SEHEMU YA SABA
Walikamata mikono yangu na kunifunga pingu
kwa
nyuma baada ya kuigeuza mikono yangu kisha
kunirudisha mpaka ndani kwangu askari wengine
walijigawa kwenye vyumba vingine wakikagua
kama kuna siraha au zana zingine amabazo zina
husiana na ujangili kiukweli nilijisikia vibaya sana
nilipo waona watoto wangu pamoja na mke
wangu
walivyo kuwa wananililia lakini askari hao
hawakujali lolote walishindwa hata kumuhurumia
mke wangu kwa hali aliyo nayo, walikuwa
wakimsukuma kila alipo kuwa ananisogelea na
kunililia,
Sikuweza kujikaza katika hali hiyo nami machozi
yakawa yananitoka kila nikiwatazama familia
yangu ikitapatapa kwa kukosa msaada hata wa
kubembelezwa, maaskari hao walipo maliza
ukaguzi wao walinitoa nje huku nikiwa bado nina
pingu mikononi jambo ambalo lilinifanya nione
aibu
kutokana na wingi wa watu hasa majirani zangu
walivyo kusanyika kushuhudia tukio hilo,
nilipandishwa kwenye gari lao kama ng’ombe
wanao pelekwa mnadani kisha kuondoka kuelekea
kituoni,
Mama David japo na hali yake ile alijaribu
kulikimbiza gari lile kama mwanamke mwenye
kichaa lakini hata hivyo hatua zake
hazikumchukua
mbali na kudondoka chini hiyo ndio ilikuwa mara
ya mwisho kuiona famila yangu na kuwaona kina
David wakimlilia mama yao pale alipo dondoka
chini hata mahakamani hawakuja si kujua
walipatwa na nini huko nyuma.
Mahakama ikatoa hukumu ya mimi kuhukumiwa
kifungo na mali zangu zote kutaifishwa na
kupigwa
mnada ndipo familia yangu ikawa imekuja huku
katika nyumbaa hii niliyo ijenga kwa siri na Dason
alizaliwa huku na hakuweza kunijua baba yake
mpaka nilipo toka gerezani kwa msamaha wa
Rais.
Hata hivyo wakati natoka gerezani nilikutana na
mwanamke mmoja aliyekuwa rafiki wa mke
wangu
ambaye alikuwa anaijua familia yangu vizuri
aliniambia kuwa ana ushahidi kuhusu tukio lililo
kuwa limetokea ambao unaweza ukanisaidia pia
kulipwa fidia au kurudishiwa mali zangu lakini
kikubwa alicho kisema ni kwamba.
“ushahidi huo Helman amesikia kuwa ninao mimi
baada ya kutonywa na mafanyakazi mwenzangu
hivyo ananitafuta kwa hudi na uvumba na mimi
pale hotelini kwetu nilipo kuwa nafanya kazi
nimeacha kwa kuona maisha yangu yata kuwa
hataliniâ€
lakini kabla hajamaliza maongeza nilimuona
katanua mdomo kwa kupigwa na butwaa na
macho yake yakiangalia eneo ambalo mimi nili
lilipa mgongo nilipo geuza shingo nilimuona
Helman ambaye alikuwa ananifananisha hivi na
yawezekana hakuamini kama ningeweza kutoka
jela kwa wakati ule na alionekana
kuchanganyikiwa
baada ya kuniona mimi na yule mama rafiki wa
mke wangu mwenye ushahidi hivyo hatukuwa na
jinsi zaidi ya kukimbia na huko mbele
tukapotezana kila mmoja akapita njia ya peke
yake
ndipo nami nilipo fanya haraka kwenda ubungo
na
kupanda abood ya kuja huku Morogoro.
Hofu yangu iliyo kuwa inanifanya ni mkataze
David
asiende mjini ni kwamba Helman yaweze kana
anajua kuwa mimi huo ushahidi nilichukua kwa
yule mama ambaye anaitwa Magdalena hivyo
japo
si rahisi kumkumbuka David kwa kuwa miaka
mingi imepita na David amekuwa sana lakini
dunia
haina siri yawezekana tu akajulikana na akapata
matatizo makubwa sana zaidi ya haya niliyo
yapata mimi. Hayo ndiyo matukio yaliobadilisha
maisha yangu.
****************************** *********
Baada ya mzee kazinge kumaliza yalio mtokea
mpaka kufikia katika hali ile aliyokuwa nayo sasa
kila mtu alichoka kwa kweli wengi walidondosha
machozi na kumuhurumia hata David akawa
amejua ukatili alio fanyiwa baba yake japo
kumbukumbu ya machache alikuwa nayo akili
mwake lakini kiini cha matatizo alikuwa hakijui
sasa ndio amejua mtoto wa kiume hata Nisha
naye aliye kuwa mdogo kwa wakati ule ameweza
kujua alicho fanyiwa baba yake na Dasoni yeye
ndio amekuwa kama Nisha wazamani asiye jua
chochote zaidi ya kuona kama watu wanasimulia
hadithi za bibi na babu tu,
Ndugu mwenyekiti alivyo taka kuongea neno
alikatishwa na sauti ya mama Coolin ambaye
alikuwa amebeba chakula alicho enda kukiandaa
kwa ajili ya mgonjwa,,,
“jamani tumechelewa kupeleka chakula cha
mgonjwa na sasa yaelekea saa tisa kasoro na
kule
ilikuwa ni saa saba ndio tulitakiwa twende tatizo
kufuata mahitaji sokoni mpaka kuandaa na mikaa
yenyewe ya siku hizi hii ndio imenichelewesha
Davidi mwanangu twende haraka tukaombe
tuingie
hata kama tumechelewa wanaweza waka
tuelewaâ€
David alinyanuka akawa anaelekea kule alipo
mama Coolin ili ampokee kikapu cha chakula na
mzee Kazinge naye akaona si vibaya kwenda
kumuona mkewe japo uso wake ulikuwa bado una
aibu kwa alicho mfanyia mkewe,
Waliongozana wale watatu mpaka barabarani na
kuchukua bajaji kuelekea Hospitali huku wakijadili
ni jinsi gani wanaweza wakalipa ile bili ya
mgonjwa kule Hospitali maana walifanyiwa
msaada kutokana na hali yake kuwa mbaya,
maongezi hayo walienda nayo mpaka yalipo
wafikisha hospitali,
Walifika getini na kumuomba mlinzi awarusu
waingie kutokana na hali walio muacha nayo
mgonjwa halafu alibaki mwenyewe, kwa kuwa
mlinzi naye binaadamu aliwaruhusu na walipo
ruhusiwa tu mama Coolin akawaomba watangulie
maana alisahau hata kununua maji ya kunywa
mgonjwa hivyo akaelekea kwenye duka lililopo
karibu na Hospitali hiyo ya gairo,
David akawa yupo na baba yake mzee Kazinge
akimuelekeza njia za kupita ili waweze kufika
kwenye chumba ambacho mama yake alikuwa
amelazwa, na ndani ya dakika kadhaa wakiwa
wanakaribia chumba kile na David alimwambia
baba yake,
“ Baba inabidi nionane na daktari kwanza maana
chumba hicho hawaruhusiwa kuingia kama hodi
zingine za wagonjwa wa kawaidaâ€.
Akamuacha baba yake pale akiwa amesimama na
yeye kuelekea kwa Daktari lakini alipo fika
hakumkuta ofisini mwake ilimbidi arudi kule alipo
baba yake sasa wakati ana mkaribia tu baba
yake,
aliona mlango wa chumba alicho lazwa mama
yake kitanda kilicho kuwa na mtu aliye funikwa
kuanzia kwenye miguu mpaka kichwani
kinatolewa
na yule daktari akawa anatoka kwenye kile
chumba
Daktarialipo muona David na yule mzee macho
ya
Daktari yalionekana kumkazia sana mzee Kazinge
kwa muda kisha kumuangalia David aliye duwaa
kukiangalia kile kitanda kilicho kua kinasukumwa
kupelekwa asiko kujua, Daktari alipo maliza
kuwangalia alisikitika
Kusikitika kule kwa daktari kulimpa wasiwasi
mzee
kazinge hakuelewa kwanini Daktari alifanya vile
hivyo alibaki akishangaa tu,
Miguu ya David ilianza kupiga hatua ndogo ndogo
kuelekea kwenye kile kitanda, kadri alivyo kuwa
anazidi kusogea ndivyo mwendo ukawa
unaongezeka na baadae mbio zikachukua nafasi.
Alifika kwenye kile kitanda na kuwasukuma
baadhi
ya manesi walio kuwa upande wake na kuufunua
ule mwili uliokuwa umefunikwa, maskini wa
mungu
macho ya David yalianza kuwa na chemchem za
machozi alipo hakiki kuwa mama yake ndio
ameaga dunia,
Dokta alimpa pole sana David na baadhi ya
manesi
wakawa wanambembeleza na kumshika
alivyokuwa
anajitupa tupa chini kwa kumlilia mama yake
kipenzi, uchungu alio kuwa anausikia David alihisi
yupo kwenye mpaka wa uhai na umauti,
Mzee Kazinge naye akawa kajisogeza eneo lile
kwa
aibu kubwa iliyo mjaa usoni mwake japo ni kweli
alikosea kwa kitendo kile cha kumpiga mkewe
wakati anaumwa ila chozi la upendo mpevu
lilimtoka wakati kitanda kile alicho bebwa
marehemu Magrety kikipelekwa kwenye nyumba
ya
kuhifadhia maiti.
Mama Coolin alipo fika naye alikuta hali si shwari
pale, hata maji yenyewe alio kuwa amefata aliya
dondosha chini na kujumuika katika kilio hicho,
baadhi ya watu walio kuwa wema
waliwabembeleza na Daktari aliwaomba waelekee
ofisini kwake akawape utaratibu na sababu za
kifo
cha mama David
Wakati wakielekea kwenye chumba cha Daktari,
David alilia sana kumlaumu baba yake kwa
kitendo
alicho kifanya mpaka mama yake kupoteza uhai
wake.ila hakuwa na jinsi ndio imesha tokea
ilimbidi
aendelee kulia kimyakimya tu kama mwanaume.
Walipofika tu ofisini kwa dakatari walikaribishwa
na Dokta akaanza kuwa eleza,,
“Kwanza poleni sana kwa msiba ulio wapata ila
hii
ni sehemu ya maisha ya binaadamu hivyo hatuna
budi kulikubali hili ambalo lipo mbele yetu lakini
pia tumejitahidi kwa kila tunavyoweza kuajribu
kuokoa maisha ya mgonjwa wetu lakini
tumeshindwa maana mungu ndio mwenye uwezo
zaidiâ€
“Lakini kikubwa kilicho sababisha kifo chake
mbali
na maradhi ya moyo aliyo kuwa nayo inaonekana
alipigwa huyu marehemu maana damu imevia
kwenye ubongo na hii ni hatari sana kwa uhai wa
binaadamuâ€
“Na swala hili hatuwezi kulifumbia macho hata
kidogo kwa sababu kila siku vyombo vya habari
vinatangaza juu ya matatizo kama haya na
serikali
ina mikakati migumu sana juu ya kesi kama hiziâ€
Daktari alipo maliza kuongea David alimwangalia
baba yake kwa jicho la hasira sana na uso uliojaa
udhia wa fadhaa mpaka Daktari alipo tia neno
“Bila shaka wewe ndie mume wa marehemuâ€aliuli
za Dokta
“ndio mimi Daktari†mzee Kazinge alijibu lakini
swali hilo lilimfanya ateseke kwa aibu
“Najua wewe ndie muhusika wa kipigo cha
marehemu mkeo kwa maelezo niliyo nayo hivyo
hatuna budi kukuchukulia hatua maana kama
nitakuacha na maelezo ya kifo cha mkeo niliyo
andika na weza nikafungwa mimiâ€Daktari
alizungumza na alipo maliza alichuku simu yake
ya
mezani na kupiga,
“hallo afande nakuomba uje hapa ofisini
kwangu�
alimpigia simu askari ambaye huwa alikuwa getini
na bila kuchelewa alifika ofisini kwa Daktari na
kupewa maelezo kisha akamfunga pingu mzee
Kazinge na kuanza kumpeleka kituoni kwa kosa
alilo fanya la kukiuka haki za binaadamu kwa
kumsababishia mkewe kifo,
Huzuni ilizidi kutawala moyoni mwa Davidi kilio
kiliongezeka moyoni mwake akawa anajilaumu
kwa
kumueleza Daktari ukweli ile asubuhi alipo muhoji
maana alijua shida na mateso yataanza kuomba
makazi katika familia yake,
Dakatari aliwapa utaratibu jinsi watakavyo weza
kuchukua maiti yao kwa ajili ya mazishi,
Basi hapo hawakuwa na jinsi zaidi ya kuelekea
nyumbani na kuwapa taarifa wengine juu ya
msiba
huo ulio wafika,
D avid alikuwa anajiuliza ni jinsi gani wadogo
zake
wata upokea msiba huo maana ndio wanabaki
yatima mama ameaga dunia na baba gerezani
kwa
mara ya pili.
Ujio wao tu pale mtaani watu wazima
walishaanza
kuhisi kuwa kuna tatizo, David jicho lilikuwa
jekundu na kilio cha kugugumia kiliendelea, mama
Coolin naye ndala zake mkononi kanga iliyojikaza
ikawa mkanda kwenye kiuno chake acha kile
kilemba alicho jifunga kichwani kilicho timka
timka,
mwendo wa haraka uliwafikisha kwenye nyumba
ya kina David,. Mayowe yakaanza kwa masikitiko
ya majonzi kwa kuondokewa na mama yake,
majirani wakaribu wakawa wanavutika na kilio
kile
amabacho kiliashiria kuwa ni msiba.
Ndani ya muda mchache tu taarifa za kufariki
Magrety mama yake na David zikawa
zimesambaa
kijijini hapo Gairo, mama muksini naye aliposikia
hakutaka kuwaambia kina Nisha pamoja na
Dasoni
alichokifanya ni kuwa shika mikono na kuelekea
kule msibani,
walipo kuwa wana karibia walishtushwa na sauti
za vilio ambavyo vilikuwa vinatokea nyumbani
kwako, nisha alipo taka kuuliza kuna nini ghafla
akamuona kaka yake david aki wakimbilia na
huku
akitoa machozi nao wakapokonyoka mikononi
mwa
mama muksini na kumkimbilia kaka yao.
walipokutana kati david akapiga magoti ili
alingane
nao urefu kisha kuwa kumbatia, aliwaangalia
huku
akivuta makasi ndani, hali ile ya huzuni aliyo
onesha kwa wadogo zake ilizidi kuongeza simanzi
kwao hasa alipo ongea maneno ambayo hata
kama
dasoni alikuwa mdogo aliweza kuelewa kuwa
sasa
ni yatima wa mzazi mmoja,,,,,,
“nisha mdogo wangu mama ameatucha wenyewe
hatuna kimbilio sisi wadogo zangu, baba nae ndio
hivyo…….†Aliongea maneno hayo kwa sauti
ambayo lazima utadondosha chozi kama
ukimsikia
mpakashindwa kumalizia baba yake amefanya
nini.
Mama muksini alimnyakuwa david pale alipo
kuwa
amepiga magoti na baadhi ya wazee wengine
wakaja kumsaidia kisha waka mchukua david na
kwenda kumbembeleza mama muksini nae
hakuwaacha nisha na dasoni hivyo nae alienda
kuwa bembeleza, kiukweli mama muksini alitokea
kuwa penda sane watoto hao.
Maturubai yaliweza kufungwa watu wakawa
wamejigawa wanawake upande wao na wanaume
upande wao, stuli iliwekwa njia panda ya kwenda
sehemu ya wanawake na wanaume hao kisha
kiungo kidogo maarufu kama kitunga kiliwekwa
juu
yake kikiwa na picha nyingi za marehemu mama
david ambazo zilipigwa alama x kumaanisha
kuwa
huyu ndie marehemu aliye fariki,
ITAENDELEA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni