sehemu ya kumi na ya kumi na moja
Ndipo mpiga debe huyo alipo ongozana nao na
kuelekea kwenye stendi kubwa ya mabasi
yaendayo mikoani na kuwafikisha mpaka kwenye
basi la abood liliokuwa mbioni kuondoka na alipo
pewa chake akaondoka zake, david alikata tiketi za
watu wawili yeye na mdogo wake kisha wakaingia
kwenye gari na kutafuta siti zao kwa kuuliza uliza,
watu wengi walionekana kuwashangaa kutokana
na muonekeno wao maana tumeshazoea kuwa kila
tunaposafiri basi lazima tupendezze lakini kina
david walikuwa kama vile wanakwenda shambani
kwa kwa ajili ya kilimo kutokana na kukurupuka
kwao.
Honi ya kujiandaa ilipigwa na baada ya dakika
chacbe tu gari ikaanza kuchanja mbuga kuiacha
morogoro mjini na kuelekea dar es salaam, nisha
alionekana kufurahia safari hiyo maana hakuwahi
kupanda gari tangu alipoanza kujitambua kwa kiasi
fulani.
David nae aliegemea kwenye siti akiutafuta usingizi
huku mawazo hayakuacha urafiki na kichwa chake,
hakika mwendo wa gari hilo ulikuwa in mkubwa
sane hata abiria waliokuwa na roho nyepesi
walianza kupiga kelele kumuomba dereva apunguze
mwendo lakini hata ivyo ikawa kazi bure kwao na
mwendo huo ulio anzia saa mbili asubuhi mjini
morogoro uliweza kuwafikisha jijini dar es saalam
saa tano asubuhi hivyo waliweza kutumia muda
wa masaa matatu tu mpaka kufika hapo..
Abairia wakaanza kushuka kwenye basi hilo na
kulakiwa na ndugu zao waliokuja kuwa pokea,,kina
david nao walishuka na kuanza kushikana mikono
kwa hofu maana sifa za jiji hilo waliweza kuzisikia
kupitia vyombo mbalimbali vya habari hivyo david
ilimbidi awe makini kidogo, alisimama pembezoni
mwagari hilo akitafakari pakwenda alipopata wazo
la kutaka kutoka kwanza mle nisha alimwambia
david,,
“kaka nimesahau mkoba wangu kwenye gari mle
ndaniâ€
“Aah nisha nawewe mbona mzembe hivyo?
Aliongea kwa kuchukia david maana aliona kama
anamchanganya hivi ndipo alipo muacha nisha
pale nje nayeye kuelekea ndani ya gari kuufuata
ule mkoba, alipofika kweli alifanikiwa kuukuta sasa
wakati anatoka alihisi kama amepatwa na upofu
hivi kutokana na kutomuona nisha pale nje alipo
muacha na kila alipo jaribu kuwauliza wale
walikuwa nae karibu walimjibu hawaju pia wapo
waliomtukana na kumpa maneno ya kejeli,,,
“we vipi umesikia sisi tumekuja kulinda watu hapa
embu chukua time bwana unatuzingua tu hapaâ€
David aliweza kuwashtua watu kwa kelele alizo
kuwa anapiga kumuita nisha huku akikimbia kimbia
ndani ya stendi hiyo kama mtu aliye pandwa na
maleria kichwani vile machozi yalimtoka lakini
hakuna hata binaadamu mmoja aliye thubutu
kushiriki huzuni na matatizo yalio mpata hapo la
kupotelewa na dada yake.
Kule kuchanganyikiwa alitoka mpaka ndani ya ile
stendi ya ubungo na kuanza kuparamia watu ovyo
kumuulizia mdogo wake lakini mbuzi wa masikini
hazai na kama akizaa huzaa dume basi ndicho
kilicho mkuta david baada ya kumparamia mama
mmoja hivi kwa ghafla na kuweza kumshtua yule
ama kinywa chake kilitoa sauti,,,
“mwiziiiiiiiiiiiii huyooooooooo jaman anataka
kunibia mwizi!!!!!!!!!!! Mwizi!!!!!!!!!!!!!!!â€
Yale mayowe yaliokuwa yanapigwa na yule mama
yaliweza kukusanya kundi kubwa la watu wenye
silaha ya kila aina walio beba matofali, wengine
walikuja na matairi maskini david wa watu kila
alipotaka kutafuta njia ya kulikimbia kundi lile
kubwa la watu nafasi alikosa kilio cha hofu
kilimtokaaa
“Jamani sio mwizi mimi mnisamehe jamani
tafadhalini naombeni mnieleweâ€
kutokana na kulalamika kwa david baadhi ya watu
waliokuwa wana utu waliweza kuhisi yawezekana
kweli sio mwizi hivyo wakawa wanaanza
kumtetea,,
“mwacheni jamani embu tumsikilize mliona wapi
mwizi aliyekuwa amekubuu analia kama mtoto
msije mkauwa mtu asiye na hatiaâ€
Wenye roho mbaya wakawa wanataka
kuwajumuisha wale waliokuwa wanamtetea david,,,
“ Haiwezekani wamezoea hawa nyie huyu
mwenzenu mnashilikiana naeâ€
Wakawa wanawavuta vuta na wale jamaa, zogo lile
kubwa lilimfanya askari wa barabarani aliye karibu
kusogea eneo lile na kujitahidi kuwazuia kitendo
cha kutaka kujichukulia sheria mkononi
“embu subirini kwanza jamani huyu kashafika
kwenye mikono ya sheria hakuna tatizoâ€
askari yule akawa anawatuliza raia wale wenye
asila kali kisha kuuliza wakati akiwa amemshika
david aliyekuwa anajitazama tazama michubuko
michache aliyeipata na machozi kumtoka,,,,
“yuko wapi aliye ibiwa? Afande aliuliza
“mimi ndiye aliyekuwa anataka kuniibia†yule
mama alijitokeza
“kwahiyo ajakuibia ila alikuwa anataka kukuibia?
Afande alimuuliza yule mama
“ndiyoâ€alimjibu
Askari yule alimwangalia david na kumkuta na
mkoba wa kike ameushika mkononi kisha kuuliza
tena,,,,
“Na huu mkoba wa nani?
Kabla david hajajibu sauti za watu waliokuwa
wanalazimisha kumtoa david kwa yule afande
wakawa wanasema maneno mengi sane tofauti,,,,
“huo atakuwa kashamliza mtu huyu mwangalie
macho yake yenyewe yamekaa kiwizi wiziâ€
“Oya mbona tunamchelewesha huyo tumuueâ€
Zogo likataka kuanza tena ndipo yule afande
akamwambia yule mama amfuate kuelekea ndani
ya stendi ambapo kuna kituo kidogo cha polisi na
huko kila mmoja alitoa maelezo yake lakini ya
david yalionekana kuto kusikilizwa hivyo alipelekwa
mahabusu na alikaa huko kwa muda wa miezi
mitatu mpaka alipotoka baada ya kuonekana
upande wa mashtaka hakuna ushirikiano hivyo
jarada lake likafungwa..
****************************** ******
Mawazo mazito yaliyo kuwa yanachanganya akili
na ubongo wa david yalimfanya kudhohofika
sana,kiasi kwamba hata ukimtazama hutamani
kurudia,mara nyingi alikuwa mtu wa kurandaranda
mitaani kana kwamba kuna kitu cha thamani
anakitafuta kwenye maisha yake,
hakuna aliye jua david anasumbuliwa na nini
kutokana na kukaa kimya muda wote.kipindi hicho
jua lilikuwa kali sana watu wengi wa jijini dare s
salaam walionekana kutembea na miamvuli na
nguo zao zilikuwa nyepesi kutokana na
joto,wengine waliketi kwenye migahawa wakipata
vinywaji baridi kupoza koo zao, hata wasichana
warembo na kina mama walipumzika ndani ya
saluni waki jipamba na wengine kufanya umbea
kama ilivyo kawaida ya wanawake.
Ndani ya saluni moja iliyopo manzese iliyo
tambulika kwa jina la “mwanamke uremboâ€mwana
mama mmoja aliyekuwa amevaa dela jeupe lenye
nakshi zinazo ng’a akitengenezwa nywele zake
huku akipiga domo ghafla alisikika
“ yesu wangu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!â€
Nini tena? Madada wa mle ndani waliuliza
lakini bila kutoa jibu alinyanyuka aliko keti na
kukimbilia nje huku akionekana kushangaa kila
upande wa eneo lile,wale madada pia walimfuata
na kumuuliza tena,
“vipi shoga mbona unatutisha? Halafu cheki
unavyo hema haraka kuna nini?
“mmh acheni tu nilivyo kuwa pale kwenye kioo
kuna kijana nimemuona akipita kwa nje lakini sina
uhakika kama ni yeye maana david ninaye mjua
pamoja na familia yake hawezi kuwa katika hali ile
niliyo muona,yupo mchafu mchafu pia amekonda
sana sijui amepatwa na nini?
“ Chaajabu nafika nje simuoni yani kama kumwaga
maji ardhini kipindi cha kiangazi ndivyo david
alivyotoweka
â€
“.pole mama Victoria huenda ukabahatisha
kumuona tena siku nyingineâ€
,wanawake wenzie walikuwa wakimpatia moyo wa
kutokata tama.
Safari ile ya david ya kurandaranda mitaani
alijikuta akitokea magomeni ambao walikuwa
wakiishi zamani,kabla ya kuhamia gairo mjini
morogoro,
bila kutegemea david katikati ya barabaraa alijikuta
akisimama huku macho yake yakitazama nyumba
moja ya kifahari iliyoko mbele yake
,ile hamadi gari aina ya†opa†lipo miguuni kwa
david liki mpigia honi,pipipiiiiiiiiiiiiiiiiiii iliapishe
barabarani lakini david hakusikia kutokana na
kupigwa na butwaa kwa alicho kiona mbele yake,,,
kelele za watu zilisikika,,,,,,
“mtumeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!, mamamaaaaaaaaaa!!!!!!!
mungu wanguuuu!!!!!!,â€
zote hizo zilikuwa juu ya david kunusurika
kugongwa na gari.hapo ndipo dereva wa gari hilo
alipoteremka na kuanza kumtoa david barabarani
huku akimsukuma na kumpa maneno yaliyo
karaisha moyo wa david,,
“we kijana unaleta pombe mpaka barabarani au
bangi zenu mnazo vuta na jua hili zina wazingua
kama wazazi wako wameshindwa kukulea sisi
tutakunyoosha ----- we huku akiendelea
kumsukumaâ€
hatimaye david akadondoka chini,akawa
anamtazama dereva huyo kwa hasira, alitamani
kumrarua rarua kama simba mwenye njaa
akimkamata swala,lakini david aliamua
kunyanyuka kwa upole na dereva kuishia zake.
David aliendelea kuingalia nyumba hiyo kwa huzuni
huku akiwa anasonga taratibu kuelekea pembezoni
mwa nyumba hiyo ambako kulikuwa na mti
mkubwa wenye kivuli na hewa safi kisha kuketi
mahali hapo.
mawazo ya david yalimrudisha sikiu chache
zilizopita na kuhisi kwamba mbele ya macho yake
kwenye ile nyumba ya kifahari kuna watoto wawili
dason na nisha ambao walikuwa wadogo zake
vipenzi wakicheza juu ya nyasi zilizo ng’a
kutokana na rangi yake ya kijani,
jicho lililojaa huruma na majonzi likaanza kutoa
mchozi taratibu huku sauti ya chini ikisikika
kugugumia
â€mhmhmhmhmhâ€
kama unavyojua damu ni nzito kuliko maji david
alishindwa kuisaliti nafsi, sauti ya david ilisikika
mtaa mzima ikiita nishaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!! !!!,
hata ndege waliokuwa juu ya ule mti mkubwa
waliruka na pia watu waliokuwa wakipita
kandokando ya barabara shingo zao zilionekana
kugeuka huku na kule kwa shauku ya kutaka kujua
sauti ile ya huzuni na majonzi ilikuwa inatokea
wapi
David aliendelea kulia kwa uchungu bila majina ya
wadogo zake vipenzi dason na nisha kukauka
mdomoni mwake.aliketi mahali hapo mpaka kiza
kikaingia,alipigwa na baridi la usiku na kung’atwa
na mbu,
hatimaye david kwenye mikono ya askari
waliokuwa doria usiku ule wa manane,hakuna
msaada alioambulia zaidi ya kipigo kutoka kwa
askari hao wakizani kuwa ni kibaka,shati lake lenye
rangi ya kijivu lililowa damu hata mguu wake
wakushoto uliteguka kutokana na kupigwa virungu
vya ugoko,alipelekwa mpaka kituo cha polisi
kilichopo hapo magomeni bila kupewa huduma
yoyote ya kwanza, siku hiyo david hakulala kabisa
kutokana na maumivu makali aliyo ya pata.
Asubuhi ilipofika askari waliokuwa zamu usiku ule
walipeleka ripoti kwa mkuu wa kituo
ikiambatanishwa pamoja na majina ya
watuhumiwa hao.,Afande cris ambaye alikuwa
mkuu wa kituo alipopitia taarifa hizo anakuta jina
la “david kazinge†alihisi kama analifahamu jina
hilo hasa la kazinge, ndipo alipo muita afande juma
na kumwambia…..
â€nenda kawatoe watuhumiwa wote walio kamatwa
usiku na wapange foleni mara moja sawa?
“Sawa afandeâ€,
afande juma alifuata agizo hilo bila kipingamizi
alielekea mahabusu na kuwaamrisha watoke nje
“haya haya toka haraka na panga foleni mara moja
huku akiwapiga na virungu migongoniâ€
.baada ya zoezi hilo kukamilika afande cris aliitwa
nakuanza kuwatazama watuhumiwa usoni kwa
makini huenda akabahatisha kumjua david
kazinge,akawa anakwenda anarudi anakwenda
anarudi mwishowe aliweka kirungu begani kwa
kijana mmoja na kumuuliza kwa ukali,,,,,
†wewe ndiye david kazinge?
Sauti yenye kutetemeka ikiambatana na woga
ilijibu,,,,,
†ndi ndio mimi afande†david alijibu
.â€haya nifuate ofisi kwanguâ€alimueleza david
.afande cris alikuwa ametangulia na david nyuma
akimfuata huku akichechemea,walipo fika ofisini
afande cris aliketi, david akawa amesimama moyo
wake ulikuwa na hofu kwakuwa hakujua kwanini
yupo pale.
ndipo afande cris alipo muamuru kukaa,,,
†hey! david alishtuka,
“unaweza kukaaâ€,alipo keti akawa anamtazama
afande cris atazungumza nini,,
.
“ Wewe ni mtoto wa mr.kazinge ambaye alikuwa
anafanya kazi benk ya nmb? afande alimuuliza
swali david
David alikubali,
Jesus Christ!!,afande alishangaa na kuuliza,,,,
“Ina maana baba yako hajatoka gerezani mpaka
leo?
Bila kujibiwa aliendelea,,,,
“Kwa hali uliyonayo ni dhahiri umekosa mahitaji
muhimu kwa muda mrefuâ€
“,kwa hiyo kwasasa mnaishi wapi wewe na family
yako na imekuaje mpaka wewe kuwepo hapa
kituoni?
Afande criss alimuuliza david huku akionekana
kuguswa sana na hali ya david
. Macho ya david yalionekana kumwangalia afande
criss kwa huruma na mdomo wake ukionekana
unataka kujibu lakini aliishia kutaja,,,,
†fa, fa fa!!!!â€
ghafla akadondoka chini na kupoteza fahamu papo
hapo.
Afande chriss alishtushwa sana na kitendo kile
ndipo alipo waita maafande wenzie kisha kumbeba
kwenye gari ya polisi na kumu waisha hospitali
iliyopo hapo magomeni.
*************************
Upande wa mama victoria ambaye alimuona david
kule saluni, alionekana kukosa amani tangu alipo
muona david,
alijikuta akifikiria mambo mengi sana hasa ukweli
na siri nzito alio nayo ndani ya moyo wake,
alitamani kuonana na familia ya kina david ili
awaelezee juu ya ukweli huo lakini hakupata nafasi
hiyo maana hakujua wapi wanapatikana,
baada ya kufikiri kwa muda mrefu alipata wazo la
kuwatafuta bila kujua wapi anaanzia...
ITAENDELEA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni