SEHEMU YA KUMI NA TANO
“ I hate boys just leave me alone please, I hate
you
go,â€( tafadhali naomba uniache mwenyewe
nawachukia wavulana, nakuchukia nenda)
dada huyo alizidi kumpigampiga david huku
akirudia maneno hayo kwa lugha ya kingereza
bila
kujua anaye mwambia lugha hiyo naye anajua
kiswahili kama yeye alivyo kuwa ana lia kwa
lugha
ya kiswahili,
David alikuwa akimtazama tu jinsi alivyokuwa
anampiga piga na kufikiri huenda yule dada naye
anamawazo kama yake kuwa hapo chuoni hakuna
mtu anayejua kiswahili kwa kutokana na wengi
wao walikuwa ni wanyaruanda na kutoka mataifa
mengine ambayo yanazungumza kiingereza, lakini
akajikaza na kumuuliza swali kwa kiswahili,,,,,
“Dada unamatatizo gani yanayokusumbua mpaka
unataka kujiua?
Ghafla tu yule dada alijikuta kaacha kumpiga na
kumsukuma david na kuanza kuduwaa kwa
alichokisika maskioni mwake kwa lugha ya
kiswahili ndipo na yeye alipomuuliza swali david
huku akitetemeka maana alihisi kama anaota
vile,,,,,,,
“we, we ni mtanzania??
David alitingisha kichwa kukubali kuwa ndio yeye
ni mtanzania, lakini kukubali kule kulimfanya
david
kuchanganyikiwa kwa muda ndipo alipo chukua
maamuzi ya kugeuka nyuma na kuondoka kwa
mwendo wa haraka kuelekea bwenini kwao,
alifika
na kujitupa kwenye kitanda hata dhana zake
alizobeba kwa ajili ya kujisomea aliziacha kule
kule
darasani,
Yule dada alibaki akijiuliza maswali na kuonesha
hali ya kutoamini kwa alicho kisikia na kukiona
mbele yake hivyo mawazo yale ya mapenzi
aliyokuwa nayo mwanzo na tukio hilo
lilimuongezea msongo wa mawazo kwa muda
huo
mchache, alidondoka palepale chini na kupoteza
fahamu, watu waliokuwa karibu na maeneo yale
walishtushwa na kile kishindo na kuanza kuelekea
kule sauti ya kishindo ilipotokea na kumuona yule
dada kadondoka chini na damu zikimtoka puani,
Walimbeba juujuu na kumuwaisha kwenye
zahanati
ya chuo hiko, wauguzi walimpokea kwa haraka
na
kumlaza kwenye kitanda kisha kumuongezea maji
ambayo yaliweza kusaidia kurudisha fahamu yake
kwa haraka zaidi,
marafiki zake hawakuwa mbali kutaka kujua hali
ya
rafiki yao inaendeleaje baada ya kupata taarifa
kwa wanafunzi walio mbeba hivyo wakawa
wanamfariji na kujaribu kumchekesha kwa vituko
vya hapa na pale ilimradi aweze kupoteza
mawazo
aliyo kuwa nayo maana walishajua kuwa huyu
atakuwa kapoteza fahamu baada ya kutendwa na
mpenzi wake aliyekuwa anaitwa Emmanuel
Regan,
Kichwa cha david kikawa kimeongeza wazo
lingine
la kuwaza, aliifikiria sana ile sauti ya yule dada
japo ilikuwa na majonzi lakini bado ilizidi kuvutia,
aliutafakari ule ufupi wake kiasi aliokuwa nao
ambao ulimfanya david kuachia tabasamu la
upendo hapo kitandani alipokuwa,
Alivuta picha na kujiuliza swali,vipi kama ataweza
kumkumbatia msichana huyo mwenye muanya
kwa
juu na aliye kata nywele zake kiasi ambazo
zilikuwa zina ng’aa kutokana na weusi wake
ambao ulizidi kufanya ile rangi yake ya usoni
inayotaka kufanana na maji ya kunde kuonekana
zaidi ni nini kitatokea?
jibu la kimahaba na bashasha likaja akilini mwake
na kujijibu
“ Ni dhahili ataweza kusikia mapigo ya moyo
wangu yanavyodunda kwa haraka zaidi kwa ajili
yakeâ€
Mawazo hayo yalimfanya david kuchelewa kipindi
darasani, na siku hiyo ikawa imepote bule,
Siku iliyofuata yule dada akawa ameruhusiwa
kule
zahanati kwa kuwa tatizo lake halikuwa kubwa
sana na kikubwa alichoshauriwa ni kupunguza
mawazo,
David alionekana kwenye viunga vya maua chuoni
hapo akizunguka zunguka kujaribu kumtafuta yule
dada ambaye hakujua atampata vipi maana
hakuwa na chochote ambacho kingeweza
kumrahisishia kumpata kama vile jina hata
mchepuo aliokuwa anasoma,
Wahenga walisema mola hamtupi mja wake
usemi
huo uliweza kumsaidia david,baada ya kumtafuta
dada huyo kwa muda mrefu bila mafanikio
akaamua kutaka kujirejesha bwenini kupumzika
alipokuwa anataka kuchukua njia ambayo itamtoa
mazingira yale ya chuoni na kumfikisha bwenini
alimuona yule dada akiwa wanabadirishana
namba
simu na msichana mwenzie ili amuelezee jinsi
mpenzi wake Emmanuely regan alivyo mtenda,
david hakuremba alijibanza kwenye mti uliokuwa
karibu na kumvizia yule dada amtajie mwenzie
namba zake,
Yule dada alipokuwa anazitaja namba zake
ambazo ni +250768000092, masikio ya david
yakayapa ushirikiano mzuri vinganja vyake na
kuanza kuziandika kwenye simu yake, basi wale
madada walipomaliza kubadirishana namba kila
mmoja akachukua njia yake bila kujua kama kuna
mtu ambaye alikuwa amejificha jirani yao,
Tukio hilo lilizidi kumuongezea david furaha na
kutaka kusahau kama anamatatizo makubwa, ali
zihifadhi namba kwenye simu yake na kuipa jina
la
Qeen tz, maana alikuwa hamjui jina lake,
Shughuli za masomo ziliendelea kwa furaha siku
hiyo kwa david na alitamani usiku ufike haraka ili
aweze kujaribu bahati yake kwakuwa huyo dada
alikuwa katoka kwenye maumivu siku mbili
nyuma
hivyo alihisi lazima kutakuwa na ugumu wa hali
ya
juu,
Ombi lake lilifanikiwa jua lilielekea magharibi na
sauti za mbu zikawa zinamsumbua david wakati
akiweka chandalua chake vizuri, kisha kuchukua
mto na kuegesha kichwa chake kwa juu na
kuanza
kubonyeza vitufe kulitafuta jina la Qeen tz,
alipolipata akabonyeza kitufe cha kijani ambacho
kina ruhusu simu kutoka au kupokea wakati
ikiingia na baada ya kuweka skioni kuzikiliza
kama
inaita alijibiwa,,
“simu unayopiga kwa sasa inatumika jaribu tena
baadaeâ€
ujumbe huo ulibadilisha sura ya david na furaha
yake kutaka kupotea, alijaribu zaidi ya mara nne
lakini jibu likawa ni lilelile mpaka alipokata tamaa
na kunza kusinzia ghafla alishtushwa na wimbo
mfupi ulikowa unaashiria kuwa kuna ujumbe
umeingia ambao na kuaza kujibizana lakini lugha
iliyokuwa inatumia hapo ni kiingereza,
“mambo? Ndio ujumbe ulio ingia kwenye simu ya
david na akanza kuuijibu,
“poaâ€
“Sijui mwenzangu nani maana hii namba in ngeni
kwangu†yule dada aliuliza
“mimi ni mtu mwenye pendo wa kweli ninaye toka
kwenye sayari ya kufuta mchozi na kuwa patia
furaha wenye majonzi kama wewe†alionge david
“Mmh wewe mbona unanichanganya na majibu
yako namba yangu amekupa nani kwanza?
Aliuliza
yule dada
“Kuna ubaya nikiwa nayo†david naye alimuuliza
swali
“Hapana ila lazima tujuane kwanza na najue
namba yangu umepata wapi kama hivyo siwezi
kukaa na namba mpya kwenye simu bila kuijua
sawa eeh†yule dada alivyojibu tu ule ujumbe
ilionekana wazi amekasirika ndipo david alimpo
mjibu,,,
“sikuzote hakuna upendo wa zamani kwa
mwanamke unaye mpenda jinsi namba yangu
ilivyokuwa mpya kwako ndivyo mimi nitakavyo
kuwa mpya ndani ya moyo wako kama utaruhusu
kupokea pendo langu kama unavyo pokea ujumbe
wanguâ€
david aliona bora afunguke kwa staili ya
kumuweka
kwenye mabano yule dada wa katanzania,
na kweli yule dada alizidi kuchanganyikiwa
maana
majibu aliyokuwa anayapokea kwa david
hakuwahi
kuyasikia kwa mwanauume yoyote yule ndipo
alipomuomba kesho asubuhi waonane kwenye
kiunga kimoja cha maua kilicho karibu na jengo
kuu la ofisi za chuo hiko david alikubali lakini
akamuuliza tena swali yule dada,,
“unaitwa nani lakini maana jina lako limejificha
ndani ya moyo wangu na alitaki kutoka kwa kuwa
onaonekana umechukia na macho yangu
yanausumbu moyo kutaka kuona jina lako kwa
mara nyingie huenda nilikuwa na kosea hata
katika
kuliandika katika kitabu changu cha matukio
ambapo jina lako ndilo lililofungua ukurasa wa
kwanza wakitabu hicho ila hata kama nilikuwa
nakosea lakini jina lako ni zuri sana tafadhali
naomba unitumie jina lako iliniliandike vizuri
kwenye kitabu changuâ€
David aliona yule dada kasha chukia na
maaongezi
yalikuwa yanakaribia kuisha kwa muda ule na jina
alikuwa bado halijui ndipo alipoamua kutumia
ujanja huo kana kwamba alikuwa analifahamu
tangu zamani ila alikuwa analikosea katika
kuliandika,
Ndege mjanja huna kwenye tundu bovu yule dada
akaingilia kwenye mtego huo na akatuma jina
lake
akihisi tayari lina fahamika kwa mtu anaye
jibizana
nae akasema,,
“Jina langu linaandikwa hivi Victoriaâ€
David baada ya ujumbe huo aliokuwa anausubiria
kwa hamu kuingia na kuusoma alifurahi sana
mpaka wenzie mle ndani wakawa wanashangaa
huyu jamaa siku zote huwa kimya vipi leo mbona
amekuwa na furaha ya ajabu sane lakini david
aliendelea kugeuka geuka na kuliangalia lile jina
mara kwa mara kisha kujifunika shuka ili apate
usingizi mapema kesho iwahi kufika------- Miale
ya jua iliyo kuwa inapenya dirishani iliweza
kumfanya david afunue shuka na kuchungulia nje
na kuona wanafunzi wenzie wakiendelea na usafi
wa nguo zao siku hiyo ya jumamosi ambayo
wengi
walikuwa hawana vipindi japo wachache walikuwa
navyo,
Alifumba macho yake na kuanza kusali
kumshukuru mungu wake kwa kumuamsha
salama
kisha kunyanyuka kitandani na kutandika vizuri
na
safari ya kuelekea bafuni ikafuata,
Ndani ya muda mchache akawa kasha maliza
kujianda na kuelekea kwenye mgahawa wa chuo
kujipatia kifungua kinywa,
marashi aliyo yapaka david yalikuwa na harufu
nzuri sana yalionekana kama yanaendana na
nguo
zake alizovaa asubuhi hiyo,ilikuwa ni pensi
nyeupe
na singrendi nyeupe yenye picha kubwa yakuvutia
na zile sendro zake nyeupe,
Wengi alio pishana nao waligeuka kumtazama
kwa
muonekano mzuri aliokuwa nao david, acha
baadhi
ya wavulana wenzie waliokuwa wanamsimamisha
kuulizia jina la marashi aliyo yapaka maana
yalionekana kuwavutia sana,
Alifika mgahawani hapo na kuagiza vitafunwa
pamoja na chai ya maziwa akajipatia na kushiba
vizuri kisha kuondoka, kurudi bwenini, kila alipo
pita au kukaa mahali popote pale basi akiondoka
ni lazima aache mada kwa watu,
walimzungumzia kwa mengi mazuri na mabaya,
japo sifa nyingi nzuri alikuwa anazipata kutoka
kwa wasichana, wavulana wengi walikuwa
wanamchukia kutokana na baadhi ya wasichana
waliokuwa wanatongozwa wengi wao walikuwa
wana sema kuwa wanawachumba tayari
naukiwauliza walikuwa wana mtaja david hivyo
kitendo hicho kilikuwa kina wakera sana,
david alifika kitandani kwake na kuchukua simu
yake ambayo alisahau kutoka nayo, alipoiangalia
akakuta ujumbe mpya kutoka kwa victoria
uliomuomba ifikapo saa saba mchana wakutane
kwenye mgahawa wa chuo kupata chakula cha
mchana na waweze kufahamiana kwa sura
maana
victoria alikuwa hajui kama anayetaka kuonana
naye walisha wahi kukutana na akazimia kwa
kutoamini kumsikia mtu akizungumza kiswahili
chuoni hapo,
******************************
Kila mmoja wao alionekana kuwa na shauku ya
kutaka kuonana na mwenzie japo victoria alikuwa
katoka kuumizwa lakini alivutika na maneno
aliyokuwa anatumiwa na david kwenye simu,
Muda uliobaki kabla ya kukutana waliweza
kuutumia kufanya shughuli zao za hapa na pale
mpaka kijua kilipokuwa kikali na kukili kuwa sasa
ni muda muafaka wa kwenda kukutana,
David alijipigilia jinsi nyeusi na tisheti jeupe
ambalo halikuwa na doa hata ya andishi moja na
chini kuvaa kiatu ambacho kiliendana na rangi ya
tisheti lake,
weusi wake mzuri wenye kuwaka waka ulizidi
kuonekana kutokana na nguo ile nyeupe
aliyokuwa
amevaa, alipojihakikishia kuwa yuko sawa na
hana
tatizo lolote lile basi hakuwa na budi kuanza
safari
yake ya kuelekea kuonana na mtoto mzuri victori,
Moyo ulikuwa una mdunda david maana hajawahi
kuongea na mwanamke ana kwa ana kuhusiana
na
mapenzi hivyo alihisi atakuwa na wakati mgumu
sana siku hiyo,
Alipokuwa anaukaribia mlango wa kuingia ndani
ya
mgahawa huo alisikia sauti ambayo ndiyo
ilimfanya mapaka kuchukua maamuzi ya kutoa
hisia zake za moyoni, ikizungumza na simu
Alipogeuka nyuma waligongana macho kwa
macho,
victoria alidosha pochi yake chini kwa mshtuko
na
david ilibidi azuge kama ndio alikuwa anatoka mle
ndani ya mgahawa hivyo alimpita na kurudi alipo
tokea,
victoria aligeuza shingo yake kumtazama david
ambaye alikuwa anaishia basi akabaki kuvuta
pumzi ndefu ambayo ile harufu ya marashi
aliyopaka david kuingia kwa wingi puani mwake,
Akili ile ya mahaba ilipomtoka victoria alishtuka
kuona baadhi ya watu wakimtazama na wengine
kucheka kwa kitendo alichokuwa anakifanya,
aliinama na kuokota pochi yake kisha kuingia mle
mgahawani huku akiwa anahema kwa haraka,
aliketi kwa muda kumsubiri mtu aliyekuwa na
ahadi naye bila kujua mtu mwenye ndiyo david
aliye pishana nae,aliendelea kusubiri lakini bila
mafanikio,maana david hakurudi tena muda huo,
Hivyo victoria naye ikabidi aondoke kwa hasira
kwa kufanywa kama mtoto mdogo mgahawi
pale,lakini furaha ilikuwa inakuja kila alipokuwa
anakumbuka jinsi david alivyompita na kuacha
harufu nzuri ya marashi,
********************
Siku kama hiyo ya jumamosi chuoni hapo kuna
kuwa na disko ndani ya ukumbi wa chuo na
baadhi
ya wanafunzi huwa wanachaguliwa kucheza
nyimbo za aina mbalimbali ilikuonesha uwezo
wao
na vipaji vyao,
Rafiki zake na victoria waliweza kugundua kuwa
victoria ameanza kumpenda david hivyo walianda
mpango na kuongea na wanachumba wenzie na
david kuwa itakapofika muda wa kucheza basi
david acheze na victoria na wengine waliobaki
watacheza na wao,
ITAENDELEA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni