Jumatatu, 15 Juni 2015

SAHIHI YA KIFO

 SEHEMU YA TANO

Alinitazama kwa dharau halafu akachukua simu
yake iliyo kuwa juu ya ile meza na kupiga, sikujua
ni nani aliye kuwa ana mpigia ila alisema,
”hallo? eeh tumesha muandaa” kisha aka kata
simu

Ndani ya muda mchache nilishtuka baada ya
kuguswa bega kwa nyuma nilipo geuka alikuwa ni
Helman, nilinyanyuka kwa kuhamaki nikarudia
kumuita tena,
”Helman ni wewe unae nifanya kukosa furaha
mimi
na familia yangu?
Alicheka kisha akasema,
”Alfred raha unajinyima mwenyewe wewe na
familia yako mbona tulivyo kuwa marafiki
haukukosa amani”?aliniuliza lakini sikumjibu.
Naye akaja aka kaa kwenye kiti, yule jamaa niliye
mkuta amekaa pale mezani mara ya kwanza
wakati naingia akawaruhusu wale mabaunsa
pamoja na wale madada mapacha waondoke
hivyo
tukawa tumebaki watatu pale mezani na Helman
akanzaa kuniambia lengo la mimi kuwepo pale,,
”Alfred kwanza unatakiwa ujue duniani kuna watu
na viatu, sasa leo nakuweka wazi kuwa mimi si
katika watu ila ni kiatu, kuunda urafiki na wewe
sio
bure ila ni kwa maana ili nitengeneze pesa kupitia
mgongo wako hivyo kazi ninazo taka kukupa ni
mbili ya kwanza,
” nataka uwe unanipa taarifa kila gari la fedha
linapo kuwa linasafirisha fedha kutoka benki moja
kwenda nyingine ili tuweze kuchukua chetu
mapema”.
Na kazi ya pili,
”Unatakiwa uni pambe kwa meneja wako kuwa
mimi ni mteja mzuri sana katika swala la mikopo
ili niweze kuwa naye karibu na aniamini hata siku
mambo yakibuma achukue muda kujua kama ni
mimi ndiye na husika atakapo sikia tetesi juu
yangu”
Jicho lili nitoka na kutetemeka baada ya
kugundua
maelezo yake yana maanisha kuwa yeye ni
jambazi
na ndio kazi iliyo kuwa inamuweka dar es salaam
hata hivyo hakuishia hapo aliniangalia kisha
akamuangalia yule jamaa mwingine na
kunitambulisha,
”huyu jamaa anaitwa Cholo yeye ni mtu wa
Rwanda ninafanyanae kazi hii kwa muda wa
miaka
mingi sana na yeye ndiye anaye nichoresha dili
nyingi sana za kwao na wale mapacha amekuja
nao huku tanzania kwa kuwa kule nchini kwao
wameshashtukiwa na wana tafutwa na polisi”
Maneno yake yalinifanya nizidi kumchukia Helman
maana alikuwa anataka kunishirikisha katika kazi
ambazo hata cheti chake sina nilinyanyuka kwa
gadhabu na kumwambia,
”hiyo kazi yako fanya na hao hao wakimbizi
wenzio lakini sio mimi, siwezi kuwa kama
kunguru
wako hawa mapacha walio kimbia nchi yao
wakati
ni raia halali wa Rwanda naenda kutoa taarifa
kituoni”
Nilipo maliza kuzungumza niligeuza mwili wangu
na kuanza kupiga hatua kuondoka, zilipofika
hatua
tano mbele Helmani akaniita nilisimama kwa
sekunde bila kumgeukia kisha ndio nikageuza
shingo yangu,
miguu ilitaka kuishiwa nguvu nilipo muona
baunsa
mmoja akimleta Sagu huku nguo zake zikiwa
zimeloa damu na kisha kumtupa chini pale
pembezoni mwa bwawa la kizungu(swimming
pool)
nilirudi haraka haraka na kumsogelea Sagu.
nikagundua kuwa walimchoma kisu dakika
kadhaa
nyuma baada yakuona tundu lililo kuwa lina toa
damu nyingi na yule baunsa akiwa ameshika kisu
kilicho lowa damu ila alikuwa bado anapumua
nikaanza kumuuliza kwa sauti iliyo kuwa
inakaribisha mchozi,,
”Sagu imekuaje mdogo wangu umefanya nini na
hawa wamekujuaje wewe eeh? Wakati huo
nilikuwa
nimepiga magoti na kujaribu kumuinua nikimshika
mabega yake,
ndipo alipo anza kunieleza.,,,,,
”hawa jamaa waliwahi kutuona mimi na wewe
nilipo kuja mara ya kwanza kununua vifaa vya
ujenzi siku za nyuma kule karia koo na
inavyoonesha walianza kukufuatilia muda sana
kabla hata ya Helman aja kufuata moja kwa moja
na kuanzisha urafiki na wewe na tulipo achana
walinifuata na kuniuliza kuwa nina uhusiano gani
na wewe, nili waambia nakusaidia tu kubeba vifaa
vyako maana sikujua wanalengo gani na nilikuwa
siwajui hivyo ilinipa ugumu kujitambulisha moja
kwa moja, ndipo walipo nipatia pesa na namba
zao za simu niwe na wapa taarifa zako, kiufupi
mimi ndiye niliye rahisisha Helman kuanzisha
urafiki na wewe”
Maneno ya Sagu yalinipandisha hasira lakini
huruma ilinijia kila nilipomtazama na hali aliyo
nayo kwa wakati ule, lakini sikujua bado sababu
ilio wafanya waamue kmchoma kisu mpaka nilipo
muuliza swali hilo Sagu na kunijibu,,
”walipo nipatia zile namba na pesa hawakujua
kama mimi sikai hapa dar es saalam na walipo
kuwa wana hitaji taarifa zako nilikuwa nakupigia
na kuzua jambo lolote lile kuhusu ujenzi halafu
nikawa na kuuliza swali ambalo walilo kuwa
wanataka kujua huku nikijichekesha chekesha ili
ujue kama ni utani”
” sasa kumbe mdogo wake na Helman alikuwa
anasoma chuo kikuu cha mzumbe aliniona siku
moja Morogoro mjini ndipo alipo mpigia simu
kaka
yake na kumueleza kuwa ameniona,
baada ya muda Helman alinipigia na kuniuliza
niko
wapi na mimi nikamdanganya kuwa nipo dar es
saalam, na neno alilo niambia ni kuwa anataka
kuonana na mimi.jumapili”
” hapo sikuwa na jinsi zaidi ya kuelekea stendi ya
mabasi msamvu na kuchukua gari kuja huku ili
asijue kama nilikuwa Morogoro ndio sababu ilio
nifanya nije usiku ule wa jumamosi bila taarifa
nyumbani kwako na jumapili ile nilivyo wapa
taarifa kuwa nipo na wewe wenzie waliamini
kuwa
nipo hapa dar na ulivyo nishusha pale ndipo nilipo
kuja kuonana na Helman,”
”kwakuwa Helman anamuamini sana mdogo wake
ilibidi anipeleleze kwa kunipa kipigo mpaka nilipo
kubali kuwa nilikuwa Morogoro na kisu hiki
wamenichoma nilipo kataa kuwaeleza ni kitu gani
na fanya kule Morogoro hivyo hawajui kama
unajenga, siri yako mimi ndio nakufa nayo”
Mpaka Sagu anamaliza kunieleza njama nzima
waliokuwa wanaifanya ya kunizunguka mimi
mchozi ulikuwa umesha lowesha shavu langu
lote,
kimya kweli kilitawala kwenye kinywa cha Sagu
kumbe alisha kata roho, hasira zilinipanda ,nilipo
geuka kwenye meza walio kuwa wameketi kina
Helman ilikuwa nyeupe kumbe wakati walivyo
mtupa Sagu pale chini wakakimbia maana
walijua
hato weza kupona na ile ni kesi ya mauaji na
ghafla maskio yangu yakaanza kusikia ving’ola
vya
polisi
Ndipo nami nilipo pata akili ya kukimbia,
niliongoza
moja kwa moja mpaka kwenye
BMW230 na kuiwasha na mwendo wa kasi
ukachukua nafasi barabarani, nilipishana na
magari
yasiyo pungua matatu ya polisi yakielekea land
mark hotel kwenye tukio japo sikujua ni nani aliye
wapa taarifa, hilo si kujali kwa wakati huo kilicho
kuwa akilini mwangu ni kutoka eneo lile maana
kama ningeonekana wange hisi kuwa ni mimi
nahusika na mauaji kwa ushahidi wa nguo zangu
kulowa damu nilizozipata wakati nime mpakata
marehemu Sagu,
kila nilipo kuwa na simama kwenye foleni hofu
ilizidi kunielemea moyoni mwangu mpaka nafika
getini kwangu sikuamini kama nimeweza kujitoa
kwenye eneo lile la hatari, nilichukua simu yangu
na kumpigia Magrety(mama David) aje
kunifungulia geti lakini simu yake ikawa
haipatikani
na usiku ndio ulikuwa unazidi kuwa mnene japo
siku angalia saa ila nili hisi yaweza kuwa ni kama
saa nane hivi.
Nilishuka kwenye gari na kwenda kuluka ukuta
kisha nikaenda kumgongea dirishani aniletee
funguo za geti, alipo kuwa analeta funguo
akataka
kupiga kelele baada ya kuziona damu kwenye
shati
langu akijua labda mimi ndiye nilie jeruhiwa
nikamtuliza na kumwambia tuta yazungumza
chumbani, nikafungua geti na kuingiza gari ndani.
Magrety alikuwa amesimama kwenye kizingiti cha
mlango akinisubiri nilimsogelea na kumshika
kiunoni ili asiwe na hofu na kwenda naye
chumbani. Huko ndipo kimbembe kilipo anza
baada
ya Magrety kushindwa kuniamini juu ya damu
nilizo nazo aliongea kwa wasiwasi huku
akinipapasa maeneo ya tumboni kama angeweza
kuliona jeraha lakini haikua hivyo, baada ya
kulikosa ndipo sauti ya ukali na yenye kuogopa
ikamtoka,,,,,
”Alfred umeua mume wangu?
”sijaua mke wangu? Nilimjibu
“Mbona umelowa damu zimetoka wapi kumbuka
uliondoka na ile bastola huku ukiwa na hasira
balaa gani hili lina ikumba nyumba yangu!!!!!!!!!!!”
alizungumza Magrety
Nikachua akili kichwani, kwamba kama nita
mwambia Sagu amefariki litazuka jambo lingine
usiku ule ili nibidi ni mbembeleze tuzungumze
kesho ili hofu na jazba alizo nazo zipungue,
nilimshika kwenye paji lake la uso na kumtazama
kwa jicho la huruma kwenye mboni za macho
yake
kwa dakika kadhaa bila kumwambia chochote
kisha nikamuacha chumbani nami nikaelekea
bafuni kuoga ili kutoa taka mwili pamoja na zile
damu.
Wakati natoka bafuni huku nikijifunga funga taulo
vizuri nikashangaa kumuona mama David
amekasirika vibaya yani na akiwa ameshika simu
yangu mkononi nilipo muuliza nini tatizo alinijibu
kwa kuniuliza swali,,,
“Kati yako na Helman nani ameusika na mauaji
ya
Sagu”?
Moyo ulinipasua ghafla, amejuaje huyu? Ndio
swali
nililojiuliza kichwani mwangu nilipo itazama ile
simu nikaona mwanga kwenye kioo hauja zimika
nika hisi huenda kuna mtu amepiga au ametuma
ujumbe,nikampokonya ile simu kwa nguvu na
nilipo
itazama nikaona ujumbe ulio kuwa umefunguliwa
muda si mlefu aliye tuma alitumia namba ngeni
hivyo sikumjua muhusika ni nani na alisema,,,,,,,
”ukijifanya mjanja naenda kutoa taarifa kituoni
juu
ya mauaji ya Sagu”
Sikuwa na jinsi ilinibidi nimueleza ukweli tu mke
wangu kwa kilicho tokea kule nilipo toka, hapo
kidogo akawa kanielewa, akanyanyuka na kwenda
kuchukua biblia kabatini na tukamuomba
mwenyezi
azidi kutuepusha na mabalaa. Tulipo maliza
nikamuomba ni lale maana asubuhi natakiwa
kuwahi kazini kama mambo mengine
tutazungumza kesho na kujua nini kitaendelea.
Asubuhi na mapema nikaamka nikajiandaa huku
moyo wangu ukiwa na hofu maana sikujua nini
hatima ya tukio lile baada ya polisi kwenda pale
hotelini,nika toka nje kuelekea kwenye gari langu
ili
ni wahi kazini lakini sikuweza kufanya hivyo
kutokana na kuona damu kwenye siti niliyokuwa
nimekalia jana usiku hivyo ilinilazimu ni pande
bodaboda mpaka kazini.
Wakati naendelea na kazi pale ofisini kwangu
akaja mfanya kazi mwenzangu akiwa na gazeti
lililo andikwa ,,,,
”mtu mmoja auwawa na watu wasio julikana
usiku
wa kuamkia leo katika hoteli ya landmark iliyopo
maeneo ya river side ubungo na jeshi la polisi
linaendelea na uchunguzi kuwa baini wauaji hao”
huku gazeti hilo likiwa limewekwa picha kubwa
kwa mbele ya marehemu Sagu iliyo pigwa
kwenye
tukio hilo.
Hali ilizidi kuwa tete kwa upande wangu siku hiyo
nilijikuta kukosa amani kabisa tangu nilipo ona
picha ile kwenye lile gazeti, ufanisi wangu wa kazi
ulipungua ilipofika mishale ya saa saba mchana
ilinibidi niombe ruhusa kwa meneja kuwa naumwa
ili nikapate muda wa kupumzika kutokana na
hekaheka za jana na kujadili swala lile na mke
wangu.
Mchana huo nilipanda daladala kurudi nyumbani
huko pia walizidi kunichanganya maana kulikuwa
hakuna jambo walilo kuwa wanazungumza zaidi
ya
tukio lile la mauaji ya Sagu
”jamani duniani kuna watu wa katili sana
unawezaje kutoa uhai wa mwenzako kama kuku”
Utazani wao hawajaumbwa au hawato kufa” hizo
zilikuwa sauti za abilia walio kuwa nyuma yangu
wakionesha kusikitika juu ya tukio lile.
Daladala ilipofika kwenye kituo changu nilishuka
nakuongoza njia ya nyumbani kwangu, baada ya
kupita nyumba kadhaa kabla sijafika kwenye
nyumba yangu nilistaajabu kumuona Cholo yule
jamaa wa kinyaruanda niliyetambulishwa na
Helman akitokea maeneo ya nyumbani kwangu
nilisimama kuhakikisha kama ni yeye au
kupagawa
kwangu tu, lakini alivyo sogea alikuwa ni yeye
kweli, naye alipo niona alishtuka pia aliningalia
kwa jicho la shari kisha akaongeza mwendo wa
kutembea.
Kitendo kile kilinifanya nianze kukimbia kuwahi
familia yangu ili nijue kama ipo salama nilifika
nyumbani na kukuta geti lipo wazi nikaelekea
sebleni nikakuta makochi yamesogezwa na vitu
vipo katika mpango usio eleweka nili nibidi niite
kwa hofu,,
”Magrety Magrety?
”Abee mume wangu”aliitika kisha kuja pale
sebuleni kutokea chumbani kwa David akiwa
ameshika kifaa cha kudekia kisha kuniuliza,,,
“Mbona mapema Alfred kuna usalama kweli
huko?
”Usalama upo kiasi ila habari za kifo cha Sagu
ndio limekuwa gumzo la jiji huko nje”
”kuna mtu aliye kuja hapa” nilimuuliza
”hapana hajaja mtu”alijibu
”Kwanini umeuliza hivyo”?aliniuliza
”Maana geti lipo wazi”
”Ooh walikuja wazoa taka watakuwa walisahau
kufunga lakini huja nijibu kwanini umewahi
kurudi?
alijibu na kuniuliza nami nikamueleza sababu iliyo
nifanya niwahi kurudi.
****************
ITAENDELEA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni