SEHEMU YA KUMI NA NNE
Maisha ya david yalianza kubadilika chuoni hapo
baada ya kumpata rafiki mmoja wa kiume
alieitwa
gozbety lakini yeye alikuwa anapenda kujiita
gozbety CT 234 ambaye ni mwenyeji wa hapo
hapo
rwanda, siku moja walipokuwa wanapata chakula
cha mchana katika mgahawa wa hapo chuoni
kwako na kupeleka kufikia katika mazungumzo
yaliomfanya david kushikilia kijijo cha chakula
kwa
muda kidogo bila kukipeleka mdomoni Baada ya
kumuuliza,,,,,
“kwanini unajiita gozbety CT 234? Gozbety
alimwangalia david kwa makini sana kisha
kumueleza,
“david rafiki yangu jina hili lina silinzinto sana
ambayo inazidi kuniumiza na kunifanya kuwa
mkiwa kwa muda sasa na hapa nikimaliza
masomo yangu nitaelekea tanzania huko kuna
baba yangu mdogo ni tajiri sana na ana
makampuni yake ya kibiashara pia nitasikitika
kukuacha hapa chuoni rafiki yangu
nilitamanikama
wote tungekuwa tunamaliza mwakani lakini wewe
bado unamika miwili mbele lakini usijali ukifika
tanzania tutatafutana tuâ€
Maneno hayo yalikuwa yanaongelewa kwa lugha
ya kingereza na kuchanganya na kiswahili kidogo
yaliendelea kuwapotezea muda hapo mgahawani
lakini david alikuwa na shauku ya kutaka kujua
kwanini anajiita CT 234 ndipo alipo muuliza
tena,,,,
“gozbety hujaniambia kwa nini unanjiita jino hilo
bado na lina siri gani?
Gozbety alicheka na kumwambia mbona
unaonekana unashauku ya kutaka kujua sane
david?, usijali nitakwambia tu rafiki yangu japo
sijawahi kumwambia mtu yoyote yule kwenye
maisha yangu hata mpenzi wangu mwenyewe
hajui
ila“Ninachokuomba iwe siri yako maana kama
huyo baba yangu mdogo akijua kuwa
nimemueleza
mtu juu ya siri la jina hili anaweza kunifanya kitu
kibaya kwa kuwa si baba yangu mdogo wa
kuzaliwa na baba yangu hapana, ila nimetokea
kumuheshimu kutokana na baba yangu mzazi
kufanya kazi kwake kwa muda mrefu japo
mwanzoni sikujua kuwa wanafanya kazi gani
kutokana na umri wangu kuwa mdogo lakini
baada
ya kukua na kujitambua nilielezwa na watu kuwa
baba yangu alikuwa anafanya kazi ya ujambazi
na
akakamatwa huko tanzania,
“Lakini siwezi kuamini maneno ya watu sana na
kuacha kumuamini yule aliyekuwa karibu na baba
yangu na kufanyanae kazi kwa muda mrefu
maana
yeye alinimbia kuwa walikuwa wanafanya
biashara
yakuuza magari yaliokuwa yamesha tumika kwa
muda mchache na kuyauza kwa watu hivyo baba
yangu kazi yake ilikuwa ni kuyasambaza sehemu
mbalimbali,
“Siku moja baba yangu alipokuwa anajiandaa
kutaka kuyasafirisha magari bandalini ndipo polisi
wakazingira nyumba yake na kuingia ndani
kuanza
kukagua na hatimaye walikuta bunduki kama tano
hivi na risasi kazaa hicho ndicho kilicho
msababisha akamatwe, na nilipomuuliza baba
yangu huyo mdogo zile bunduki zilitoka wapi
aliniambia kuwa kuna rafiki yao mmoja ambaye
alikuwa nafanya kazi benki ndiye aliyetuma watu
kuzipeleka pale baada ya kushindwana bei katika
gari moja zuri aina ya masidinzi benzi na
kutoleana maneno ya kashfa mbele za watu hivyo
rafiki yao yule hakupenda kuzalilishwa mbele za
watu akaamua kumuabisha kwa aina hiyo ili baba
yangu aonekane jambazi
“na kuhusu jina hili la CT 234 nimeliweka kama
kumbukumbu ili hata watoto wangu watakapo
zaliwa waweze kukumbuka kwa urahisi maana
litakuwa linatamkwa na wengi bila ya watu hao
kujua lina maana gani, hii herufi C ni jina la baba
yangu mzazi lina maana ya Cholo na T ni
Tanzania na hiyo namba 234 ni namba ya usajiri
ya ufungwa wa baba yangu huko tanzania, hivyo
ndivyo nilivyo amua kuweka kwamfumo huo hata
watoto wangu wakiulizwa huko baadae
watasemaâ€
babu yetu alikuwa anaitwa cholo alifungwa
tanzania kwa namba yake 234 hivyo ndivyo
nilivyo
amua kuwekaâ€
“baba yangu aliweza kufungwa tanzania japo ni
raia wa rwanda ni kutokana na huyo baba yangu
mdogo kufanya mipango ya kumsajili kama raia
wa tanzania kwa kuhonga pesa haraka haraka ili
kesi isiwe kubwa na isiweze kumuingiza na yeye
kama jambazi kwa kumuajili raia wa rwanda bila
kibali chochote kile.
“Kiukweli rafiki yangu david inaniuma sana kila
nikikumbuka alichofanyiwa baba yangu na huyo
jamaa wao wa benki nilitamani kumjua japo jina
tu
lakini baba yangu mdogo hakuniambia kwa
wakati
huo alinificha kutokana na jazba niliyokuwa nayo
ambayo ingenipelekea kushindwa kusoma na
kudili
kumfanyia kitu kibaya jamaa huyo yeye na familia
yake maana imenifanya nimeishi maisha ya bila
baba kwa muda mrefu,,
Gozybety alipomaliza kueleza siri ya jina lake kwa
david alishangaa kumuona david jicho limemuiva
na kuwa jekundu mchozi mwembemba ukimtililika
huku misuli ya kwenye mikono yake ikiwa
imekaza
kama mtu anayejiandaa kupigana lakini alijitahidi
kujizui kuonesha fadhaa yake pale baada ya
kukumbuka maneno ya marehemu baba yake
yaliokuwa yanasema….
“utulivu wako ndio utakao kufanya ujue mengi na
kuzipata mali zakoâ€
Japo alijitahidi kujizuia lakini jina la cholo ndilo
lilikuwa linaelea ndani ya kichwa chake maana
analijua vizuri ni mmoja wa watu walio panga
mpango wa baba yake kufungwa kwa mara ya
kwanza na ndio matatizo mengine yakaanza
kuongozana lakini alicho ambiwa na gozbety
kuhusu kufungwa kwa baba yake mzazi cholo,
anaona kinataka kumuangamiza yeye na wakati
waliofanya ubaya ni wao,
akafikiri kwa muda na kutaka kujua huyo baba
yake mdogo wa tanzania ni nani ili apate uhakika
juu ya cholo anayezungumziwa yule ambaye
alikuwa anashirikiana na adui yake mkubwa
helman ambaye amemfanya mpaka kupoteza
ndoto
zake za kuwa daktari na kusomea maswala ya
kibiashara ili ampate kwa urahisi au mwingine?
Alipokuwa anataka kumuuliza Gozbety jina la
baba
yake mdogo huyo wa tanzania walikatishwa na
mayowe yaliokuwa yanapigwa na wanafunzi hapo
chuoni wakilalamika kuwa bweni la wasichana
linawaka moto,
wote walikurupuka na kwenda kusaidia huko,
watu
walionekana kuchanganyikiwa,wengi walikimbia
mahali pasipo julikana wengine walikuwa
wanataja
majina ya watu waliokuwa wapo ndani ndipo
gozbety aliposikia jina la mpenzi wake ambaye
alikuwa anaitwa Segito kuwa yupo ndani na moto
unazidi kuongezeka,
Nguvu ya mapenzi ikamsukuma gozbety kukimbia
na kuingia mle ndani ya bweni ili ikiwezekana
amuokoe mpenzi wake lakini kwa bahati mbaya
alizidiwa na moshi mle ndani alipoteza maisha na
hiyo baada ya kuwa uchunguzi umefanyika na
kugundua kuwa katika watu sita walioaga dunia
na
ajali hiyo ya moto mmoja alikuwa ni mwanaume
aliye kwenda kuwasaidia ambaye alitambulika
kwa
jina la gozbety,
Kifo cha gozbety kilichukua sura mpya kwenye
moyo wa david maana alikuwa bado anahitaji
kujua mambo mengi sana kupitia yeye hasa
kutaka
kuhakikisha kuwa helman ndiye baba mdogo wa
gozbety?
Taratibu za mazishi zilifanyika kwa wanafunzi
waliopoteza maisha na ajali hiyo ya moto, wageni
wengi walihuzulia msiba huo akiwemo rais wa
nchi
hiyo paul kagame akiambatana na wanae, msiba
huo ulihuzunisha wengi sana maana ulikuwa ni
waghafla,
kwa kuwa ajali haina kinga basi ilibidi
wakubaliane
na tukio hilo la moto ambao chanzo chake
kilikuwa
ni shoti ya umeme,
siku zilikatika baada ya wanafunzi kupata
mapumziko mafupi ili ikiwezekana waweze
kupunguza mawazo ya tukio hilo lakini david
hakurudi tanzania alipata hifadhi kwa rafiki
mwingine ambae hawakuwa karibu sana ila
walifahamiana kutokana na kusoma kozi moja,
muda ukawa umewadia wa kurudi chuoni na
walikuta mambo yamebadilika kiasi fulani baada
ya yale majengo yalio kuwa yameungua
kurekebishwa na kupakwa rangi upya,wengi
walifurahi kukutana kwa mara nyingine na
kusimuliana mambo mengi ya mtaani kwao, hasa
yalikuwa maswala ya kimapenzi ndio yaliochukua
nafasi kubwa katika maongezi yao,
Lakini david muda mwingi alikuwa kimya sana na
nakujitenga na wenzie, hali hiyo kuna watu
walikuwa wanahisi analinga na kujisikia sana hata
wengine walidriki kusema ile sababu ambayo kila
mtu wa kutoka nchi nyingine anapokuwa kwenye
nchi ya wenyeji huonekana wa thamani sana
hivyo
utanzania wa david pia ulimuongezea umaharufu
chuoni hapo.
Madada wengi walimpenda kwa ukimya wake huo
na walitamani kuwa naye kwakuwa hawakuwahi
kusikia kuwa anamahusiano ya kimapenzi na
msichana yoyote yule chuoni hapo japo kwa uzuri
alionao na weusi wake ulio kuwa una waka waka
na kumeremeta, wapo waliojipeleka wenyewe
lakini
david aliwajibu kwa ustaarabu wa hali ya juu hata
kama walikataliwa lakini walijisikia fahari kukaa
nae,
Siku moja usiku david alikaa kwenye kitanda
chake
huku wengine wakiendelea na maongezi ya hapa
na pale, wenye kuongea na simu na wapenzi wao
waliongea na wenye kurudia kusimulia lile tukio la
moto lilivyotokea waliendelea kusikitika,
Utulivu wa david pale juu ya kitanda ulimfanya
kuanza kufikiria vitu vingi sana alimkumbuka sana
mdogo wake nisha hakujua kama yuko hai au
amekufa,alitamani kuwahi kurudi tanzania
iliakafanye harakati za kujaribu tena kumtafuta
maana alimtafuta mara ya kwanza bila mafanikio,
Lakini maneno aliyokuwa ameyazungumza
marehemu gozbety yalichukua utawala kwenye
kichwa chake aliyatafakari kwa kina sana na
kujiuliza maswali mengi ambayo alipata majibu
baada ya kuchekecha akili na kulinganisha
matukio
akajua kabisa kuwa huyu baba yake mdogo wa
marehemu gozbety ni helma tu hakuna mwingine,
Alijaribu kufikiria tena kwanini maelezo yake
gozbety yaonekane ni yakutaka kulipa kisasi kwa
familia yake akahisi kuwa ni dhahili helman
amenywesha sumu ya maneno ili apate usaidizi
wa kutaka kuendelea kuingamiza familia yake na
hapo aliapa kwa sasa yuko tayari kufa au
kufungwa, popote atakapo kutana na helman na
kumjua basi kitakachotokea hapo itakuwa habari
ya kusikitisha tanzania nzima na haitosahaulika
kamwe,
Mawazo hayo yalimsindikiza mpaka akapitiwa na
usingizi, alipoamka mida ile ya saa mbili asubuhi
akaangalia ratiba yake na kuona kuwa anakipindi
majira ya saa nne ndipo alipo jiandaa na
kuchukua
vifaa vyake na kuelekea kwenye darasa moja
ambalo lilikuwa halina mtu yoyote yule ili
akajisomee wakati anasubiria kipindi, ukimya wa
darasa lile ulimridhisha david na kwenda kukaa
kwenye kona kabisa ya darasa maana alikuwa
hapendi kelele wala kujichanganya na wenzie
kutokana na matatizo aliyo nayo hivyo aliogopa
siku moja asije akayasema mbele za watu na kila
mtu kujua kilichompata na kuwa mada chuoni
hapo,
Alipo kuwa akiendelea kujisomea ghafla alishtuka
alipohisi kama kuna mtu amepita kwa kasi nje,
alipepesa macho yake kutazama ni nani huyo
aliyepita lakini hakufanikiwa kumuona,ndipo
alpoendelea kujisomea,
Ndani ya muda huo mchache masikio ya david
yaliweza kusikia sauti nyembamba ya mtoto wa
kike ikitokea nje ya dirisha ambalo lilikuwa karibu
na yeye, sauti hiyo kwa mara ya kwanza iliweza
kumvutia david japo bado hajafanikiwa kumuona
kwa sura na kikubwa na kilichomshngaza ni
kusikia akilia kuyalalamikia mapenzi tena kwa
lugha ya kiswahili fasaha kabisa ambapo
hajawahi
kumsikia mtu yoyote yule akizungumza kiswahili
fasaha hata kama baadhi ya wa nyaruanda
wengine chuoni hapo walikuwa wanajaribu jaribu
ila kiswahili hicho kilikuwa ni tofauti kabisa hivyo
masikio yake akayatega kusikiliza maneno
haya,,,,,,,,
“hii ni sayari gani jaman kila siku watu wanalia
nimekosa nini mimi? Au sikustahili kuishi kwenye
sayari hii ya mapenzi mbona niliingia kwa furaha
na ninatoka kwa machozi,kumpenda kwangu
naonekana malaya leo,sioni faida ya kuishi ni
bora
kupoteza maisha kuliko kuishi kwenye sayari
isiyokuwa na upendo na mimiâ€
Maneno hayo dada huyo alikuwa akiyazungumza
huku machozi yakimtoka alijutia kupenda sana
mpaka kufikia kuchukua maamuzi ya kutaka
kujiua
na hilo ndilo swala david lililomfanya kunyanyuka
pale alipokuwa amekaa na kutoka nje kuifuta
sauti
ile nzuri iliyokuwa ina yalalamikia mapenzi kwa
lugha ya kiswahili,
Alipofika alimkuta msichana huyo amejiinamia
chini akizidi kulia kwa uchungu alisimama kwa
sekunde hivi akitafakari ataanza vipi
kumuongelesha yule mdada na yeye mazoea na
wasichana hana lakini alipo kuwa anajifikiria yule
dada pale chini alihiisi kuwa kunamtu kasimama
mbele yake, alipo nyakuwa kichwa chake na
kugundua kuwa yule mtu aliyesimama ni
mwanaume alimrukia na kuanza kumpigapiga na
mikono yake laini huku akimwambia,,,,
“ I hate boys just leave me alone please, I hate
you
go,â€( tafadhali naomba uniache mwenyewe
nawachukia wavulana, nakuchukia nenda)
dada huyo alizidi kumpigampiga david huku
akirudia maneno hayo kwa lugha ya kingereza
bila
kujua anaye mwambia lugha hiyo naye anajua
kiswahili kama yeye alivyo kuwa ana lia kwa
lugha
ya kiswahili,
ITAENDELEA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni