SEHEMU YA SITA
Kitendo kile kilinifanya nianze kukimbia kuwahi
familia yangu ili nijue kama ipo salama nilifika
nyumbani na kukuta geti lipo wazi nikaelekea
sebleni nikakuta makochi yamesogezwa na vitu
vipo katika mpango usio eleweka nili nibidi niite
kwa hofu,,
â€Magrety Magrety?
â€Abee mume wanguâ€aliitika kisha kuja pale
sebuleni kutokea chumbani kwa David akiwa
ameshika kifaa cha kudekia kisha kuniuliza,,,
“Mbona mapema Alfred kuna usalama kweli
huko?
â€Usalama upo kiasi ila habari za kifo cha Sagu
ndio limekuwa gumzo la jiji huko njeâ€
â€kuna mtu aliye kuja hapa†nilimuuliza
â€hapana hajaja mtuâ€alijibu
â€Kwanini umeuliza hivyoâ€?aliniuliza
â€Maana geti lipo waziâ€
â€Ooh walikuja wazoa taka watakuwa walisahau
kufunga lakini huja nijibu kwanini umewahi
kurudi?
alijibu na kuniuliza nami nikamueleza sababu iliyo
nifanya niwahi kurudi.
****************
Miaka kama mitatu ilipita mke wangu akapata
ujauzito ambao mtoto ndio huyu dason na
uchunguzi ulifanyika juu ya kifo cha sagu ila
wakafanikiwa kumkamata cholo yule mnyaruanda
ilisemekana kuwa helman alihonga pesa nyingi
sana mpaka yeye hakuhusishwa katika ile kesi.
Mpaka siku moja nikiwa nimetulia na magrety
nikapokea ujumbe kutoka kwenye namba ambayo
alijitambulisha moja kwa moja kuwa yeye ni
helman na kunipa vitisho,,,,
â€NAJUA KUWA WEWE NDIYE ULIE TOA TAARIFA
KITUONI MPAKA CHOLO AMEKAMATWA NA KAMA
ISINGE KUWA PESA ZANGU LEO NA MIMI
NINGEKUWA GEREZANI SASA UTAKIONA
KILICHOMFANYA NYOKA KUKOSA MIGUU KAMA
SIO KUFA WEWE BASI FAMILIA YAKO ITAKUWA
KWENYE MATATIZO NA HIVYO VIKISHINDIKANA
UTAMFUATA CHOLO GEREZANI KWA GHARAMA
YOYOTE ILEâ€
Huo ndio uliokuwa ujumbe wa mwisho kutumiwa
na Helmani kabla ya kuundaa mpango wake
ulionifanya mpaka nikaenda gerezani
Vitisho kutoka kwa Helman ndio ikawa sehemu
ya
maisha yangu kwa kipindi chote hicho japo tangu
tukio la mauaji ya marehemu Sagu sikuwahi
kumtia machoni zaidi ya kupata ujumbe huo nami
sikutaka kujua yuko wapi maana kwa kiasi fulani
hali iliaanza kuwa shwari kutokana na jeshi la
polisi nchini kuwa makini na matukio kama hayo.
Nami umakini ukazidi kwa familia yangu na
kuzidisha upendo kwa wanangu na kumngojea
kwa
hamu kiumbe kilicho kuwa tumboni kwa Magrety
na ufanisi wangu wa kazi ukawa umerejea kama
kawaida hivyo amani kwa ujumla ikawa imerejea
nje hata ndani ya moyo wangu ikawa nikitoka tu
kazini sina sehemu ya kwenda zaidi ya kuelekea
nyumbani,
Jumatano moja iliyo pambazuka na hali ya
mvuamvua kulikuwa na watu wengi nje walio
kuwa
wana subiri kuingia ofisini kwangu kwa ajili ya
kusaini fomu za mikopo ili wakaendeleze biashara
zao na wale walio kuwa ndio wanaanza kuchukua
mikopo walikuja na kopi za hati za nyumba zao
pamoja na picha baada ya taratibu zote kufuatwa
kama wasaidizi wangu kwenda kuhakiki nyumba
hizo na sahihi kuwekwa na mdhamini kama mtu
alizaminiwa nyumba.
Kazi ilikwenda vizuri wengi niliwakamilishia
huduma walizo kuwa wanahitaji lakini hofu ilirudi
tena baada ya kupata mteja aliyetambulika kwa
jina la Khaji Kipeneko baada ya kunionesha fomu
yake iliyokuwa na sahihi yake na ya mdhamini ila
ile ya mdhamini nilikuwa na ifananisha na ya
Helman alipo nionesha na picha ya nyumba
nikahakiki kuwa ni kweli ni ya Helman macho
yalipepesuka marambili mbili kisha ni kamtazama
yule jamaa kwa makini na kumuuliza kwa
dhihaka,,,,,
“aliyekudhamini nyumba hii ya thamani ni nani
yako maana anaonekana ana moyo sanaâ€
“ni bosi wangu†alinijibu
Mdomo wangu ukapata kigugumizi kidogo na
wala
sikuta kuendelea tena maana anaye kuwa mfanya
kazi wa Helman lazima watakuwa wanashirikiana
katika maswala yao ya ujambazi tu nikamsainia
haraka haraka na kumueleza siku ya kuja
kuchukua mkopo wake na kumruhusu aondoke
maana alisha niharibia siku. Na bahati yeye ndiye
aliyekuwa wa mwisho hivyo nami sikuchelewa
ilinibidi niondoke kwa kuomba ruhusa ya uongo.
Nikiwa njiani ndani ya gari langu BMW230 huku
mvua ya rasharasha ikiwa inaendelea na kifaa
maalumu cha kusafishia kioo kikiwa kinabadilisha
upande kwenda kulia na kushoto iliniweze kuona
vizuri hakika macho yangu yalimuona yule jamaa
mwenye jina la Khaji Kipeneko akiwa na Helman
kwenye mgahawa mmoja ambao haukuwa mbali
sana kutoka pale benki na kama kuna jambo
walikuwa wana lijadili hivi, ilinibidi nisimame na
kuwaangalia vizuri walipo liona gari langu
walinyanyuka na kuondoka.
Nilifikiri kwa muda pale huku kichwa changu
nikiwa
nime kiinamisha kwenye usukani,
“ kwamba maisha haya nitaishi mpaka lini na kwa
nini niwe mtumwa wa elimu yangu mwenyewe?
“Helman yeye ni nani kwangu mungu ? Hapana,
sasa kwanini nimuhofie? nilijiuliza maswali mengi
na kujijibu mwenyewe, ilinibidi nichukue maamuzi
ya kumfuata anieleze kama kuna sababu nyingine
inayo mfanya aendelee kunifatafata maana ni
miaka mitatu imepita lakini bado anataka
kuendelea kuwa kikwazo kwangu.
Nilifungua mlango wa gari kwa hasira bila kujali
mvua iliyo kuwa inaanza kuchanganya na
kumfuta
Helman kule waliko kuwa wanaelekea na yule
kibalaka wake Khaji Kipeneko nilifika mpaka
maeneo yale lakini njia ilikuwa nyeupe sikujua
waliingilia upande gani, ilinibidi nirudi kwenye ule
mgahawa na kutulia kidogo kushusha pumzi
kidogo mpaka muhudumu alipo kuja na
kumuagiza
aniletee bia ya Kilimanjaro ya moto.
Nilikunywa bia ile taratibu mpaka nikamaliza japo
nilihisi inaweza ikanipunguzia mawazo lakini
haikuwa hivyo, nikatoa waleti yangu mfukoni na
kumuita muhudumu ili nimpatie fedha yake cha
ajabu alicho nijibu alinifanya nimpatie maneno
yasio stahili kuambiwa binaamu,,,
“ mbona umeshalipiwa hicho kinywaji’? aliniambia
“Na nani�
“Amesema ni kwambie mgomvi wako†alinijibu
yule
muhudumu
“Wewe dada unakichaa? Utawezaje kupokea pesa
toka kwa mtu mwingine wakati kinywaji
nimekunywa mimi na isitoshe umeniona nimekuja
peke yangu hapa embu nitokee usoni mwanguâ€
nilimjibu na kumtupia pesa usoni naye akainama
akaziokota na kuniomba radhi ambayo sikumjibu
kisha akaondoka, jibu lile alilo nijibu kuwa
mgomvi
wako ndiye aliye kulipia nilijua yawezekana kuwa
Helman bado yupo maeneo yale nilinyanyuka na
kutaka kuweka waleti mfukoni baada ya kuitoa
nilipokuwa nataka kumpatia fedha yule
muhudumu,
lakini kumbe kutokana na zile papala niliangusha
pale chini badala ya kuweka mfukoni kama
ilivyokuwa nia yangu.japo kwa muda huo sikujua.
Nilimfuata yule muhudumu na kumuuliza aliye
nilipia yuko wapi alinionesha sehemu ambayo
aliyo
kuwepo mwanzoni lakini baada ya kwenda mimi
sikumuona yule dada allisema
“ alikuwa hapa mida sio mirefu wakati mimi
nakuja
kwako†nilikasirika sana ilinibidi niondoke zangu
nyumbani.
Nilipofika nilimkuta Magrety pamoja na Nisha
wamejipumzisha kwenye makochi kutokana na
mzigo aliokuwa nao tumboni mwake. Nilielekea
mezani na kujiandalia chakula mwenyewe, nilipo
kuwa naanza kula tu David naye alikuwa anarudi
kutoka shuleni basi nikaungana naye pamoja
tukala wote, kisha nikaelekea chumbani kutafakari
mpaka Magrety naye alipo amka nakunikuta nipo
chumbani
“eeh mme wangu umerudi saa ngapi tena�
aliniuliza
“Muda mrefu mpaka nimekula we ulikuwa bado
ume lala na Nisha wako pembeni sikutaka kuwa
sumbuaâ€
Basi baada ya maongezi hayo mafupi ilinibidi
nimueleze kilicho nikuta siku hiyo naye alinipa
wazo,
“Baba David mme wangu swala hili sasa naona
linazidi kuelekea pabaya zaidi maana huyu
Helman
inaonekana ni sugu na anaweza akakusababishia
matatizo makubwa maana haiwezekani kipindi
chote hiki awe bado anakufuatilia halafu bila kosa
lolote lile cha msingi hapa kesho twende tukatoe
taarifa kituoni hata kama kuna jambo lita tokea
basi polisi lisiwe geni kwaoâ€
“Nimekuelewa mke wangu mpendwa nitafanya
hivyo kweli hali hii inazidi kuniogopesha sana
hasa
nikifikiria usalama wa familia yanguâ€
Tuliweza kukubaliana maamuzi yetu mimi na mke
wangu kilicho baki tulikuwa tunaomba uzima kwa
mwenyezi mungu tufike salama siku inyofuata ili
tuelekee kituoni;
Waswahili wana sema mwenye nacho
huongezewa
kwangu usemi huo ulichukua nafasi baada ya
kuongezewa matatizo niliyo kuwa nayo,
Asubuhi na mapema wakati nikiendelea kujiaanda
ili nieleke kituoni na baada yapo ndio niende
kazini,
sikujua kilicho nisukuma kuwasha luninga yangu
ya chumbani ambayo ilikuwa inatangaza habari
mpya,,
“ndugu watazamaji wa kipindi chetu cha â€
matukio
yetu†siku ya leo tunaamka na habari ambayo
imeshika katika habari zote tulizo nazo,
“Gari lililo kuwa linasafirisha fedha jana jioni
kutoka Dar es salaam kwenda Tanga lilivamiwa
na
majambazi wasio julikana na kuwajeruhi baadhi
ya
maaskari waliokuwa wana linda gari hilo ila kwa
bahati nzuri kuna baaadhi ya vielelezo ambavyo
vimeweza kuonekana eneo la tukio ni pamoja na
waleti iliyokuwa na vitambulisho ambavyo
vinasemekana ni vya mmoja wa wafanyakazi wa
benki ya NMB akitambuliwa kwa jina la Alfred
kazinge pamoja na bastola moja ambayo
ilionekana kutumiwa katika tukio hilo na kwa
taarifa tulizo nazo ni kwamba polisi wanaelekea
kumkamata mtuhumiwa baada ya kuthibitisha
kuwa vifaa hivyo ni vya muhusika wa tukio hilo
kwa uthitisho ulio tolewa na meneja wake wa tawi
la magomeniâ€
Nilizima luninga ile haraka na kusimama kwa
muda bila kujua cha kufanya na kutoamini
nilichokiona na kukisikia kwa masikio yangu
mawili,mpaka nilipo kumbuka mazingira ambayo
nitakuwa nimeangusha ile waleti ndipo nilipo
gundua kuwa ni pale mgahawani niligeuka nyuma
kumtazama Magrety aliye kuwa kitandani nika
mkuta kashika kichwa na mdomo ukimtetemeka
kwa hofu, nilitupa macho yangu chini kisha
kuyainua na kupiga hatua kumsogelea na
kumwambia,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
“ Magrety mke wangu hapa sina njia nyingine ya
kukwepa kesi hii maana ile waleti ni kweli yangu
na vile ni vitambulisho vyangu pia kama
unakumbuka ile bastola nilisha wahi kuishika
tena
bila gropsi na wale mapacha walikuwa na grops
walivyo ichukua kwangu yawezekana huu mpango
ulikuwa endelevu ulioandaliwa
“ pia kwa kipindi chote hicho yawezekana ikawa
haikutumiwa na kama ilitumiwa basi watumiaji
walivaa gropsi ili zile alama za mikono zikipimwa
zionekane ni za kwangu Helman namjua anaakili
sana ya kijambazi japo mimi sio muhusika
inanibidi nikimbie tu ilibaadae nije kulea familia
yangu nakuomba usiwaambie chochote hawa
watoto maana wanaweza kuishi kwa hofu sana
katika maisha yao nami napenda wawe na amaniâ€
Nilibusu tumbo la mke wangu na kukiomba radhi
kiumbe kilichopo ndani..,,,,,,,,,
“ewe malaika usiye jua chochote kinacho endelea
naomba unisamehe sana kwa uwamuzi ninao
uchukua wa kuondoka bila ya wewe kuzaliwa
maana utakosa upendo wangu kwa muda na sina
ninachoweza kukuachia kwa sasa zaidi ya
kumbukumbu za maumivu utakazo kuja kuzikuta
utakapo zaliwa na kujitambua.
Maneno hayo niliyo kiambia kiumbe kilichopo
tumboni yali mchoma sana Magrety alisikia
uchungu usio na mipaka, machozi yalianzisha
ujirani na mashavu yalitililika vyakutosha acha
makamasi yalio kuwa yana toka kwa kupiga hodi
hata kile kilio cha kwikwi kikachukua nafasi
kinywani mwake. Nami sikutaka kupoteza muda
zaidi ya kuingia kwenye droo na kuchukua kiasi
kidogo cha fedha ambacho nilikiweka kama akiba
na kingine kumuachia Magrety kwa ajili ya familia
yangu na kuhusu hati za mali alikuwa anajua
wapi
zilipo.
nikampiga busu la mwisho na yeye ambalo
lilimfanya azidi kutoa machozi na kutaka kunizuia
nisiondoke lakini sikutaka kumuendekeza nikatoka
kwa nguvu mpaka nje kisha nikafungua geti na
kurudi kwenye BMW230 na kuiwasha na kutoka
mpaka nje ya geti
wakati najaribu kunyoosha matairi vizuri ilinianze
kuondoka ghafla nikaona vikofia vya polisi
vikibembea kwa nyuma ya gari lao walikuwa ni
wengi waliobebwa nyuma ya gari hilo huku mitutu
ya bunduki ikiwa mbele ya vifua vyao ilinibidi
nijisalimishe mwenyewe tu.,
walishuka hata kabla gari lao halija simama vizuri
na kunivamia moja kwa moja walinijua baada ya
kuoneshwa na meneja wangu ambaye ndiye alie
waleta nyumbani kwangu.
Walikamata mikono yangu na kunifunga pingu
kwa
nyuma baada ya kuigeuza mikono yangu kisha
kunirudisha mpaka ndani kwangu askari wengine
walijigawa kwenye vyumba vingine wakikagua
kama kuna siraha au zana zingine amabazo zina
husiana na ujangili kiukweli nilijisikia vibaya sana
nilipo waona watoto wangu pamoja na mke
wangu
walivyo kuwa wananililia lakini askari hao
hawakujali lolote walishindwa hata kumuhurumia
mke wangu kwa hali aliyo nayo, walikuwa
wakimsukuma kila alipo kuwa ananisogelea na
kunililia,
Sikuweza kujikaza katika hali hiyo nami machozi
yakawa yananitoka kila nikiwatazama familia
yangu ikitapatapa kwa kukosa msaada hata wa
kubembelezwa, maaskari hao walipo maliza
ukaguzi wao walinitoa nje huku nikiwa bado nina
pingu mikononi jambo ambalo lilinifanya nione
aibu
kutokana na wingi wa watu hasa majirani zangu
walivyo kusanyika kushuhudia tukio hilo,
nilipandishwa kwenye gari lao kama ng’ombe
wanao pelekwa mnadani kisha kuondoka kuelekea
kituoni.
ITAENDELEA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni