SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Upande wa mama victoria ambaye alimuona david
kule saluni, alionekana kukosa amani tangu alipo
muona david,
alijikuta akifikiria mambo mengi sana hasa ukweli
na siri nzito alio nayo ndani ya moyo wake,
alitamani kuonana na familia ya kina david ili
awaelezee juu ya ukweli huo lakini hakupata nafasi
hiyo maana hakujua wapi wanapatikana,
baada ya kufikiri kwa muda mrefu alipata wazo la
kuwatafuta bila kujua wapi anaanzia...
Muda ulikwenda masaa yalikatika, kule hospitalini
david alionekana kupata fahamu baada ya kupewa
huduma nzuri katika hospitali hiyo,wakati huo
afande criss alikuwa katika dirisha la muhasibu
akilipia bili ya matibabu,
,saa ambayo anajirejesha hodini alimkuta david
akijitahidi kujiinua pale kitandani,tabasamu
lilionekana kwenye uso wa afande criss baada ya
kuona hali ya david inaendelea vizuri,
ndipo alipo msogelea na kumshika kichwani huku
akimwangalia usoni na kumwambia maneno ya
faraja,,,
â€David mwanangu pole sana ninachokuomba kuwa
na amani kwenye moyo wako,
Hutorudi tena kituoni tutaenda kuishi wote sawa�
David alitingisha kichwa kukubali.
Afande criss alipomaliza tu kuongea sauti ya dokta
ilisikika,
â€Unaendeleaje davidâ€?
â€Nzuri tu dokta namshukuru mungu,â€
Baada ya mazungumzo na david dokta akawa ana
ongea na afande criss,
â€Afande,,.mgonjwa wako hana tatizo kubwa ila
kilichokuwa kina msumbua ni msongo wa mawazo
yaliyo ambatana na njaa ambayo yalipelekea
mzunguko wa damu kuwa mdogo ndio maana
alipoteza fahamu hivyo chukua cheti hiki ukanunue
hizi dawa zita msaidia na sasa mnaweza
kwenda.dokta alitoa ruhusa.
Bila kupoteza muda safarari ya kuondoka ikaanza
wakiwa na gari ile ya polisi,afande cris alimpeleka
david hotelini kisha kumpitisha dukani na
kumnunulia nguo kadhaa za kuanzia,
Walifika mabibo external ambapo afande cris
alikuwa akiishi,
David alkaribishwa vizuri nyumbani kwa afande cris
lakini ukimya wa nyumba hiyo ulimfanya david
kuuliza,,,
â€mkeo na watoto zako wako wapi?
Afande cris alitabasamu kidogo kutokana na swali
ambalo david amemuuliza kisha kumjibu,,
â€tume tengana muda mrefu sasa na hapa naishi
mwenyewe tu kwakuwa na wewe upo basi angalau
nyumba itakuwa imechangamkaâ€
David alionekana kutoamini ukarimu alio kuwa
ameoneshwa na afande cris kwa muda mfupi,
Alitaka kumuuliza maswali mengi zaidi lakini
alikumbuka usemi wa baba yake kuwa
â€usimuamini yoyote yule pia penda kuwa mtu wa
kusikiliza na kusema kidogo tu ili upate kujua
mengi zaid.â€
Hivyo david akafunga kinywa chake na kuendelea
kusikiliza afande criss akizungumza tu;
****************************** **
Mwaka huo ulikatika na david akawa amesha
mueleza afande criss yote yalio mkuta na juhudi za
kumtafuta nisha zikawa zinaendelea ila
hakumwambia swala la ushahidi kuhusu
mwanamke ambaye baba yake alimwambia akifika
mjini amtafate na afande criss kumuahidi kuwa
atakuwa nae bega kwa bega mpaka atakapo
fanikiwa kupata mali zake,,
Siku moja ya mapumziko mishale ya saa mbili
usiku wakati taarifa ya habari inatangazwa waziri
wa elimu alitangaza kuwa matokeo ya kidato cha
sita sasa yapo hewani na kiwango cha ufaulu
kimeongezeka kwa asilimia 65 toka yale ya awali
yalio kuwa na asilimia43,
Taarifa hizo zilimshtuwa sana david maana na
yeye alikuwa anahusika katika mtanange huo
Hivyo afande cris naye hakuchelewa akaenda
kuchukua laptop yake na kuanza kutafuta namba
ya mtihani ya david ambayo alimueleza tayari,
Nyuso za furaha zilionekana usoni kwa kila mmoja
baada ya kuona matokeo ya david kuwa amefaulu
kwa kupata daraja la pili hasa yale masomo yake
ya sayansi,
Lakini ghafla tu furaha ya david ilikatika na afande
cris alimuuliza,,,,
â€vipi david hukuridhika na daraja ulilo pata? Swali
hilo david hakujibu na mchozi mwembamba
ukaanza kumtoka,
Afande criss ilibidi amuulize tena,,,
â€David mwanangu tatizo nini embu niweke wazi
basi?
Ndipo alipo nyakuwa kinwywa chake na kusema,,,,,
â€nafanikio haya madogo nilitamani wangekuewepo
familia yangu hapa lakini sina jinsiâ€â€™
Afande cris alizidi kumpa maneno ya kiume david
na kumueleza jumatatu wataenda morogoro mpaka
gerezani alipo mzee kazinge na atapata
kuzungumza naye david jicho lilimtoka------------
Ile siku iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu ya
kwenda kijijini kwa kina david ikawa imewadia,
david alionekana kubadilika kutokana na siha nzuri
ya uso aliokuwa nao kutakata na maji yale ya
chumvi ndani ya jijini lenye kila aina ya ufuska na
wingi wa watu jiji la dar es saalam,
Afande cris kazi yake ilikuwa kuachia tabasamu tu
kwa david maana alikuwa kanyonga tai ya
kiuutuuzima shati lake la mikono mirefu renye
rangi ya zambarau lilijitosheleza vizuri ndani ya
suruali ile nyeusi achia mbali kile kizibao
kilichoendana na rangi ya suruali,
Nywele zake alizofuga kiasi na kuzitana vizuri
zilizidi kung’aa hasa kutokana na mafuta maalumu
kwaajili ya nywele, hakika shida ndizo zilizo kuwa
zinauficha ushababi wa david lakini kwa hali ya
sasa hakuna mwanamke ambaye akaambiwa lugha
ya ushawishi wa kimapenzi akakataa kwanza ni
lazima huyo mwanamke atapata uwoga kwa
kutojiamini kusimama na david,
Afande cris na david waligonisha matabasamu yao
kisha kupanda kwenye ile mazda yenned namba za
usajiri Tz6210, kisha mafuta kukolezwa safari
kuelekea morogoro, foleni ile ya pale maeneo ya
kimara mpaka mbezi kwa msuguli iliwapotezea
kama dakika 45 hivi walipo imaliza mazda ikawa
imepamba moto,,
Injini ya gari ile iliweza kuwatunzia heshima yao
kwa kutowasumbua njiani mpaka walipo kuwa
wanaingia kwenye ardhi ile yenye sifa ya kuwa na
udongo mwekundu na kunyimwa bahari, hiyo ni
ndani ya milima ya uluguru Morogoro
Hapo morogoro mjini waliweza kupumzika kwenye
bar moja inayoitwa makuti
Kupata vinywaji na chakula kupoza njaa kidogo
baada ya kuwa wametembea njiani kwa muda usio
pungua masaa matau hivyo walikuwa wanatoa
uchovu wa safari hiyo,
Wahudumu waliokuwa wana wahudumia
walitamani kwenda kwenye meza hiyo mara kwa
mara kutokana na mvuto wa david japo mwenyewe
aliweza kujua kuwa wasichana hao walikuwa
wanajigonga gonga kwake lakini kwa upande wake
hakujali yani kama moyo wake wa upendo ulipigwa
kufuli na matatizo yalio kuwa yana muandama kwa
muda mrefu,
Hapo ilikuwa sio mwisho wa safari walikuwa na
saa moja na nusu hivi mpaka kufika gairo kijijini
kwa kina david hivyo walivyo maliza kula na
kunywa mazda ikawashwa upya na kuchukua
barabara inayoelekea dodoma ili waweze kufika
gairo eneo maarufu kwa ulimaji wa viazi vitamu,
Ndani ya saa saba na mchana wakawa wapo ndani
ya kijiji cha gairo, watu wengi walianza kulishanga
lile gari lilikuwa linaelekea nyumbani kwa kina
david maana palionekana kuwa kimya kwa muda
mrefu sana, majani mengi yaliota kuzunguka ile
nyumba ambapo ilikuwa in dalili tosha kwamba
kulikuwa hakuna mtu,
Jambo hilo pia lilimshangaza david sana yani,
hakujua kwa nini pale nyumbani pako vile,iliwabidi
washuke haraka na david akaanza kugonga lile
geti,,,,,
“mzee nyomolage, mzee nyomo lage!!!!!!!!!!!!!!!!!!!,
lakini kimya kilizidi na mwangi ndio uliokuwa
unamjibu kama yeye alivyokuwa anaita,
Lakini punde tu kuna mmama mmoja hakuwa
mbali na pale akawa anawapigia kofi kama ishara
na kuwaoneshea mkono kama ishara ya kuwaita,
afande cris alimtazama na david kisha wakaelekea
kule alipo yule mama,
Walivyofika yule mama aliwaomba waelekee
nyumbani kwake ambako kulikuwa si mbali sane
na pale na huko aliwakalibisha na kuanza
kuzungumza,,,,
“david baba yani mmekuwa maarufu kijiji kizima
hakuna asiyejua habari zenu ,hakuna asiyetoa
chozi kwa ajili yenu kila mtu anawa hurumia
nyie!!!!!!!
Maneno hayo bado yakawa yanamuweka katika
wakati mgumu sane david na afande criss
walishindwa kumuelewa yule mama alikuwa ana
maana gani ilibidi david ambembeleze azungumze
kitu ambacho wanaweza wakamuelewa,,
“mama tafadhali in yale yale au kuna mengine
yametokea maana hali ya nyumbani kwetu
sijaielewa!!!, wakati naondoka tulimuacha mzee
yomolage pale nyumbani lakini tunafika kuna
onesha hakuna dalili zozote zile za kuwepo na mtu
wala vitu ndani kwa kuwa ule mwangi nilikuwa
nausikia kama vile nyumba ipo tupu nakuomba
mama tueleze ukweli mzee nyomo lage yuko
wapi?????
David sasa hali ikaanza kubadilika kwake na
machozi kuonekana kulenga lenga kwake hapo
afande cris kama mtu mzima naye alichukua nafasi
ya kuzungumza na yule mama iliawaeleze hali
halisi iliyo tokea ndipo yule mama ikabidi awaeleze
kilichotokea,,,,,
“ilikuwa ni siku moja ililyokuwa na mvua kiasi
ambapo watu wengi walikuwa wakipishana
kuikimbia mvua ile kuelekea ma kwao nami nikiwa
mmoja wao niliyekuwa naikimbia ile mvua kuja
nyumbani kwangu, sasa wakati na pita nilisikia
kelele mle ndani kwenu zikijibizana na sauti
niliyoweza kuitambua ni ya mzee nyomolage
ikilalamika kujibu maswali ila ile iliyokuwa inauliza
sikuweza kuitambua,,,,,
“watoto wa alfred wako wapi wewe mzee eeh?
Kunamtu alikuwa anauliza kwa ukali sane
“Sijui mimi jamani walipoenda, nimewatafuta sana
kila kijiji lakini sikuwapata na ukweli sijui
watakuwa kijiji gani kwa sasa†mzee nyomolage
nilimsikia akijibu swali hilo kwa sauti ya machozi
tena nikasikia sauti za watu wengine zikimuuliza
swali hilohilo la kuwaulizia nyinyi,,
Ghafla niliwaona watu ambao walikuwa wamejazia
wasio pungua watatu na mmoja aliyekuwa amvaa
suti na miwani ya kitanashati wakitoka mle ndani
na kupanda kwenye gari kisha kuishia punde tu
alitoka mzee nyomolage na kutimua mbio kuelekea
kusiko julikana mpaka leo hii hatuji kama mzima
au amekufa,
Wanakijiji ambao nao walipata kuliona tukio hilo
kwa mbali kama mimi niliye jibanza kwenye mti
kushuudia tukio hilo tuliaandamana mpaka kwenye
serikali ya kijiji na kutaka swala hili lifatile kisheria
kuna tatizo gani mpaka familia hii inyanyasike kiasi
hiki na yote hayo yalibebwa na tukio zito ambalo
tulipata kusikia kwamba na baba yako mzee
kazinge amefariki huko akiwa gerezani na kuzikwa
na serikali baada ya kukosa ndugu,,
hicho ndicho kilichotokea yani mungu ashukuliwe
kuwaepusha wewe na nisha katika tatizo hili
yawezekana kizazi chenu kingeishia siku ile kama
nanyi mngekuwepo,,
***********************
Maneno hayo yalimfanya afande criss alijisikia aibu
sana kwakuwa na yeye in mmoja katika vyombo
vya dola na baada ya david kushikwa na hasira na
kulalamaika kwa kilio ambacho alikuwa anailaumu
serikali nzima.,,
Afande cris alizungumza na yule mama na
kushukuru kwa ujumbe ambao walimpatia kisha
kumbembeleza david anyamaze iliwajue wanaanzia
wapi kulifatilia tatizo hilo,,
Baada ya kuwaza na kuwazua afande alitoa wazo
waende kwanza shuleni kwako alikosoma david
wakachukue vyeti vyake vya form six lakini kabla
hawajaelekea huko afande alimuuliza swali yule
mama,,
“sasa mbona na ule mlango umefungwa in nani
aliyeufunga na wakati mzee nyomolage alikimbia?
“ni mimi ndie niliyempa kufuli mwenyekiti alipokuja
kuhakikisha na serikali ya kijiji baada ya kusikia
mzee nyomolage amekimbia hivyo funguo zingine
ni nazo mimi kama mnazihitaji naweza kuwapatiaâ€
afande cris alizihitaji ili wakaangalie usalama wa
mle ndani,
Zoezi hilo lilifanyika wakawa wamekwenda mle
ndani na kwa bahati nzuri vitu muhimu walivikuta
kama vile picha na vyeti vya kidato cha nne vya
david na walikwenda shule wakapatiwa vyeti vya
kidato cha sita na siku hiyo wali lala kwa huyo
mama na asubuhi yake safari ya kwenda gerezani
kutaka kujua kilichomuua mzee kazinge ni nini na
swala hilo afande cris kuahidi kuwa atalifatilia-
Ndami ya david alikuwa anaona kama wanachelwa
vile kufika kule gerezani, mawazo ya hasira
yalikuwa yanakuja kichwani mwake juu ya afande
criss kuona ndio wale wale tu kama maaskari
wengine, uso uliiva kwa hasira kila akifikiria
matukio yaliokuwa yanaongozana,afande crss nae
alisha gundua gadhabu anayo ipata david kwa
wakati ule hivyo alijitahidi kuendesha gari hilo kwa
mwendo kasi mpaka lilipo wafikisha salama
kwenye kwenye gereza alilokuwa amefungwa
afande mzee kazinge,
Walifika getini na kufuata utaratibu wa
kujiandikisha jina lako, mahali unapoishi na mtu
unayekwenda kumtazama,. Swala hilo halikuwa
gumu kwako, walijiandikisha lakini ujanja
alioutumia afande criss ulikuwa wahali ya juu sana
alimnong’oneza david sikioni kisha matokeo ya
yale aliyo mwambia kwa siri yalikuwa ni haya,,
Kwakuwa afande criss alikuwa in mtu mzima pia
hakuvaa kipolisi alikwenda kama raia wa kawaida
hivyo yeye aliandika anakwenda kwa mkuu wa
gererza na divid aliangalia jina moja la juu baada
kama ya majina matano hivi akaliandika kuwa
anakwenda kumuona mtu yule kumbe hata kumjua
hamjui ila lengo lilikuwa in kutaka kuonana na
wafungwa angalau anaweza akapata chochote kitu
juu ya kifo cha baba yake..
ITAENDELE
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni