASTOLA ”0768606510 NDIO NAMBA
UTAKAZO TUMIA KUTUTAFUTA UKIFIKA.
Ujumbe huo nilio kuwa na usoma kwa sauti ili
mke
wangu pia asikie ukazua taflani kwa muda huo
baada ya mke wangu kupandwa na hasira na
kuanza kunipigapiga na mikono yake kifuani huku
akilia na yote hayo ni kwasababu ya upendo
alionao kwa watoto wake,,,,
”sitaki mimi Alfred hayo mambo yako kama
ulikuwa unafanya na wenzio mmalizane wenyewe
sio kutuingiza na sisi watoto wangu nawapenda
sana”
Alilalamika kwa muda kisha kuondoka chumbani
kwa hasira na kwenda kwa watoto wake nami
nilibaki chumbani nikiendelea kufikiria ni kwanini
yanatokea haya kuna nini nilicho kifanya kwa
mtu?
Japo mawazo yakawa yananijia na kuanza
kumshtumu pia Helman lakini kila nikijiuliza mara
mbilimbili ni kipi nilichomkosea sikupata jibu na
kama kukataa mimi na yeye tusiwe marafiki ndio
anifanyie hivi mbona mambo yanayo nitokea ni
makubwa kuliko hilo la urafiki? Hayo ndio
mawazo
yalio kuwa yana zungukazunguka ndani ya
kichwa
changu.
Magrety alishinda na watoto wake siku nzima bila
kurudi chumbani wala kuniita kwenye chakula
japo
hata kama angeniita nisinge weza kula maana
yalio nikuta kwa muda mfupi nilihisi kushiba,
nami
nilishinda ndani mpaka kiza kika ingia nilipo
tazama saa yangu ikawa inaniambia ni saa 3:30
usiku hivyo nikaona muda huo unanifaa sana
kujiandaa ili kwenda kuonana na wapuuzi nisio
wajua. Maana kutoka magomeni mpaka maeneo
ya ubungo ningeweza kumudu foleni kwa muda
huo.wa usiku.
Nilipo maliza tu kujiandaa nikachukua biblia
yangu
kisha kupiga magoti chini ya kitanda na kuanza
kumuomba mwenyezi mungu..
.
”eeh Mungu baba mimi kijana wako nina nyoosha
mikono yangu kwako kwa kuwa wewe ndio unaye
jua vinavyo onekana na visivyo onekana naomba
unilinde mimi na familia yangu,umlinde mke
wangu
kipenzi na huko niendako naomba nirudi salama
maana sijui ninacho endea ila ni katika hali ya
kuilinda familia amin,
Baada ya sala hiyo fupi nilirudiaha biblia yangu
kabatini kisha kuchukua ile bastola na kuiseti
vizuri.
wakati naendelea na kitendo hicho Magrety
akaingia, alishtushwa na kitendo nilicho kuwa
nakifanya maana usoni mwangu nilisha tengeneza
v na kama alijua nilichokipanga vile kwamba
kama
kuna mtu atanilitea ujinga na muua hapo hapo.
Magrety alinisogelea na kunieleza
”Nakuomba mume wangu usiende huko tafadhali
tupige simu kituo cha polisi kwanza kama kwenda
basi uende na maaskari”
kipindi hicho wakati anazungumza hasira zake
zilikuwa zimemuisha na kwa bahati mbaya
kukasirika kwake kwa mara ya kwanza ndiko
kuliko
nifanya nijitolee maisha yangu kwenda huko kama
kufa ni kafe maana najua nitakufa kishujaa kwa
kuilinda familia yangu kama baba anaye jali na
kuipenda familia.
Nilipo kuwa nataka kutoka Magrety akawa
ananikataza nisiondoke nilicho, kifanya nika
msukumia kitandani huko na kumpa onyo asipige
simu kituoni maana hatuwezi jua kuwa hao jamaa
wana nia gani na wameweka mitego gani hivyo
tuna weza kuongeza tatizo badala ya
kulipunguza.
kisha nikatoka mle chumbani na kumuacha
Magrety akilia kilio cha kwikwi nami nikaanza
safari ya kuelekea huko,
wakati nimeshika komea la mlango wa kutokea
nje
nikakumbuka kitu kichwani ilinibidi nielekee
chumbani kwa Nisha nikambusu shavuni wakati
akiwa amelala kisha kwenda na chumbani kwa
Davidi pia alikuwa amesha lala nilimshika
kichwani
na kumuambia maneno ya kiume,,,,
”David wewe ndio kidume changu cha baadae na
kiongozi wa famila hii mungu aendelee kuku kuza
na ukuwe salama ili baadae uje kulinda familia
yako kama mimi leo ninavyo jitolea maisha yangu
juu yenu”
Nilirudi vyumbani kwao kuwaaga maana sikujua
huko ninako kwenda kama nitaweza kurudi hai
au maiti, baada ya hapo safari yangu ikawa
imeiva
sasa nilitoka na kuwasha BMW230 yangu
kuelekea huko na ndani ya dakika kadhaa nikawa
nimefika eneo husika nikatoa simu yangu na
kuanza kubonyeza vile vitufe husika kama namba
ilivyo kuwa inajieleza 0768606510 nika piga na
simu ikaanza kuita na baada ya sekunde tu
nikasikia sauti niliyo ifahamu kabisa
Ikisema hallo??!!
Nilipo mjibu kuonesha kwamba ninamskia
alinipatia maelezo,,,
”Alfred subiri hapo hapo nimeshakuona”
Nilitamani kumuita jina lake ili nijue kama ni yeye
au nimefananisha sauti, tatizo simu ikakatika
ghafla,nilipo itazama ilikuwa imekatwa kusudi,
Niliendelea kusubiri kama alivyonielekeza huku
kichwani na mimi nikipanga maarifa yangu
nifanyeje kama litatokea tatizo juu ya uhai
wangu.
Baada ya dakika kupita sauti za viatu zikawa
zinasikika zikinisogelea nilipotazama mbele
nikaona warembo wa wili walio panda kiasi,wenye
shingo ndefu na nyembamba zilizo pambwa na
mikufu ambayo ni ghari kununua pia hata miili
yao
ilikuwa ni myembamba japo kuanzia kiunoni
walitenga kiasi kwa vijana wa sasa wanawaita
umbo namba nane.
walivaa nguo zilizo fanana, makoti mafupi yenye
rangi nyeusi pamoja na vimini, .mikono yao
ilivalishwa gropsi zilizo fanana na rangi ya
makoti
yao sura, zao zenye weusi uliong’a
uliwatambulisha kuwa wao ni waafrika halisi,
sura
hizo ni kazi kuzitofautisha kama huja zizoea.
Nilishangaa walivyo jigawa, mmoja akakaa
upande
wangu wa kulia na mwingine kushoto hapo
uvumilivu ulinishinda ikabidi niwaulize kwa ukali
ili
kujihami,,,,,
”nyie ni wakina nani”?
Twin killers(mapacha wauaji) walinijibu huku
wakiwa wameweka sura ya ukatili
”Kwa hiyo mnataka nini sasa”? niliwauliza nami
kwa ukatili maana nilijua wanawake ni waoga
hivyo wanaweza kutishika lakini kumbe ndio
nikawa nime wachochea, wakanishika mikono
yangu yote wakiwa wamegawana kila mmoja na
upande wake.
Nilipojitikisa kwa nguvu zangu zote ili waniachie
kumbe bastola yangu niliyokuwa nimeiweka kwa
nyuma walisha itoa bila mimi kujua na kuniwekea
kichwani,,, moja alizungumza,,
”Songa mbele haraka we kijana”
Kutokana na jinsi alivyo zungumza kile kiswahili
chake nikaanza kuhisi kuwa hawa si watanzania,
wakanikukusa hivyo hivyo huku nikiwa na weka
hali ya ubishi mpaka tulipo fika nyuma ya ile
hoteli
ambapo kulikuwa na meza moja iliyo jitenga
kwenye maua mengi marefu na mwanga hafifu
wa
taa zenye rangi tofauti,na kulikuwa na bwawa la
kizungu pembeni(swimming pool)
Meza hiyo ilikuwa imezungukwa na watu wapatao
saba walio shiba vilivyo wote wakiwa wame
simama kumzunguka mtu moja ambaye yeye
aliketi kwenye kiti nikahisi huenda huyu ni bosi
wao nikaanza kuogopa,
Sauti ya kofi ilisikika kutoka kwa yule jamaa aliye
keti na kuwaambia wale madada kwa lugha nilio
weza kuitambua kuwa ni kinyaruanda, ila siku
bahatika kujua maana ya yale maneno.
baada ya ishara hiyo ya kofi wakaniachia kisha
nika sogezewa kiti nami nika keti pamoja nae.
Alinitazama kwa dharau halafu akachukua simu
yake iliyo kuwa juu ya ile meza na kupiga, sikujua
ni nani aliye kuwa ana mpigia ila alisema,
”hallo? eeh tumesha muandaa” kisha aka kata
simu
Ndani ya muda mchache nilishtuka baada ya
kuguswa bega kwa nyuma nilipo geuka alikuwa ni
Helman, nilinyanyuka kwa kuhamaki nikarudia
kumuita tena,
”Helman ni wewe unae nifanya kukosa furaha
mimi
na familia yangu?
Alicheka kisha akasema,
”Alfred raha unajinyima mwenyewe wewe na
familia yako mbona tulivyo kuwa marafiki
haukukosa amani”?aliniuliza lakini sikumjibu.
ITAENDELEA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni