SEHEMU YA NANE
Mama muksini alimnyakuwa david pale alipo kuwa
amepiga magoti na baadhi ya wazee wengine
wakaja kumsaidia kisha waka mchukua david na
kwenda kumbembeleza mama muksini nae
hakuwaacha nisha na dasoni hivyo nae alienda
kuwa bembeleza, kiukweli mama muksini alitokea
kuwa penda sane watoto hao.
Maturubai yaliweza kufungwa watu wakawa
wamejigawa wanawake upande wao na wanaume
upande wao, stuli iliwekwa njia panda ya kwenda
sehemu ya wanawake na wanaume hao kisha
kiungo kidogo maarufu kama kitunga kiliwekwa juu
yake kikiwa na picha nyingi za marehemu mama
david ambazo zilipigwa alama x kumaanisha kuwa
huyu ndie marehemu aliye fariki,
wengi wasio mjua marehemu walipita kwenye stuli
hiyo na kutazama picha hizo wengi walisikitika na
maneno mengi kuwatoka mdomoni mwao hasa
walipo oona picha aliyo piga na familia yake
ambayo aliyo wakumbatia watoto wake vipenzi,,,
“maskini watoto wake hawa wawili wadogo kweli
sijui watakuwa kwenye mazingira gani? Alikuwa
anajisemea mmama moja ambaye alikuwa
akitazama picha hizo.
Muda ulivyozidi kwenda mkusanyiko ulizidi kuwa
mkubwa hasa kwa habari zilizo zidi kusambaa
kuwa amefariki kwa kipigo japo wengine
walizungumza mengi ambayo yasio na ukweli
kama vile, alifumaniwa ndio sababu ya kupigwa,
lakini hayo yalikuwa ni maneno ambayo hutokea
kwenye mkusanyiko wa watu au jambo ambalo
lina utata. Ila walio jua walitulia tu wakitafakari
msibao huo na nini cha kufanya.
Wazee wakaribu na marafiki wa mzee kazinge
waliitana na kuweka kikao kutaka kujadili taratibu
za mazishi bila kumsahau david pia alijumuishwa
katika kikao hicho maana alishakuwa mtu mzima
na alikuwa na uwezo wa kutoa maamuzi au
kupinga jambo ambalo ataona si bora kufanyika,,,,
“Ndugu zangu tumekusanyika hapa ili tuweze kujua
tunafanya nini juu ya msiba huu ambao umemfika
mwenzetu wa kufiwa na mkewe na matatizo
ambayo yeye yamemkuta wengi tumesikia sikia juu
juu tu kama amekamatwa na polisi na yupo kule
kwenye kituo kidogo kwa kosa la kumsababishia
mkewe kifo jambo hilo ni kweli kwa maelezo
ambayo tumeletewa na mwanamke
huyu,,alimuonesha mama coolin.
“ ambayo yeye aliyapata toka kwa daktari walivyo
kwenda jioni hii kwa ajili ya kupeleka chakula na
hata waliweza kushuhudia maiti ya mama davidi
ikipelekwa sehemu maaulumu ili kuuhifadhi mwili
huo, mpaka taratibu zitakapo kamilika na kwenda
kuchukuliwa kwa ajili ya mazishi†alizungumza
mzee nyomolage ambaye alichaguliwa kuwa
mwenyekiti wa kikao hicho kutokana na ukaribu
alio kuwa nao kwa mzee kazinge.
“na kama mnavyo jua ndugu yetu mzee kazinge
tumeishi nae hapa kwa miaka mingi sana na hana
ndugu hapa na hakuna anayejua mawasiliano yao
jambo tunalo lijua sisi in kuwa wazazi wake
walikuwa wanaishi mkoani tanga na walisha faliki
muda mrefu hivyo sisi ndio tumekuwa ndugu zake
hatuna budi kubeba majukumu haya ili
tumpumzishe mkewe mahali salama hata uko
atakapo kwenda basi ahisi kweli alikuwa anaishi
na binaadamu na sio watu na sasa nafikiri kikao
kimeanza rasmi tuweze kusikia mawazo yenu
tuyapatie ufumbuzi kwa haraka†hayo yalikuwa
maneno ya mzee nyomolage ambaye alizidi
kuonesha utu kwa familia ya mzee kazinge.
Kidole cha kwanza kilikuwa ni cha mama coolin
ambaye alianza kwa kuchangi yanayo hitajika
hospitali, alijifikicha macho yake kwanza na sauti
iliyo karibia kukauka kutokana na kulia sana
ilianza kuzungumza,,,,,
“jamani wakati tunampeleka mgonjwa hospitali
hatukuweza kulipa chochote kile in msaada tu
tulifanyiwa na yule daktari kutokana na hali ya
marehemu ilivyo kuwa mbaya hivyo kuna kiasi cha
fedha tunadaiwa ndipo pia tunaweza kuchukua
mwili wa marehemuâ€wazo hilo la mama coolin
lilisikilizwa na ufumbuzi ukatolewa na mtu
akateuliwa kwenda kukusanya michango kwa
waliohudhulia msibani.
“pia me nafikiri tungeweza kwenda kuomba ili hata
mzee kazinge aje kumzika mkewe na kuona nana
na familia yake huku akisindikizwa na akari nahisi
tuna weza kukubaliwa kwa hili maana si mnajua
kule alipo anaweza asitoke mpaka siku ya kwenda
mahakamani na nchi yetu mnaijua hii sio chini ya
miaka mitatu utasikia bado wapo kwenye
uchunguzi†hilo lilikuwa wazo la mzee kombo.
Mawazo hayo yalijadiliwa na kupatiwa ufumbuzi na
baadhi ya watu walichaguliwa ambao kesho ikifika
salama basi watajigawa wengine watakwenda
kulipia gharama za matibabu na kuuchukua mwili
wa marehemu ambapo hata bajeti ya jeneza ilisha
pigwa kutokana na kiasi cha michango kilicho
patikana jioni hiyo iliyokuwa inaelekea magharibi
na wengine watakwenda kuonana na mkuu wa
kituo cha polisi ili mzee kazinge aweze kwenda
kuhudhulia mazishi ya mkewe na kwenda kuwaaga
familia yake na watakao baki watabaki kuchimba
kaburi ambalo david alipendekeza lichimmbwe
nyuma ya nyumba yao, na muda wa mazishi
ulipendekezwa utakuwa na saa kumi na nusu jioni
na watu wakatangaziwa yote yaliojili kwenye kikao
hicho.
Mpaka kikao kinaisha watu waliweza kula kisha
kila mmoja kujichukulia nafasi kwenye turubai na
kuweka ubavu wake na wengine wakiendelea
kuombeleza.
***************************
Sauti zile za mapambio zilizo kuwa zinaimbwa na
wana mama ziliweza kuwaamsha walio lala pale
nje kwenye maturubai na kuwa fanya waanze pilika
pilika za kujiandaa ili kila mmoja ashike njia ya
kwenda sehemu husika kukamilisha mambo
aliyokuwa amepangiwa ndani ya saa kuminambili
hiyo asubuhi,
Baada ya wote kukusanyika safari ikaanza
kuelekea kituo cha polisi na hospitali, kwa bahati
nzuri wote wakawa wamefanikiwa wale wa
hospitali kuupata mwili wa marehemu na
kuuhifadhi kwenye jeneza ambalo wali linunua nje
ya hospitali karibu na jengo la kuhifadhia maiti
kisha kurudi nao nyumbani na wale wa kituo cha
polisi waliambiwa abaki mmoja ambaye watarudi
wote ma gari la polisi mpaka kwenye mazishi.
Ilipofika mishale ya saa tisa maandalizi ya
kuuwaga mwili wa marehemu yaka andaliwa na
mapambio yakaanza kuimbwa na wanakwaya
ambao walialikwa na padri nae akawa anafungua
biblia yake kutafuta maandiko matakatifu ambayo
ataweza kuyasoma kwenye hadhara hiyo iliyo
kusanyika msibani hapo na baada ya muda
aliweza kuyapata na kwaya ikasimama na
maandiko matakatifu ya kaanza kusomwa,,,,,,,
“kwa jina la baba na la mwana, alitoa ishara ya
msalaba kisha kuendelea,hakika kila mpandaji
mazao atavuna kile alicho kipanda na bwana
mungu wetu leo amevuna kwenye familia hii ya
mzee alfredy kazinge ili kukamilisha kazi yake
kutokana na tukio hili na maana ya sisi
kukusanyika hapa ili tujifunze kuwa na sisi siku
moja tutalala hapa mbele na kusomewa kama
huyu marehemu ndugu yetu magrety john
tumuombe bwana mungu wetu atuepushe na
madhambi ambayo tuna yafanya aminaâ€
padri alimaliza kutoa neno na funzo kwa walio hai
ili waweze kujifunza kupitia mwili wa magrety
ambao uliwekwa mbele pamoja na picha yake
kubwa aliyo kuwa ameipiga enzi za uhai wake,
wakina david pamoja na wadogo zake walinyolewa
vipala kama wafiwa na kuvaa nguo zao nyeusi
kisha kuketi kwenye viti vya mbele ambavyo
viliandaliwa na kutazama jeneza lala mama yao.
Padri aliweza kutoa ruhusa ya kuungalia mwili wa
marehemu magrety kwa mara ya mwisho ili
kuelekea kwenye njia ambayo inaweza kumpeleka
motoni au peponi kutokana na matendo aliyo kuwa
anayafanya enzi za uhai wake.
Watoto wa marehemu waliweza kushikiliwa katika
kipindi hicho kigumu cha kuuaga mwili wa mama
yao kipenzi, hasa david ambaye alikuwa anafikilia
mambo mengi kama mzigo ambao alio achiwa wa
kulea familia akiangalia ndio kwanza ametoka
kumaliza kidato cha sita na matokeo hayajatoka
na kazi hana jambo hilo lilimuongezea sana
sononeko moyoni mwake,
Waliomshikilia waliianza kushindana nae nguvu
alipo nga’ang’ania kwenye mwili wa mama yake
huku akiushika kwenye paji la uso na kuutikisa
huku akiuuambia,,,
“mama amka mama mi najua umelala tu mama
yangu amka basi utuone wanao tunavyo hangaika
na machozi kututoka kwa huzuni unayo tuachiaâ€
maneno hayo yaliwafanya hata walio mbali
kusogea eneo ambalo walilo kuwa wanaagia mwili
huo baada ya kusikia sauti ya david ikiongea na
maiti tena kwa masikitiko.
ghafla vumbi na upepo mkali ukaanza kutanda
eneo hilo na hali ya hewa ikaanza kubadilika,
mbigu juu ikaanza kuwa nyeusi kutokana na
mawingu yalio kuwa yameanza kutawala ikabidi
zoezi la kuaga lisitishwe na watu wakabeba jeneza
kuelekea nyuma ya nyumba ambapo ndipo kaburi
lilipo chimbwa na hapo watu wakatumbukia ndani
ya kaburi kulipokea jeneza hilo na wengine
wakibaki juu kulishusha kwa kamba ambayo
ilipitishwa pembezoni mwa jeneza hilo.
“baada ya zoezi hilo kukamilika watu walio kuwa
ndani ya kaburi walitoka kisha padri akasoma
harakaharaka kisha kuchukua udongoulio kuwa
kwenye chepeo na kuanza kuumimina juu ya
jeneza hilo ambalo lilishwa tumbukizwa kwenye
kaburi na kumalizia na maneno haya,,,,
“wewe in vumbi na utarudi kuwa vumbi jina la
bwana lihimiliwe†sauti za watu zilisikika zikijibu
amin.
Kisha chepeo lenye udongo kugeuzwa kwa david
naye akachota udongo kabla hajaweka udongo tu
kwenye kabuli alishtushwa na sauti ya gari
lililokuwa linakuja kwa kasi eneo la kaburi hilo
lakini kabla halija simama alimuona baba yake
akiwa na pingu mkononi akiruka kwenye gari kabla
hata ya askari kushuka kwenye gari hilo la polisi
na kuanza kukimbia huku akilalamika kwa sauti
akimuomba magrety amsubiri, lakini kila mmoja
hakuamini kwa alicho kisikia maskioni mwake in
baada ya kusikia mlio wa risasi aliyo pigwa mzee
kazinge na askari aliye dhani kuwa anataka
kutoroka kupitia umati ule wa watu david
hakukubali
Aliuchukua ule msalaba alio kuwa ameushika mtu
aliye mpokea wakati yeye akiweka udongo kwenye
kaburi na ndio ikawa silaha yake, alimtazama yule
askari aliye mpiga risasi ya mguu mzee kazinge na
kuaanza kumfuata kwa kumkimbilia alipomsogelea
alinyakuwa ule msalaba kwa kunguvu zake zote
iliampige nao kichwani lakini jambo hilo
halikufanikiwa baada ya askari wenzie kuudaka
msalaba huo na kumshika david kwa kumbana
mikono yake kwa nyuma,,
Uso wa david uliiva kwa hasira kila alipofikiria jinsi
mama yake alivyo patwa na umauti na matatizo
yalio mpata baba yake, kiukweli mambo hayo yote
yaliweza kumpunguzia david moyo wa ubinaadamu
na maneno yalioufanya mioyo ya maskari wale
kupanda kooni lakini wakuwa na lakufanya,,,
“mtu malize wote sasa si ndio kazi yenu inavyo
watuma kupiga risasi ovyo kwa wananchi wenu?
“elimu yenu inawasaidia nini sasa hakuna mncho
kumbuka juu ya wananchi zaidi ya kuwapa kesi
hata kama hawana hatia nimalizeni kama mnajua
sana kupiga risasi ni uweni nasema piga hiyo risasi
yako mbona unachelewa, fikirieni in mzigo gani
nilio kuwa nao hii yote imesababishwa na nyinyi
kuto kuwa makini na kufuatilia mambo kwa undani
zaidi.â€
Malumbano yaliendelea na baadhi ya watu hawa
kujua lakufanya kutokana na mshtuko wa risasi na
zile vulugu zilizo kuwa zinaendelea pale kaburini,
wengine walikimbia kwa kuhofia maisha
yao,mtawanyiko huo wa watu walishindwa kuelewa
mzee kazinge yuko wapi na hali yake ikoje,
Kumbe baada ya kupigwa risasi ile ya mguu pale
alipokuwa ameangukia aliweza kujivuta taratibu
mpaka kwenye kaburi la mkewe na kujitupa mle ili
wazikwe wote maana alihisi anastahili kufa kwa
mateso anayo yapata kwa miaka yote tena bila
sababu ya msingi.
Watu walirudishwa tena mahali pale lilipo kaburi la
mama davidi baada ya manyunyu ya mvua kuanza
hata davidi aliachiwa na wale askari, hapo ndipo
walipo gundua kuwa mzee kazinge yupo mle ndani
ya kaburi,,,,,
“jamani hii familia kama mungu haioni vile in
misuko suko kila kukicha eeh mungu wasaidie
hawa,,
“Mmh inatia huruma kwa kweli watazame watoto
wake walivyo kuwa na huzuni “
Hayo maneno yaliwatoka watu tofauti katika eneo
hilo na wakati huo wakina mzee nyomolage
walitumbukia ndani ya kaburi na kumtoa mzee
kazinge, taarifa ziliweza kuwafikia mapaparazi
ambao walitoka kwenye kwenye vituo tofauti
tofauti kama vile redio,magazeti na hata wale wa
televisheni ili kukusanya habari hiyo amabayo
walijua kuwa lazima itawapatia pesa ya kutosha
kutokana na uzito watukio hilo picha nyingi
zilipigwa ili kupendezesha magazeti..
Padri aliamrisha wazike maana mvua ilianza kuwa
kubwa watu walimfukia mama david kwa haraka ili
mvua ile iliyo kuwa inanyesha isije ikaleta balaa
lingine wakashindwa kuufukia mwili wa marehemu
magrety.
David alilia sana maana hakuamini kama mama
yake ndio safari yake imefika mwisho,
Wale askari walimshikilia mzee kazinge ambaye
alikuwa anavuja damu kwenye mguu ule ulio kuwa
umepigwa risasi, mama muksini nae hakuwaacha
watoto wake nisha na dasoni.
ITAENDELEA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni