SEHEMU YA KUMI NA TATU
Kwakuwa afande criss alikuwa in mtu mzima pia
hakuvaa kipolisi alikwenda kama raia wa kawaida
hivyo yeye aliandika anakwenda kwa mkuu wa
gererza na divid aliangalia jina moja la juu baada
kama ya majina matano hivi akaliandika kuwa
anakwenda kumuona mtu yule kumbe hata kumjua
hamjui ila lengo lilikuwa in kutaka kuonana na
wafungwa angalau anaweza akapata chochote kitu
juu ya kifo cha baba yake..
Walivyo maliza wote walitoka kwa pamoja na kila
mmoja alikwenda kwenye upande wake lakini
afande alizi kumsisitiza david awemakini katika
uulizaji wake, na yeye alikwenda kuonana na mkuu
wa gereza na maongezi yao yakaanza baada ya
kuwa amefika ndani ya ofisi,,,
“habari ya kazi mheshimiwa? Afande criss
alimsalimia yule mkuu wa kituo
“salama tu habari yako na wewe?
“Namshukuru mungu niko salama:†afande criss
alijibu
“Mmmh nikusaidie nini? Ule mkuu wa kituo
alimuuliza afande criss
“mheshimiwa mimi ni ndugu yake na marehemu
alfred kazinge ila sikuwepo hapa nchini kwa muda
kidogo na nimekwenda nyumbani kwake kule gairo
sikufanikiwa kuikuta hata familia yake zaidi ya
kukuta makaburi mawili la mwanane na mkewe na
taarifa za majonzi ambazo zimenifanya nije hapa
hivyo nilikuwa napenda kujua ndugu yangu alikufa
kwa ugonjwa gani na wapi alipo zikwaâ€
Jicho lilimtoka yule mkuu wa kituo na kuanza
kukuna kichwa akitafuta jibu la kumpatia afande
criss na baada ya kujishauli kwa muda kidogo
aliweza kumwambia ,,,
“kwanza pole sana kwa msiba ulio kupata na hata
hivyo kifo chake kimetuhudhunisha sana hapa
gerezani alfred alikuwa na ucheshi sana kila
mmfungwa alikuwa nanamtania lakini kumbe
ucheshi huo tulishindwa kuutambua mapema kuwa
alikuwa ameanza kuchanganyikiwa mpaka siku
moja walipo kuwa wanafanya usafi mdogo wa
gereza hili kulimalima na kufyeka majani alijaribu
kuchukua kifaa kimoja na kutaka kujiua lakini
wenzie walimuwahi na kumpeleka gerezani na
baada ya siku tatu hivi alikutwa amekufa pembeni
ya pembeni ya kuuta wa gereza ambapo wenzio
walikuwa wanalima na uchunguzi wa polisi
ulipofanyika tuligundua kuwa amekufa kwa sumu
na wala hatujua aliitoa wapi naa kuuamua kuinywa
hivyo ndivyo tulivyo mpoteza alfred kazingeâ€
Pumnzi ndefu ilishuka kwa afande criss na
kumwangalia yuke mkuu wa gereza aliyekuwa
anajiangaisha pale kwenye kiti huku akionekana
akili yake haipo sawa na kisha kumuuliza tena,,,,,
“Na alizikwa na nani?
“Serikali ndio ilimzika baada ya kuwa hakuna
ndugu hata mmoja aliyekujaâ€
Kwa maelezo aliyo sema yule mkuu wa gereza na
kutokana na uzoefu wa kazi yake ya kipolisi afande
criss aliweza kugundua kuwa kuna kitu kinafichwa
pale basi hakutaka kupoteza muda alimshukuru
yule mkuu wa gereza na kumuaga kuwa
anaondoka basi walipeana mikono kisha afande
criss kutoka nje,.
Na upande wa david yeye alilitumia jina lilelile
ambalo aliiandika kwenye kile kitabu na kuitiwa
yule mfungwa mwenye jina la frank mgaya ambaye
au kwa jina lake la utani walikuwa wanamuita sir/
side in kutokana na ucheshi aliokuwa nao. Na
kuanza kuonge nae,,
“samahani sana kaka najua hunijui na wala mimi
sikujui lakini niliweza kupata jina lako pale kwenye
kitabu cha wanao wasili na ombi langu kubwa
ambalo kama utanisaidia basi mimi kuanzia leo
nitakuw anakuja kukusalimia na kukuletea
chochote ambacho utakuwa uanataka kutoka njeâ€
david alizungumza,
Yule jamaa frank mgaya aliposikia maswala ya
kuleteana vitu hakutaka kulemba akijiweka vizuri
kutaka kusikiliza hilo jambo amabalo anataka
kuambiwa na david ndipo alipomuuliza,,,
“ namjua alfred kazinge ambaye sasa in
marehemu?
Frank kabla hajajibu alikuwa kama amelisahau jina
hilo hivyo akawa kama nanjaribu kulikumbuka hivi
ndipo na yeye akamuuliza swali david iliapate
uhakika,,,,
“umesema kuwa sasa in marehemu?
“ndiyo†david alimjibu na ndipo yule mfungwa frank
alipokuwa amekumbuka na kumwambia,,
“aaah nimekumbuka ungesema Bob “k†ndio jina
mbalo kila mmoja alikuwa analijua hapa kutokana
na kule kudata kwake na mambo aliyokuwa
anayafanya kwani wewe nani yako? Frank
alimuuliza david
“ni baba yangu mzaziâ€
“Sasa rafiki yangu ulikuwa wapi mpaka baba yako
anakufa kinyama na kuzikwa na wafungwa kama
vile mbwa yani dah kiukweli bob k alichofanyiwa
lilikuwa sio jambo la kiuungwana kabisa wengi
walishuhudia tu mazishi yake lakini wachache ndio
ulishuudia kifo chake na mimi in kiwepo yani kama
unamungu sana kukutana na mimi yani†frank
alimwambia david na david sasa akaa mkao wa
kula kusikiliza kilicho tokea baada ya kumuiliza
ilikuwaje,,,,,,,,,,,,
“siku moja tulikuwa tumetoka kumaliza usafi
tukawa tuna kula na ukweli mzee wako alikuwa
ameanza kuchanganyikwa bila watu wengi kujua
kwakua alikuwa anaucheshi sana lakini hata hivyo
kuna baadhi ya mambo alikuwa anayafanya lazima
mtu ushtuke kidogo kuwa huyu mtu hayupo sawa
sasa tulipokuwa tunaendelea kula tukaona kuna
watu kama wanne hivi wamekuja mmoja akiwa
mevaa suti nyeusi na wengine walikuwa wamejazia
jazia hivi na bob k yeye alikuwa amejitenga na sisi
ambao tulikuwa karibu na eneo lile lakini ili kuwa
si rahisi kutuona, basi wale jamaa walionekana
kuelekezwa na askari alipo kuwa bob k na
wakafika mpaka pale na kumzunguka wakijifanya
wanacheka nae kumpa mikono ilikutengeneza
uhalisia wa udugu,
lakini bob k alipigwa na butwaa kumuangalia yule
jamaa aliye kuwa amevaa suti nyeusi kisha
kujipiga piga kichwani kulazimisha kukumbuka kitu,
wakati tukio hilo la bob k kupigwa na butwaa
mmoja kati ya wale akatoa kitu kwenye koti lake
na kuweka kwenye chakula cha bob na mwingine
akampiga na gazeti kichwani na kuliacha pale
kisha kuondoka zao na baada ya muda tu ndipo
tuliposikia bob k amefariki dunia na ukweli hakuna
hata mmoja aliyejitokeza kufuatilia swala hili ila
nimeshangaa sana unasema wewe mwanae na
ulikuwa wapi siku zote?
“Nilikuwa shuleniâ€: david alimjibu kwa mkato na
kuonekana kutafakari jambo hivi kisha kumuuliza
tena yule mfungwa,,
“hilo gazeti liliandikwa niniâ€
Kiukweli mimi sikufanukiwa kuliona ila waliokuwa
zamu kufanya usafi kule kwenye ofisi ya mkuu wa
gereza waliliona na kuja kusema kuwa bob k
alikuwa na matatizo sane ya kumpoteza mkewe
sijui nini mambo mengi sana si alikuwa nakaa
gairo?
“ndiyoâ€
“Basi mle pia waliandika baada ya washkaji
wengine waliokuwa wanatokea huko kulala mika
kuwa wamempoteza ndugu yao wa kutoka kijijini
kwakoâ€
Wakati maongezi yakiendelea muda wao ukawa
umeisha hivyo yule mfungwa alirudishwa gerezani
na david alimpatia dole kuwa usijali tuko pamoja
kisha david kuondoka na alipofika nje alikutana na
afande criss wakawa wanaelekea kwenye geti
kubwa la kutokea nje lakini wakati wanaenda
afande criss aligundua kuwa amesahau funguo
npale kwenye meza ya mkuu wagereza ilimbidi
arudi moaka kule na alipo fika mlangoni alimsikia
yule mkuu wakituo akiongea na simu iliyomshtua
afande criss-Baada ya kusikia manane haya,,,,,,
“ee bwana ule mpango umeharibika kuna,,,,,,,!!!!!!!â€
wakati hajamalizia kusema kuwa kuna nini kuna
askari alikuwa anapita pale nje alihisi kama afande
cris ametega sikio ndipo alimpomhtua kwa
kumwambia,,,,
â€â€nikusaidie nini mzee wangu?afande criss
alijiumauma na kusema,,,,
“asanate sana kjiana naingia humu sema nilisahau
in mlango gani hivyo nikawa anafananisha hii sauti
lakini sasa nimegundua kuwa ni humu
ninakotakiwa kuingiaâ€
Yule askari alistupa macho yake juu ya mlango wa
mkuu wa gereza na kukuta kibao kimeandikwa
“ofisi ya mkuu wa gereza†kisha akarudisha macho
yake kwa afande criss ambaye naye hakutaka
kupoteza muda akausukuma ule mlango bila
kubisha hodi na kuingia mle ndani,
Mkuu wa gereza aliposikia mlango wake
unafunguliwa alikata ile simu haraharaka na
kujifanaya anatafuta baadhi ya nyaraka pale juu ya
meza yake na afande criss naye akajifanya kama
hakusikua hata neno moja ambalo lita mfanya
ajaue pakuanzia. Alimuomba ladhi yule mkuu wa
gereza kwa kuingia bila kubisha hodi na kuchukua
funguo zake na kutoka zake huku akiwa na jambo
kichwani na kumuachia maswali yule yule mkuu
wa gereza aliyokuwa anajiuliza na kujipa majibu
yasio kuwa na uhakika,,,,
Alitoka njee kabisa na kuungana na david kisha
kuanza safari ya kuelekea ndani ya jiji la dar es
salaam. Ndani ya gari walitumia umbali huo
mpaka kufika dar es salaam kwa kuambizana kila
mmoja alichokipata walivyo jigawa iliwajue wapi
pa kuanzia,
Maelezo ya david yalimpa afande criss uwanja
mkubwa sane wa kufikiria nini afanye ili wa weze
kukamilisha ushahidi bila ya kujua kuwa kuna mtu
ambeye david alimsikia kuwa anaushahidi ambao
ungeweza kuwasaidia lakini naye pia hakusema
jambo hilo kwa afande criss akihisi asije
akamfanyia kama yale ya aliyofanyiwa marehemu
baba yake na helman,
Safari ilizidi kunoga kwa kila mmoja kutoa wazo
lake juu ya swala hilo mpaka walipofika jijini na
moja kwa moja gari ilianza kukataa mitaa na
kuelekea nyumbani kwa afande criss, kila mmoja
alikuwa amechoka kutokana na uzito wa jambo
hilo akifikiria ni wapi pakuanzia maana kama
utakurupuka unaweza kufungwa wewe ndivyo
afande criss alivyokuwa anawaza,,,
Afande criss alimuangalia david ambaye
aliyeonekana kuchoka zaidi hasa kwa mawazo ya
jinsi babaye alivyo uwawa kikatili na kuzikwa kama
mbwa lakini hakuna mtu aliye jali wala kufatilia
swala hilo ndipo afande criss alipo mwambia david
ampatie vile vyeti vyake vya form four na form six
kisha akaanza kuviangalia kwa makini na
kugundua kuwa katika somo la hesabu pia david
alifanya vizuri amabalo linaweza kumpa fursa ya
yeye kusomea kitu ambacho yeye alikuwa
anakifikiria ilikiweze kuleta urahisi katika uchunguzi
wake,
Afande cris alimuita david ambaye alikuwa mbali
kimawazo na kumwambia,,,,
“david kuna wazo nimelipata!â€
“Lipi hilo? David aliuliza na kukaa mkao wa kula
“embu somea shahada ya mambo ya
kibiaharaâ€afabde criss alimwambia, lakini david
alionekana kupinga
“kwa nini afande mimi nina ndoto zangu za kutaka
kuja kuwa daktari bingwa wa moyo iliniuma sane
mama yangu alipokufa kwa ugonjwa huo hivyo
inanibidi nisomee udaktari ilinije kushuhudia
mgonjwa anakufa kwa ugonjwa wa moyo mbele
yangu, mimi siwezi kusome hayo maswala ya
kibiashara afande†david alikataa katakata lakini
afande criss ndipo alipoamua kumuelewesha na
kumfafanulia vizuri zaidi,,,,,,,,,
“david sikia in kwambie kumbuka kuwa baba yako
alikuwa anafanya kazi benk maana yake alisomea
maswala ya kibiashara hivyo na marafiki wake
wengi in lazima watakuwa in wafanya biashara
hata matatizo yake yametokana na fedha za benki
ambazo in za biashara kwa hiyo sasa wewe
ukisomea maswala hayo in rahisi kuwajua watu
wengi waliokuwa wanafanya biashara na baba
yako, matajiri wengi utawajua na huenda huko
ukapata wapi helmani anapatika na nina uhakika
yeye kukukumbuka sio rahisi kwa kuwa umekuwa
sana na mpaka utakapo maliza masoma yako
utazidi kuwa mbaba na mimi nitakuwa nimepata
baadhi ya vitu katika uchunguzi wangu
umenielewa?’
David alionekana kufikiria swala hilo na kuona
limemuingia akilini na kuona kweli linaweza
kuwapa nafasi ya pakuanzia na urahisi wa kumjua
helman anapopatikana, hivyo david alikubaliana na
ushauri wa afande criss, na afande criss
alinyanyuka alipoketi na kumpiga kofi la pongezi
begani kwake kisha kuelekea chumbani kwake,,
Baada ya siku kadhaa kukatika afande criss kumbe
alifanya mawasiliano nchi moja ya jirani hapo
rwanda na nakupata chuo cha kibiashara ambacho
ndicho alichoprndrkrza david akasome na david
alikubali hilo na mipango ya safari ikawa
imeandaliwa na david akaelekea huko na atakaa
kwamuda wa miaka minne bila kurudi nchini
tanzania,,
Chuoni huko david alipokelewa vizuri na baadhi ya
wanafunzi wa kirwanda ambao kiswahili kwao
ilikuwa ni tatizo kidogo na gata kama
wakizungumza kuna utoauti na watanzania hivyo
wengi wao walipenda kuzungumza kingereza na
lugha ya kwako,
Maisha ya david yalianza kubadilika chuoni hapo
baada ya kumpata rafiki mmoja wa kiume alieitwa
gozbety lakini yeye alikuwa anapenda kujiita
gozbety CT 234 ambaye ni mwenyeji wa hapo hapo
rwanda, siku moja walipokuwa wanapata chakula
cha mchana katika mgahawa wa hapo chuoni
kwako na kupeleka kufikia katika mazungumzo
yaliomfanya david kushikilia kijijo cha chakula kwa
muda kidogo bila kukipeleka mdomoni Baada ya
kumuuliza,,,,,
“kwanini unajiita gozbety CT 234? Gozbety
alimwangalia david kwa makini sana kisha
kumueleza,
ITAENDELEA
Hadithi yako nzuri sana dada, Nina zawadi yako naomba nitafute 0674364245
JibuFuta