Nakumbuka ilikuwa ni siku ya alhamisi
nilipokutana naye kwa mara ya kwanza.Siku hiyo nilikuwa shuleni,alipokuja
shuleni kwetu.
Nilikuwa nje nikimalizia muda wa mapumziko,niliegemea kwenye
nguzo ya nje ya darasa letu,nimeinama nikiwaza juu ya ombi la John la kuwa naye
kimahusiano ya kimapenzi aliloniambia jana.
Nilipoinua
kichwa changu nilimwona mvulana mgeni katika macho yangu, mrefu na mwenye mwili
mwembamba,alikuwa amependeza sana.Si kwamba alivaa vipi ,ni jinsi ya rangi ya bluu
na fulana nyekundu,ndiyo iliyomfanya aonekane simati na kunitoa udenda.
Alipozidi kusogea karibu na kuonekana barabara mapigo ya moyo yalibadilika nikaona yanaanza
kwenda mbio mbio.Mfumo wangu wa damu ulibadilika,damu ikaanza kwenda kwa kasi
zaidi.
Ni upendo mkubwa uliojitokeza baada ya kuonana na Krisi,moyo
wangu ulivutiwa sana na mwonekano wake tu,ingawa sikuwa namfahamu tabia yake na
hata jina ,sikulifahamu ,lakini hayo yote hayakuwa na nafasi katika fikra
zangu.
Nilimtazama sana macho yangu yalikuwa kama yamepigwa na shoti
ya umeme kwani yaligeukia huko yakaganda kumtazama.Nilitamani aniongereshe
ingawa sikuwa na uhakika kama angeweza
kufanya hivyo.
Nikiwa bado nafikiria na kumungoja ili nione kama atapita
nilipokuwa nimesimama,Yule kijana alizidi kusogea karibu yangu.
Moyoni nikawa namshukuru Mungu, nikimwomba japo yule kijana
aseme neno moja tu.
’’Anti mambo,antii mambo’’
ni salamu ya Krisi nikiwa kama
niko usingizini au nimezimia,hivyo nimesituliwa ,nikamjibu kwa kusituka ‘’mh! salama’’.
’’Eti unamfahamu Juma
anayesoma Kidato cha nne’’ aliniuliza
swali,nikamjibu kwa kutafakari kwanza ni Juma yupi,nikamwuliza Yule Juma bonge bonge anayesoma kidato cha nne B?
Naye akasema ‘’ndiye
huyo,ninaweza nikamwona ,mimi ni kaka yake nimekuja kumtembelea? ‘’Nilimwomba
anisubirie kidogo ili nikamwangalie,kama atakuwemo darasani.
Bahati nzuri nilipoenda nikakuta darasa limetulia utazania
wote walikuwa wamesinzia,kila mtu akipekua daftari lake na kumsubiria mwalimu,nikauliza
kwa nguvu kwa kutanguliza kuomba radhi kwa usumbufu,
‘’ Eti juma yupo, kuna
ndugu yake anamtafuta, yuko pale nje?”.
Juma akajitokeza ‘’yuko wapi huyo ndugu yangu”.Macho yote
yakageukia kwa Juma,watu wakafunika daftari zao na kumtazama yeye.Juma aliinuka
kwenye kiti chake akanifuata, nikwamongoza tukaenda pale alipokuwa amesimama
Krisi.
’’ Aah vipi Krisi ,karibu sana kaka’’ Juma akimkaribisha
Krisi huku akimsogelea na kumkumbatia,
Krisi naye alijibu,
“nashukuru sana kaka”
“kiskani vipi mwanangu?”
‘’ Poa tu wote, ni wazima,wanakupa hai tu”
Baada ya
kumaliza kusalimiana ,mimi nikiwa nimesimama nikiwasikiliza tu,nijue nini
kitakachoendelea,Juma alimwambia Krisi amsubirie akachukue daftari zake ili
waondoke.
Krisi akajibu ‘’ hamna noma utanikuta nakusubiri.’’
Sasa tukabaki mimi na yeye,nikavuta pumzi
,nikijiuliza namna ya kumuanza,na mimi ni msichana ,nikimwambia ai lavu yuu ataniona
mimi kicheche,kwa maana ni mara ya kwanza kuonana naye na mimi ni msichana.Maswali
yakazidi kuzunguka katika ubongo wangu wa mbele,huku ukimya ukiwa umetawala.
‘’anti nashukuru sana kwa kunisaidia” haya ni maneno ya Krisi
baada ya muda kama wa dakika mbili ya ukimya akinishukuru.
‘’Hamna shida kaka
kawaida tu ‘’ nikaona hii ndiyo nafasi ya kuitumia ,nikiwa na falsafa ya
kimichezo inayosema “one chance one goal” yaani ikimanisha “nafasi moja ,goli
moja” nikamuuliza ,
’’ eti kaka unatokea wapi?”
‘’natokea igoma’’ .Nikamwuliza swali
lingine “unasoma?’’
‘’ee mimi ni mwanafunzi wa arusha teki”.
Sikuishia hapo
nikamuuliza habari za masomo,
‘’ masomo
yako freshi tunakomaa mdogo mdogo’’
Hata hivyo
yeye alionekana kutotaka kujua habari zangu kabisa kwani hakuniuliza lolote
kuhusu mimi masomo au habari za hapa shuleni.
Nilipoishiwa maswali nikanyamaza ndipo ukimya ukatanda tena
kabla hajaja Juma.Lakini baada kama ya dakika mbili nikasikia akiniuliza ,
‘’hivi wewe anti jina lako nani”
Kwa haraka
haraka nikamjibu,nikajiseme amoyoni haya ndiyo niliyokuwa nayasubiria ‘’ naitwa
Aneth John”.
Ingawa
tayari nilikuwa nimesikia kuwa anaitwa Krisi nikaona nimuulize nione mwitikio wake ’’ naitwa Krisi’’. Ndipo nikaanza kumsifia
‘’aah jina zuri sana’’.
Akionyesha tabasamu
akasema ’’asante! hata wewe una jina zuri’’.
Hii ikamfanya afunguke,na kuanza kuniuliza
maswali mbalimbali.
“walimu vipi hapa”
‘’ kwa kweli walimu ni tatizo hasa mwalimu wa fizikia
na hesabu hatuna kabisa,huwa wanaletwa tu kutoka shule mbalimbali kutuelekeza
kwa wiki moja katika mwezi mmoja’’
‘’ poleni sana,hapa inabidi ukifunga
ukasome tuition tu, kama unataka ufaulu vizuri masomo hayo”
“huwa tunafanya hivyo”
Akazidi
kuuliza ‘’ kwa hiyo wewe unaishi kwenu au na wewe umepanga?’’
‘’mimi ninaishi nyumbani,wazazi wangu wanakaa hapa hapa ”.Tukiwa tunaendelea, juma akaaja
‘’twende kaka”
Basi Krisi akaniaga ‘’aneth nashukuru sana
tutaonana Mungu akipenda”
Niliumia sana moyoni kwani nilikuwa nimeanza
kupata faraja kubwa.Ile tu kuongea naye ,nilikuwa najisikia kama kwamba tayari
alikuwa amekuwa wangu.
Nilitaka
kushindwa kumjibu ,nikajilazimisha ili nisionekane kuwa tayari nilikuwa
nimezimika niilimjibu kwa unyonge ‘’ poa safari njema”
Juma aliponiona najibu kwa unyonge akahisi
kitu ,akaniambia
‘’ hata hivyo atakuwepo geto njoo mpige pige stori kabla
hajarudi sikani “.
Moyo wangu uliripuka furaha, ingawa
sikuonyesha kuwa nimefurahi kiasi hicho,nikajifanya kama sina uhitaji
sana,nikamwambia Juma ‘’nitacheki kama nikipata muda nitakuja”
‘’powaa baadaye”
Waliniacha
wakaondoka,mimi nikabaki kumalizia muda wa kuwa shuleni siku hiyo uliokuwa
unaisha saa nane na nusu.Yalikuwa yamesalia kama masaa matatu,tutakapotawanyika
kurudi nyumbani.
Baada ya kuondoka kiukweli , sikuwa tena shuleni wala
darasani akili yangu yote nilikuwa namfikiria Krisi.
Ni mwanaume niliyekutana naye mara moja lakini alifanikiwa
kwa asilimia kubwa kuteka sehemu kubwa ya moyo na akili yangu.Kila nikimwangalia
katika macho ya akili yangu mwili wote ulisisimuka.
Kila mwalimu aliyeingia darasani kufundisha alinitambua kuwa
siko sawa kwani sikuwa nimechangamuka hata kidogo ila nilionekana kama niko
kwenye dimbwi la mawazo.
“unawaza nini aneth leo mbona unaonekana
hauko sawa?” mwalimu mmoja wa Kiswahili aliniuliza.
“mbona nipo sawa mwalimu”
‘’uko sawa
wewe,mbona tangu niingie umeinama tu unaelewa ninachokifundisha kweli?”
Nikaa kimya
sikujibu lolote.Alipoona hivyo hakutaka kunifuatilia sana akaendelea
kufundisha,nami nikaendelea kuweka mawazo yangu kwa Krisi nakuweka kando swala
la kumsikiliza mwalimu.
Nilihisi siku hiyo muda ulikuwa hausongi mbele kama inavyokuwa
kwani nilitamani ufike mapema ,tutawanyike ili mimi niende nikaoanane na Krisi
getoni kwa Juma.
Nikawa namwoma Mungu ayakimbize masaa ili muda wa kutowanyika
ufike ,ili niende nikamwone tena Krisi
Nilimwomba pia Mungu anisaidie ili atambue nini ninachokiwaza
moyoni mwangu.Tunajua sote kuwa kwa mwanamke kumuanza mwanaume ni vigumu sana
ingawa inawezekana.Nikiwa katika kuwaza hivyo nilijikuta nimepitiwa usingizi.
Usingizi ulinoga sana siku hiyo na bahati nzuri mwalimu wa
somo la histori hakuwepo siku hiyo kwa hiyo hakukuwa na kipindi
darasani,nilichapa usingizi kama li saa moja hivi.Nikiwa ndotoni mawazo yangu
yalielea kumuota Krisi tu,nilimwona kama
tuko pamoja tunaeleka katika sayari Fulani ya mapenzi.
Tukiwa hewani tunaelea ,tuliongea kwa furaha huku
tukikumbatiana,pigana busu na kuzama katika mahaba mazito.
Nikaja kusituka pale niliposikia ninaamushwa,kwaa kuwa jina
la Krisi ndilo lililokuwa limetawala sehemu kubwa ya ubongo wangu wa mbele
nilijikuta naitika “naamu Krisi” akili yangu iliporejea katika mfumo wake wa
kawaida nikagundua kuwa hakuwa Krisi bali alikuwa mwanafunzi mwenzangu alikuwa
akiniamsha baada ya kengele ya
kutawanyika kwenda nyumbani kugongwa na
mimi nilikuwa naendelea kufaidi usingizi.
Niliamuka,nikajifuta macho yangu kwa leso yangu kuondoa tongo
tongo,nikijinyosha nyosha mikono na shingo,huku nikipiga miayo.
Nikakusanya madafutari yangu huku nikimshukuru julieth kwa
kuniamsha.
‘’hamna shida,lakini mbona unaniita Krisi au Krisi wa wapi?”
‘’ndoto za usingizini tu hizo,hamna shida”
‘’ok{sawa) fanya haraka tuwahi paredi”
‘’haya ngoja nichukue sweta langu tuondoke’’
Tulienda
paredi,tukafika tukajipanga kwenye mstari.Mwalimu alikuja akatoa matangazo
kisha akatutowanyisha.
Kwa kuwa nilikuwa ninaenda kwa kina Juma ilibidi nimuarifu
mdogo wangu Pendo ili akawape taarifa wazazi watakapohoji kwamba nimeenda wapi.
Nilimwambia mama akikimuuliza amwambie tu kwamba nimebaki
shuleni mwalimu ametuambia tubaki ili tufanye prakitiko.
Alikubali ila akaniuliza swali ‘’kwani dada unaenda wapi
kiukweli?”
‘’wew nenda nikirudi nitakuja nikwambie”
nilimwambia hivyo huku nikiondoka kuelekea kwa kina Juma.
Sikuwa nimefika alipokuwa anaishi Juma kwa hiyo ilibidi
niende na mwanafunzi mmoja aliyepanga nyumba moja na akina Juma.
Baada ya dakika chache tukawa tumefika kwani walipanga karibu
na shule.yule dada akanionyesha mlango
wa chumba cha akina Juma,yeye akaingia kwenye chumba chake.
Nikamshukuru kisha nikasogea mlangoni nikapiga
hodi
‘’karibu”
‘’hodi mpaka
ndani”
‘’ingia tu
hapa ni geto”
Nikafungua
mlango uliokuwa umeegeshwa na kuacha viatu vyangu mlangoni.
“ingia tu na viatu ,wewe usihanye”
“nashukuru,nilikuwa
nimeshavua kwania kuna mtu anaweza kuja kuchukua?”
“hamna mwizi mitaa yetu hii”
Niliingia
ndani nikakaribishwa kukaa kwenye,situri.
Krisi
yeye alikuwa amejilaza kwenye godoro,nilipofika akainuka,na kunikaribisha,
“karibu miss
aneth ,hapa ni kwetu sote” Alionekana kuwa ni kijana mtaratibu, mstarabu na mwenye
moyo wa kujali, kitu ambacho kiliongeza kumpenda zaidi.Alinijali sana ,aliagiza
soda na keki mbili kwa ajili yangu ,huku tukisubiria pia chipusi mayai ambayo
aliagiza nitengenezewe kwasababu wao walikuwa wamemaliza kula.
Alitambua kuwa nimetoka shuleni nimechoka na nina njaa ndiyo
maana akatafuta chakula ili tuweze kuongea vizuri kwa maana ukiwa na njaa hata
kuongea unaweza kushindwa.
Kwa kweli kadri muda ulivyokuwa ukienda ndivyo nilivyozidi
kudata kwa Krisi,alinichanganya sana kiasi cha kufukia kushindwa hata kuongea.
Niliingiwa na usingizi wa mahaba,nikainuka pale kwenye situri
nikajilaza,alipokuwa Krisi kwa kisingizio kuwa naanza kujisikia vibaya,kichwa
kilikuwa kinanigonga.
Krisi alienda kumuita Juma na kumpa hela akanichukulie dawa
za kichwa kisha akarejea ndani na kunituliza,
“usihofu Aneth utapona,nimemtuma Juma ameenda kukuchukulia
dawa”.
“Asante,ila usingehangaika hivyo kwani nadhani ni uchovu tu”.
“usijali uhai,ndiyo kitu cha muhimu kwa mwanadamu”.
Nilianza kumlaumu moyoni,ina maana hajaelewa kuwa haya ni
mapozi tu?
Alichukua shuka akanifunika kiwiliwili akaniambia,nikute
nimepumzika nikisubiria dawa.
Nilivuta shuka nikajifanya niko siliazi nimelala,kumbe mawazo
yote yako kumuwaza Krisi.Baada ya muda mfupi Krisi aliniamsha kwa kunipapasa
miguu na vidole vyangu vya miguu,akiniambia niamke ninywe dawa.
Kulingana na raha niliyokuwa naipata,niliekiti nimesinzia ili
aendelee kuishika shika miguu yangu.
Alipoona siamki aliniacha niendelee kulala,nitakunywa
nitakapoamka.
“dada naona alikuwa amechoka,umemwamsha hivyo hata hajielewi” nilimsikia Juma akimwambia Krisi,
“inawezekana,ngoja tumwache apumzike”.
Baada ya kumaliza kusema hivyo,Krisi alianza kuangalia picha
za Juma zilizokuwa kwenye Albamu,Juma yeye alichukua daftari akaanza kujisomea.
Krisi alipomaliza kuangalia picha alisogea karibu na kichwa
changu ,kisha akaanza kunipapasa papasa hasa kwenye kichogo au pale medulla
obulongata hukaa.
Uzalendo ulinishinda ,ikabidi niamke nimwambie laivu kuwa
nampenda.
Alipoona nimeamuka aliondoa haraka haraka mkono wake kwenye
kichwa changu.Nijishosha kana kwamba nilikuwa kwenye usingizi mzito.
“Vipi kichwa,kinaendeleaje?”
“afadhari ,kimepunguza maumivu”
“pole”
“asante”
“tumekuletea dawa,hii hapa” alinipa
Nikaipokea tu ili nisimhuzunishe kwa kuona kwamba amefanya
kazi bure lakini sikunywa niliiweka mfukoni nikamwongopea kuwa nitaenda kunywa
nikifika nyumbani.
Nilinyanyuka pale kitandani nikajiandaa kwenda nyumbani,kwani
usiku ulikuwa umekaribia kufika.
Niliamuka nikanawa uso,nikajifuta na kujipaka mafuta ya baby
care niliyoyakuta pale .kisha nikamwomba Krisi anisindikize.
“si ungelalala huku tu”
Krisi
alinitania
“aa,hapa nitalala
wapi?”
“si humo
,tunalala wote”
“subutuu..”
Niliposema
hivyo akanishika mkono wangu akiniambia tuondoke asije mama akaja kunitafuta.
Tulianza safari kuelekea nyumbani,huku Krisi
akiwa amenishika mkono wangu wa kushoto.
Tukiwa njiani,yeye mwenyewe Krisi
alijiingiza kwenye kumi na mbili zangu,baada ya kuniuliza kama ninampenzi ama
mchumba?nikagunduamkuwa na yeye alikuwa ameanza kunizimia.
Sikutaka kuvunga kuwa ninaye kwani niliogopa
kuwa angeweza kukata tamaa,ikabidid nimwambie ukweli kuwa sinaye.
“je akijitokeza sasa hivi mtu akakuomba awe
mchumba wako,utakuwa na maamzi gani?”
“nitamwangalia,na
mchumba mwenyewe,kama nikimwona anafaa,nitakubali”
“kwani unahitaji
awe na sifa gani”
Nilianza
kuporomosha sifa nyingi ambazo yeye alikuwa nazo zote.Akaniuliza kama sifa hizo
yeye alikuwa nazo.
“unazo” nikajiweka kwenye ndoano mwenyewe,bila
taabu.Niliposema hivyo alinitazama usoni,akanisimamisha,kwani tulikuwa sehemu
ambayo watu hawakuwepo njiani,alikanishika shingoni,na mimi nikamshika
kiunoni,tayari tukaingia sayari nyingine kwa sekunde chache sana kwasababu
ilikuwa njiani.
Kila
mmoja aliramba mdomo na ulimi wa mwenzake,na kupigana busu nyingi nyingi kisha
tukaendelea na safari kwa sababu kuna watu walikuwa wanakuja mbele yetu.
Krisi alinieleza kuwa ananipenda
sana,ingawa hajanifahamu vizuri lakini aliniona kuwa ninafaa kuwa naye
kimapenzi.Kwa hiyo sote tulipendana,kwani mimi nilifikiri kuwa ninampenda mimi
tu ,nikashangaa kuona kuwa na yeye alikuwa ameshanipenda.
Hivyo ndivyo safari yetu ya mapenzi
ilianza,tulipokaribia nyumbani Krisi aliniaga kuwa hataweza kufika
nyumbani,anaogopa wazazi wangu.Mimi nilimlazimisha tukafika mpaka nyumbani.
Nilimkuta mama anaandaa chakula cha
jioni,tulimsalimia mama.Baada ya salama nikamtambulisha Krisi kwa mama kuwa
alikuwa mwanafunzi mwenzangu,akamkaribisha.
Tuliingia ndani,nikamkaribisha Krisi
kwenye kochi,akakaa,mimi nikaenda kubadilisha nguo,nikavua nguo za shule na
kuvaa nguo za nyumbani.
Baada ya kumaliza kuvaa,nilikuja sebuleni
alipo asali wangu wa moyo.Aliniomba maji ya kunywa,nikampa.
Nilipokaa akaniomba
kuwa anataka kurudi nyumbani ,kwasababu giza la saa moja lilikuwa limeanza
kuingia.
Nilimkubali, tukaenda kumuaga
mama.Mama alimwomba Krisi asubiri chakula ,lakini hakukubali kwa kudai kuwa anawahi,atakuja siku nyingine
kula.
Tuliondoka,nikamsindikiza
Krisi.Nilienda naye mpaka sehemu moja hivi ambapo kuna nyumba ilikuwa inajengwa
na hakukuwa na watu kwenye nyumba jirani
ambayo nayo ilikuwa inafanyiwa finishingi,hivyo hawakuwa wamehamia.Tuliingia
ndani ya nyumba hiyo tukakaa na kuanza
kupiga stori.
Nilikaa kwenye mapaja ya Krisi,
tukiendelea kupiga stori,za kufahamiana zaidi,huku akizungusha mikono na vidole
vyake katika sehemu mbalimbali za mwili wangu.Alikuwa fundi wa kucheze sehemu
mbalimbali za mwili wangu,akizungusha mikono yake kwenye tenesi zangu,kiuno na
uti wa mgongo wangu.
Alivyokuwa akinishika shika ilinifanya nishindwe kuendelea na
stori,nilizidiwa sana kwa jinsi alivyokuwa akitembea katika sehemu zangu
nyeti.Nilijiachia nikalala kwenye nyasi zilizokuwemo ndani.Krisi akakaa juu
yangu kwenye kiuno changu ,akanifunua kwenye tumbo langu akaanza kuramba kitovu
changu huku akielekea kwenye kifua changu.Hali hii ilinifanya nizidi
kuchanganyikiwa kuanza kutetemeka.Nikamshika kwa nguvu Krisi,hata hivyo
alishtuka akashuka juu yangu ,nikamshikiria lakini akaniomba sana tusifanye
siku hiyo.nilimlaumu kwa kuniandaa kimchezo harafu akaahirisha mechi,wakati huo tayari nilikuwa nimimeingia katika hali ya mchezo,kuahirisha mchezo iliniumiza
sana.
Hakutaka tucheze mechi siku hiyo kwa kuwa hatukuwa na Mwamvuli na
tulikuwa bado hatujazoeana.
Aliniaga ,akaondoka na mimi nikarejea nyumbani huku jasho la
mazoezi tuliyofanya likiwa linanitoka.Nilienda nakimbia ili nimuwahi baba kabla
hajarudi toka kazini, saa mbili.
Nilimkuta mama ameshaivisha
chakula,nikaenda kwanza kuoga kabla ya kula.Nilipomaliza kuoga, mdogo wangu
pendo alitenga chakula,tukala.
Baada ya kula nilienda kitandani kulala.Sikutaka kuangalia
hata muvi ya siku hiyo,kwani nilikuwa nimechoka sana na akili yangu haikuwa
sawa .Hata kujisomea nisingeweza kwani mawazo yangu yote yalikuwa kwa Krisi.
Baba alipokuja aliniulizia akaambiwa
nimelala.Pendo akatumwa kuja kuniita.Nilienda ,akaniuliza kwanini ninalala
mapema sana siku hiyo ama nilikuwa naumwa?
Nilimwambia baba kuwa nilikuwa
nimechoka tu,kwa kuwa nilikuwa nimeshinda shuleni.
Akaniruhusu kwenda kulala,nikaenda
kulala.
Usingizi
ulipaa kabisa,akili yangu ilikuwa ikizunguka katika kumuwaza Krisi,nilikumbuka jinsi alivyonifanyia
kwenye nyumba ile.Nilikumbuka soda na keki,chipsi na jinsi alivyonijali pia kwa
kwenda kuninulia dawa baada ya kuona kuwa naumwa.
Nikajisemea moyoni kuwa yule ndiye anafaa ndiye anafaa
kuwa mwenzi wangu wa maisha,na hili ndilo chaguo la Mungu kwangu kuwa
awe wangu wa maisha.
Nilikumbuka hata kitendo chake cha
kukataa kufanya kitendo cha wakubwa cha usiku,nikatambua kuwa si mwanaume
mpenda uasherati,kwani angekuwa mpenda kufunga magoli asingekubali kuacha
kufunga, kwa kuwa tayari nilikuwa nimeliacha goli wazi ili afunge.
Nikiwa katika kumwaza mahabuba wangu
wa mtima wange,nilimsikia mama yangu akiniita kwa nguvu ,nikanyanyuka
nikamfuata,akanipa simu kwa kuniambia ni simu ya mwalimu wangu.
Nilipoipokee nikagundua ya kuwa alikuwa Ni Krisi
alijifanya kuwa ni mwalimu wangu,hivyo ananiomba nije na kitabu chake
kesho.Alitaka kunijulisha kuwa amefika salama,na kunitakia usiku mwema.
Hatukuweza kuongea sana kwasababu
mama alikuwa amesimama akisubiria simu yake aende kulala.
Nilikubali
tu nakumjibu kwa kifupi kisha nikata simu asije mama akashtukia dili.Nilimpa
mama simu yake nikamshukuru.Baada ya kuipokea akaniuliza habari za Krisi kama
nilikuwa ninamahusiano naye ya kimapenzi,nikakana.Mama alianza kusifia uzuri wa
Krisi na unadhifu wake.
Akaniuliza kuwa
anakaa wapi yeye,sikumwambia kuwa alikuwa mgeni kwa hofu kuwa angegundua
kuwa nilikuwa nina uhusiano naye kwani isingewezekana mgeni tu awe rafiki yangu
nimlete mpaka nyumbani bila mahusiano ya kimapenzi,nikamwambia kuwa alikuwa
anaishi sehemu ambayo Juma ,nduguye alikuwa akiishi.Akanijibu sawa.Nilimuaga
mama kuwa naelekea kulala,nikaondoka.
Nilimwacha mama akiwa amesimama huku
akionekana kama alikuwa akifikiria inshu Fulani nikataka nimwambie ukweli, lakini
moyo wangu uligoma nikaogopa kuwa huenda mama alikuwa ananitega.
Nilirudi kulala ,usiku karibu wote nilikuwa
na mwaza Krisi,nikilala na nikiamka.Kwa sehemu kubwa alifanikiwa kuiteka akili
na mawazo yangu,nilishindwa hata kusoma katika usiku ule.Tulikuwa na kawaida ya
kuamuka saa tisa,mama alikuwa anatuamsha ili tujisomee na kujiandaa kwenda
shuleni,lakini siku hiyo sikuweza kuamka .Mama alijaribu kuniamsha mara nyingi
lakini sikuweza kuamka.Baba akamkataza asiendelee kuniamsha huenda nilikuwa
sijisikii vizuri.
Nilipoamka saa kumi na mbili
asubuhi,mama aliniuliza kama nilikuwa naumwa kwasababu aliniamsha sikutaka
kuamka,nikamwongopea kuwa nilikuwa najisikia vibaya.Kichwa kilikuwa kizito
lakini sasa hivi najisikia vizuri.
Nikaenda kuoga,nikamaliza nikavaa
nguo za shule ,nikaanza kwenda shuleni.
Nilienda
moja kwa moja hadi kwa kina Juma ili nikaonane na Krisi.Niliwakuta bado
wamelala.Niliwagongea ,Juma akaja kunifungulia , alishituka aliponiona,akarudi
ndani.Akaenda kuvaa fulana,kwani alikuwa amevaa pensi tu hapo mwanzo.
Nilimuuliza, Krisi hajaamka?
“bado,alichelewa
sana kulala jana?”
“hawezi
kuamka?
“Labda
nijaribu kumwamsha” aliingia ndani akaenda kumuamusha Krisi akimweleza kuwa
kuna mgeni wake nje.
“mgeni gani au aneth?”
“nani
mwingine zaidi ya huyo?”
“mwambie
anisubiri hapo nje”
Alikuja nje
akaniapa situri ,nikakaa.
Baada ya
muda mfupi Krisi alikuja ,akanikaribisha.
“asante”
“za tangia
jana”
“nzuri tu”
“vipi
ulimuwahi mzee?”
“ee,nilipofika
,nikakaa kidogo na yeye akaja”
“du! Kwa
hiyo ungechelewa kidogo tu ,ingekuwa baraa”
“mzee yule
alivyo hataki kutuona saa mbili hatuja fika nyumbani,sijui ningemdanganyaje?
Yeye anataka akirudi kutoka kazini awakute wote.Asipowakuta atauliza mno fulani
kaenda wapi?”
“haha haha,
inaonesha mzee anawapenda sana”
“kusema
ukweli baba anatujali sana”
“ok !ngoja
ninawe uso basi nikusindikize”
“poa fanya
fasta kwa maana ,taimu limeenda”
“poa”
Aliondoka
akaenda kunawa uso ,akaniacha nimekaa nje,huku nikiangalia simu yake aliyoniachia.
Baada ya muda mfupi alikuja yule dada aliyenileta hapa
jana,akitokea chumbani mwake.Nikahofu kidogo kuwa tayari naenda kuumbuka ila nilijiamini kwa
kuwa yeye alikuwa anasoma kidato cha pili asingeweza kuvumisha habari zangu
masikonga.
“vipi
aneth?”
“poa
tu,naona unatangulia?”
“ee,vipi
wewe tusepe”
“tangulia
nitakukuta”
“poa basi mimi natangulia”
“hayaa”
Baada ya
sethi kuondoka,nilikaa muda kidogo Krisi alikuja,alikuwa amevaa nguo nyingine
mbali na zile za jana ,alipendeza kweli kweli,nikaanza kujisifu moyoni kumpata
mwanaume nazifu kiasi hicho.Nikamuuliza kama tayari ili tuanze safari,akasema yuko
tayari tuanze safari,tukaondoka.Tukiwa njiani Krisi aliniongeresha,
“leta habari
sasa Aneth”
“mimi niko
byee ,sijui wewe?”
“hata mimi
niko safi”
“basi
vizuri”
“ila leo
mimi naondoka”
“ee unarudi
nyumbani,kwanini usingeenda kesho?”
“hata mimi
nilikuwa nimepanga hivyo ila mzee kakomaa nirudi leo”
“kwaa hiyo
utaondoka saa ngapi?”
“saa nne”
“kama ni saa
nne nisubirie saa sita ili nije nikusindikize kwa maana leo ni siku fupi”
“sawa mimi
nitakusubiria”
“Asante”
Tulitembea
kidogo tukipiga sitori za kuhusu masomo,Krisi akaniaga,
“ngoja mimi
nikuache”
“nashukuru
kwa kunisindikiza”
“haya,
masomo mema”
“nashukuru
na wewe pia siku njema”
“nakupenda”
“na mimi
nakupenda sana Krisi” niliongea kwa sauti ya kimahaba.
Nilimwacha, nikawahi
shuleni kwani tayari muda ulikuwa umekaribia kuisha wa kufanya usafi
asubuhi na eneo langu lilikuwa chafu.
Nilijitahidi kutembea kwa kasi ili
nifike nifanye usafi eneo langu kabla ya muda wa usafi haujaisha.Nikafika
nikaweka begi langu darasani ,kisha nikaenda kuchukua mfagio.Nilipopata ufagio
,nilienda kwenye eneo langu la usafi ,nikafika ,nikaanza kufanya usafi.
Wakati naendelea kufanya usafi,John
alikuja pale nilipokuwa nafanya usafi
“mambo
aneth” John alinisalimia,
“poa “
“buku vipi?”
“safi tu”
Nilipomjibu
hivyo aliomba ufagio wangu ili anisaidie,nikampa nikiwa namshukuru.
Akanza kufagia mimi nikiwa nimesismama.Baadaye akaniuliza juu
ya ombi lake la kuwa mpenzi wake aliloniambia juzi.
“mimi tayari
na nina mtu,tunapendana sana ,jaribu kwingine”
“lakini Aneth
ujue mimi nakupenda sana,ninateseka kwa ajiri yako”
“hata mimi
najua unanipenda lakini tayari mimi na ninamtu ninayempenda na yete ananipenda”
Aliendelea
kunishawishi nilikubali ombi lake,nikaamua kunyamaza kimya ili aendelee
kunisaidia kufagia ,mimi niachane
naye,kwani mimi mawazo yangu yalikuwa kwa Krisi.
Alipoona amegonga mwamba,alitupa
ufagio wangu akaondoka kimya kimya akionekana mwenye sura ya kunyong’onyea.Hata
hivyo alikuwa amemaliza kufagia eneo langu lote ambalo nilikuwa nafanya
usafi.Nikazoa takataka ,nikaenda kuzitupa kwenye shimo la taka.
Baadaye nilienda paredi.Tukaimba
wimbo wa taifa na wa shule.Tulipomaliza ,Mwalimu wa zamu aliwaadhibu wale ambao
hawakufanya usafi,walioandikwa majina yao.Baadaye tuliruhusiwa tukaenda darasani.
Siku hiyo nilikuwa nimechangamka
sana,kwa sababu ya Krisi,niliona masaa yalikuwa yanaondoka haraka sana.Kila
mwalimu aliyekuja nilijitahidi
kumsikiliza vizuri na kuuliza maswali sehemu ambayo sikuelewa .Wanafunzi
wenzangu wakashangaa sana,kwani si kawaida yangu.
Muda wa mapumziko ulifika,tulitoka
tukaenda kunywa chai kantini.Tulipotoka nje twende kunywa chai,nikiwa na rafiki
yangu Perepetua nilishangaa kumwona Krisi akija, tena karibu na darasa langu.
Nilienda kumpokea ,tukasarimiana,na
kumtambulisha rafiki yangu Perepetua kwa Krisi.Krisi alifurahi kumfahamu
Perepetua.
Akaniambia amekuja kunichukua
tukanywe chai getoni kwao ,ili tuagane
aende nyumbani.
Nilimuaga perepetua , nikaongozana
na krisi,hadi nyumbani kwao.Nilimwacha Perepetua akiwa anatumezea mate kwa
jinsi tulivyokuwa tukionekana tulipokuwa tukitembea pamoja .Sikutaka kwenda na
peereptua kwa sababu ya kuhofia kukosa uhuru wa kuinjoi na Krisi.
Tulifika nyumbani kwa Juma
,tukamkuta yuko ndani.Tulipiga hodi akatukaribisha,nasi tukaingia wote,Krisi akiwa
amenishika kiuno changu.Tukakaa wote
kwenye godoro.Krisi akanilalia kwenye mapaja yangu.
Juma akatenga chai,ilikuwa ni chapati
za mayai na chai ya maziwa.Krisi akainua kichwa chake,akanikaribisha
chai.Tuliamuka Juma akatunawisha ,tukanywa chai.
Tulipomaliza kunywa chai ,Krisi
akaenda kuoga, tayari kwa kuanza safari ya kurudi kwao Igoma.Alipomaliza kuoga
alibadilisha nguo alizokuwa nazo,alivaa nguo nyingine si zile za asubuhi,na
zenyewe zilimtoa sana.
Juma akachukua begi lake,nikamwomba nilibebe akanipa,
tukaanza kumsindikliza kwenda kivukoni Kamanga.
Tulimsindikiza hadi sehemu moja
iliyoitwa chemagati Juma akaomba kutuacha tuendelee yeye arudi nyumbani.Waliagana kwa kukumbatiana ,Juma
akamshukuru sana Krisi kwa kuja kumtembelea na kumtakia safari moja.Krisi
alimshukuru Juma kwa kila alichomfanyia na kumtakia masomo mema.
Mimi niliendelea naye,tukapeana
ahadi nyingi za kwamba tusisaritiane.Akaniahadi kuwa ataendelea kunipenda mpaka
anaingia kaburini, ,hatanisariti na atakuwa anakuja kunitembelea.Mimi pia
nilimwahidi sitaigia kwenye dimba kucheza mpira na mwanaume mwingine zaidi yake.
Nachokumbuka cha mwisho ,Krisi
alinisogelea karibu akashika shingo yangu akanisogeza karibu yake akanipiga
busu ya kwenye paji la uso na busu la pili kwenye shavu langu la kulia.Aliniaga,kwa
unyonge sana akachukua begi lake nililokuwa nalo mimi.Akanitazama sana na mimi
nikiwa namtazama sana huku machozi yakiwa yamenilenga,nilimuaga kwa ishara
,akaanza kuondoka na mimi nikarejea shuleni kumalizia vipindi.
Nilirejea shuleni nikiwa na furaha
yenye mchanganyiko wa huzuni.Moyoni nikijiuliza ni lini nitakutana na wewe
tena? Ni lini tutakuwa wote pamoja?
Nilifika shuleni ,nikamalizia
vipindi vilivyokuwa vimesalia. Siku zote siku ya ijumaa huwa ni fupi kwa ajiri
ya waisilamu kwenda kuabudu.kwa hiyo ikifika saa sita vipindi vyote husitishwa,mpaka
juma tatu.Wengine huenda kwenye vipindi vya dini na wengine huondoka kwenda
nyumbani.
Mimi niliamua kutoenda kwenye
kipindi cha dini badala yake nilienda nyumbani.
Sikumkuta mtu nyumbani ,mama alikuwa
bado yuko kazini,Nikafika nikafungua mlango nikaenda kitandani kwangu,nikafika
nikajilaza.
Muda kidogo mama naye akafika kutoka kazini kwake
,nikaenda kumsalimia na kumpokea mzigo aaliokuwa amebeba mkononi .
Mama alianza kuandaa chakula cha mchana,nikasaidizana
naye,hadi tukaivisha.
Pendo ,mdogo wangu akawa amesharudi toka
shuleni,mama akamwagiza alete maji ya kunawa na ya kunywa ,akatenga tukala
chakula .Nilikula kidogo tu kwasababu bado nilikuwa nimeshiba chapati za kina
Juma,nilinawa nikaenda kulala.
Maisha yaliendelea ,usiku ule Krisi
alimpigia simu Juma akamwambia kuwa amefika salama na anisalimie na kunipa
taarifa hiyo.
Safari ya maisha iliendelea nikiwa
mbali na Krisi.Nilikuwa nasalimiana naye kwa muda mrefu nilipotaka kusalimiana
naye kwa njia ya simu za watu mbalimbali kwa kuwa mimi nilikuwa bado sijanunua
simu.
Muda wa kufanya mtihani wa taifa wa
kidato cha nne ulifika nikafanya mtihani,nikamaliza.
Baada ya kumaliza mtihani, niliingia
mtaani na maisha mapya ya kitaa yalianza.
Bahati nzuri baba alininunulia simu baada ya kumaliza mtihani, kwahiyo hii ilinirahisishia
kuwasiliana na Krisi muda wowote niliohitaji kuwasiliana naye ,hata yeye
kusalimiana na mimi kwa muda aliohitaji kuwasiliana na mimi.
Baadaye nilipata safari ya kwenda
Dare salaamu kumsalimia mama yangu mdogo.Aliniomba niende kwake kwa kuwa
nilikuwa nimemaliza shule.
Niliwasiliana na Krisi ili tukutane
naye Nyegezi aniage.Kikwazo kilichokuja ni kwamba baba ndiye aliyekuwa ananisindikiza,nikamwambia
aje kigogo jioni nilipokuwa kwa baba mdogo ili kusubiria kwenda nyegezi kesho
asubuhi.
Jioni ilipofika Krisi akiwa njiani
kutoka Igoma kuja mjini, baba aliniambia twende
Nyegezi tukakate tiketi, nikajaribu kumkatalia nikamwambia ninataka
kwenda kwa rafiki yangu perepetua ameniambia yuko Bugalika.Baba akaniambia
tukitoka huko nitakuja niende.Nikawa sina jinsi ikabidi niondoke na baba mpaka
Nyegezi.
Tumefika stendi, tulikata
tiketi,huku Krisi akawa ameshafika muda mrefu mjini akinisumbua kwa meseji kuwa
kwanini sitokei?Nilimwambia kuwa baba amenibana sina chansi ya kuja huko
sasa,nikamwomba anisamehe kwa usumbufu.
Akaniambia anarudi nyumbani,mimi nikamruhusu kwasababu baba
hakutaka niende kuzurura zurura mjini ndiyo maana alikuwa ananga’ana twende naye
pamoja Nyegezi.
Tulirejea nyumbani baada ya kumaliza
kukata tiketi na jioni jioni ya saa moja tulienda milongo kwenye soko la joni
ili nikanunue nguo nitakazoenda nazo huko.
Tulipokuwa tumenunua kila
tulichokuwa tunakihitaji tulienda nyumbani kupumzika .
Kesho saa kumi na nusu baba aliniamsha ili nijiandae tuwahi
usafiri Nyegezi stendi.Nilienda kuoga,baada ya kuoga nilivaa nguo tayari kwa
kuanza safari.
Tulienda
mpaka kwnye kituo cha daradara,na kwa muda mfupi gari ilipita tukapanda
lkuelekea Nyegezi.
Tulifika
nyegezi kwenye saa kumi na moja na nusu asubuhi,tukafika tukapanda kwenye gari
ya,,,,,,.
Baba aliniaga akaondoka kurudi nyumbani,na sisi safari ilianza
ilipofika saa kumi na mbili tukaondoka Nyegezi kuiendea Dar.Nikiwa njiani baba
alikuwa akinipiogia simu kuniuliza nilipokuwa nimefika.Krisi naye vivo hivo
karibu safari yote niliongea naye akaniomba nisifike huko nikamwacha yeye na
kuandamana na mwanaume mwingine.
Safari yetu haikuwa na matatizo yoyote hivyo kwenye mida ya
saa tatu saa nne tulifika Ubungo.
Nilimkuta mama mdogo yupo stendi amenisubiria,akanipokea yeye
na mtoto wake wa kike anaitwa Jenifa alikuja naye kuja kunipokea.
Baada ya hapo tulipanda gari za kwenda msasani,kwasababu yeye
alikuwa anaishi Kinondoni shamba.
Tulishukia kwenye kituo kinachoitwa manyanya, tukaenda
nyumbani anapokaa shangazi.
Usiku Krisi alinipigia simu kuniulizia kama nimefika
salama,nikamweleza kuwa tulikuwa tumefika salama na sasa niko nyumbani.
Kesho yake ,nilichelewa kuamka sana,nilijikuta naamuka saa tatu kwasababu ya uchovu wa
safari.Niliamshwa kwa ajiri ya kunywa chai.
Nilinawa uso na kwenda kuoga,baada ya kuoga nilienda mezani
kunywa chai.
Niipomaliza kunywa chai,Jenifa alinichukua tukaenda Kariakoo
kutembea kwa kuwa ni sehemu niliyokuwa natamani niifahamu kutokana na namna ilivyokuwwa inasifika sana
huko nyumbani.Tuliondoka mpaka Kariakoo,tukatembea tembea.Nilipomaliza pale
nilitamani pia nifahamu machinga complex ilipo.Basi Jenifer alinichukua tukaenda
hadi Karume,nikakutana na soko la karume,nikataani kununua viatu.
Tuliingia mle tukaanza kutafuta viatu,lakini katika kutafuta
aina ya kiatu niliyokuwa nahitaji nilijikuta simuoni jenifer,niliangaza pande
zote nne za dunia lakini sikumwona.
Nikaanza kumtafuta ,nikajikuta nimepotea zaidi kwasababu ya
ugeni wa soko hilo.Hata njia ya kutokea
nikawa siioni,nilizunguka sana kama nusu saa bila kuona mlango wa
kutokea,nikafanikiwa kutokea kwenye stendi ile yya Karume sokoni.
Niliogopa kuulizia kwa hofu ya kuibiwa.Nikiwa natafakari
jinsi gani nitaweza kurejea nyumbani,nikijiamini kuwa nitafanikiwa kutokana na
kwamba nilifahamu ninakoelekea,ningemuuliza trafik akanielekeza,nilimwona
Jenifer akiwa anaan gaza angaza huku na kule.
Nilimuita,aliponiona alifurahi sana,kwani alijiuliza ataenda
kujibu nini nyumbani kwa kunipoteza.Tulifurahi,akanionyesha yale majengo ya
machinga complex tukarejea nyumbani.
Siku nyingine tulienda cocobeach siku ya sikukuu ya
Krismas.Tulipokuwa njiani tukienda msasani kupanda gari,kuna watu walituzunguka
wakaninyang’anya simu yangu na kuchukua pochi ya dada Jenifa.Walitutishia kuwa
tukipiga makelele wangetudhuru hata kutuua.Waliendelea na mchezo wao huo mchafu
hasa kwa wasichana na baadhi ya wanaume na hakuna aliyeweza kuwazuia.tulilia tu
na dada Jenifa kwa kupoteza vitu vyetu vya muhimu.
Ikatulazimu kutembea kwa miguu toka kokobeach hadi kinondoni
shamba.Tulipitia barabara ya hail selase.
Huu ndio ukawa mwanzo wa kupoteza ,mawasiliano na Krisi.
Nikiwa nasubiria
matokeo, mama mdogo alinipeleka chuo kikuu huria kusomea kozi fupi ya mwezi mmoja
ya kompyuta.
Matokeo ya klidato cha nne yalitoka ,sikufanya vizuri.Nilipata
daraja la nne ya ishirini na saba.Wazazi wakata kunipeleka vyuo vya ualimu
lakini mimi sikukubali kwa kuwa nilipenda sana kusomea utangazaji .Pia nilikuwa
na hamu ya kusoma Advance.
Ikanididi nirejee nyumbani nikafanye tena upya mtihani wa
kidato cha nne nipate sifa za kujiuunga na kidato cha tano na hatimaye chuo
kikuu.
Nilipofika Mwanza,Nilianza harakati za kumtafuta Krisi mjini
mwanza kuona huenda ninaweza nikagongana naye.Nilikuwa kama kichaa,kwani nilitembea
pasipo kuwa na mwelekeo,nilienda Kamanga,kuona huenda ninaweza kumwona pale
kivukoni akivuka,sikumwona na nusura nigongwe na gari pale kamanga kwasababu
nilitembea tu bila kuangalia kulia na kushoto.
Nilipomkosa pale nilienda
posta kwani kule kulikuwa na wanafunzi wengi waliokuwa wanaangalia
matokeo ya kidato cha nne kwa kuwa kulikuwa na internet kefu
kubwa.Sikumpata,nikarejea nyumbani kwa baba mdogo Igogo.
Kesho yake tena nikasafiri mpaka Igoma kuona kama ninaweza
kubahatisha kumwona lakini hata hivyo sikufanikiwa.Nilijaribu kuuliza watu
mablimabli lakini Krisi ninayemtaka mimi sikumpata.Nikarejea maskani.Siku moja
nikiwa natembea tembea mjini nilikutana na rafiki yake Juma,nikamuuliza kama
alikuwa na namba za simu za Juma,anipe,alinisomea,nikazisevu kwenye simu
yangu.Niliamni nikimpata Juma nitakuwa nimempata Krisi.
Nilianza kumtafuta Juma kupitia namba ya simu niliyopewa na
rafiki yake lakini hakuwa hewani.Nilijaribu kwa siku kadhaa bila mafanikio
,nikahisi huenda amepoteza simu au amebadili laini.
Niliposhindwa kumpata kwa njia hizo niligeukia mitandao ya
kijamii,nikaenda kumtafuta kwenye
facebuku.kwa siku ya kwanza nilijaribu kumwangalia kwa majina ya Krisi,kama Kristofa,Christian
na Krispirin hata hivyo sikumpta.Nikakata tamaa kuwa huenda hayuko kwenye
fecebuku au amejiisajiri majina mengine.
Siku
nyingine nikiwa na chati na marafiki zangu,niliiona sura ya Krisi akiwa
ameandika statas lakini hakuwa anaiitwa Krisi,aliitwa Zakaria.Nilipofuatilia
habari zake nikajilizisha ndiye yule Krisi wangu.
Nikamwomba urafiki(friend request),nikamwandikia na meseji ya
kumweleza kuwa mimi ni aneth, nikampa na namba yangu mpya ya simu.
Nilienda kuangalia kama atakuwa ameitikia, hata hivyo hakuwa
amefanya hivyo.Niliendelea na masomo katika shule ya sekondari ya Mwanza
,nikafanya tena mtihani,nikafanikiwa kufaulu.
Nikachaguliwa kujiunga na Nganza sekondari,nikasoma miaka
yangu miwili pale hadi mwisho, nikafanikiwa kujiunga na chuo kikuu cha Sauti
Mwanza.
Katika muda wote huo nilijitahidi kumtafuta Krisi bila
mafanikio yoyote.Wanaume wengi walijitokeza kuhitaji mahusiano ya kimapenzi na
mimi na wengine kuhitaji kunioa nikakataa.Niliamini kuwa ipo siku ningeonana na
Krisi na kutimiza ahadi yetu ya kuishi kama me na mke.
Marafiki zangu walinikatisha tamaa mara kwa mara,kuwa
nisihangaike na mtu ambaye hata hajulikani yuko wapi,na pengine kashampata mtu
mwingine.Walinilaumu pia kuwakataa wanaume waliojitokeza kutaka kunioa kwa
kuniambia mithali nyingi kama nafasi haiji mara mbili,ukiichezea utakuja
kujuta.Lakini mimi niliendelea kukaza
kuwa nitamtafuta Krisi mpaka nimpate.
Mara kwa mara aliniijia ndotoni na akilini mwangu kana kwamba yuko karibu.Kadri
siku zilivyozidi kwenda ndivyo nilipozidi kumpenda zaidi,ingawa simwoni.
Hata hivyo muda ulivyokuwa ukizidi kusonga nilianza kukata
tamaa na ukiunganisha na maneno ya marafiki zangu yalinivunja moyo,nikamruhu
mwanaume mmoja kuwa naye kimapenzi.
Tumeenda naye kwa muda wa mwaka mmoja na nusu,tukaanza
kufanya mipango ya kuona.
Moyo wangu mara nyingi ulisita kwenda naye nyumbani kwao ili
akanitambulishe,nikawa naahirisha safari kadhaa tulizopanga niende kwao
akanitambulishe.
Alienda kuongea na marafiki zangu,wanishawishi nikubali
kwenda wao.
Wakaja kuongea na mimi kwa kunirazimisha sana na kuniambia
simulizi nyingi nikakubali,nikaenda kwao kunitambulisha.Nilikutana na wazazi
wake wote.Ikabaki safri ya yeye kuja kwetu kuleta barua ya uchumba.
Siku zilivyokuwa zinaenda ,moyo wangu ulianza kupotea kwa
Krisi,na kuhamia kwa Kelvin,mchumba wangu.
Mawazo yangu kwa Krisi yalizidi kutoweka baada ya Kelvin kuja
nyumbani kwetu kuleta barua ya uchumba.Kelvin alijitahidi sana kuniondoa kwa
Krisi kwa kunifanyia mambo mengi kama kunipeleka bichi ,shopingi na kwenye starehe
mbalimbali.Kusema ukweli Kelvin alikuwa amenipenda kwa dhati,alifanya hivyo
kwani marafiki zangu walimpa mkanda mzima wa kuhusu Krisi .
Wazazi wangu waliniiita nyumbani ili kwenda kukiri kama kwao
kuwa kweli nimempenda na ninakubali kujifunga naye ndoa ,isije baadaye ikaleta
shida.
Nikatoka chuoni, nikaenda nyumbani ambako nikama mwendo wa
saa moja na nusu.Nikiwa katika Plantoni ya kutoka Mwanza mjini kwenda Kamanga
,niliona namba mpya ikinipigia,nilipokea nikatambua kuwa ilikuwa ni sauti ya
mwanaume,akajitambulisha kuwa alikuwa Krisi.
Kwanza sikumwelewa vizuri kwasababu ya mawimbi ya ziwani
,baada ya kuvuka nikambipu,akapiga akajieleza sana kuwa ni Krisi yupi
nikatambua kuwa alikuwa ni Krisi niliyekuwa ninamtafuta sana.
Leo hii amepatikana nikiwa nimempata mwingine ambaye tayari
amejitambulisha nyumbani kwetu itakuwaje?
Nilifika nyumbani,nikawakuta wazazi wangu wote wapo ,lakini
pia alikuwepo bibi na shangazi yangu.
Krisi alinipigia tena simu ,Nilimhoji sana kwanini
hakujitokeza zamani zile nilipokuwa nikimtafuta akadai naye pia alikuwa
akinitafuta na isitoshe alienda kusoma Uganda kwahiyo mwanzo alikuwa anapatikana
mida ya likizo tu.
Alinieleza kuwa alikuwa anajaribu kunitafuta ingawa
hakufanikiwa naya kwamba hana mchumba wala hajaoa.Namba yangu alipewa na Juma
ambaye Juma aliipata kwa rafiki yangu mwingine niliyekuwa nakaa naye mtaa mmoja
ila yeye alikuwa Morogoro walpokutana na Juma.
Nilimweleza ukweli kuwa mimi nina mchumba tayari na
ameshajitambulisha nyumbani.
Alinisihi sana kwa kunikumbusha jinsi tulivyoahidiana kuwa
tutapendana mpaka Mungu atakapotutenganisha,hivyo nibadili mpango wangu wa
kuolewa na jamaa huyo.Nikiwa ninaendelea kuongea na Krisi mama aliniita kwenda
kula chakula ili tuendelee na ratiba nyingine ya Kikao.
Nilienda kula,baadaye nikaekiti kuwa nimeanza kuumwa na tumbo
ili kikao kisifanyike,baba kwa vile alivyokuwa ananipenda akawashauri wenzake
kuwa kikao kifanyike kesho asubuhi.
Niliwaza sana jinsi nitakavyoweza kulitatua jambo hili,Krisi
ndiye alikuwa yuko ndani ya moyo wangu lakini Kelvin alikuwa ananipenda
sana,amenifanyia mambo mengi,nikimwambia nimeahirisha anaweza hata akajidhuru
au huenda kunidhuru,nitawaambiaje wazazi wangu ambao wamekuwa wakiletewa zawadi
nyingi na Kelvin,nilizozileta mimi mwenyewe?
Usiku kucha niliwaza mambo hayo pasipo kupata majibu.kulipokucha
nilipata wazo kuwa nimuite shangazi nimweleze ukweli ili yeye anisaidie
kuwaambia wazazi .
Nilimuita shangazi nikamweleze picha yote jinsi ilivyo.Hata
yeye hakuwa na majibu,alitikisa kichwa tu na kuniuliza swali ,tutafanyaje sasa
mwanangu?
Lakini akaniahidi kwenda kuongea na wazazi wangu waone jinsi
watakavyolitatua swala hilo.
Walipomaliza kunywa chai.Saa tatu shangazi aliwaita wote kuwa
kuna jambo gumu wanalotakiwa kulijadili kabla hawajaongea na mimi.
Walikaa kikao,shangazi akawafungulia mkanda wote.Mama
alichukia sana,kama ada yake kwani yeye
ndiye alikuwa mkali zaidi hata ya baba,akaniita ,lakini baba akamkataza kuwa
wajadili kwanza hoja iliyo mezani,wataniita.
Walijadiliana na mwisho wa kikao hicho wakaniita,wakasema kuwa
wamekubaliana kusitisha suala la uchumba wangu,na ili kumsaidia
mwenzangu(Kelvin) ninatakiwa kumdanganya kuwa kunamatatizo Fulani yamejitokeza
wamekubaliana hadi mwakani,baadaye nianze kuwa mbali naye kidogo kidogo mpaka
atakapoona mwenyewe kuwa sitaki kufunga naye ndoa.
Nilirejea chuoni,Kelvin alinipokea akitaka kujua sababu ya
wazazi kuniita nyumbani.Nilimwambia kama wazazi walivyonieleza kuwa wameona
maswala haya wayahamishe mwakani kwahiyo awe mvumilivu.
Kelvin alihoji sana kwanini wameamua hivyo wakati mimi kila
kitu kiko sawa ,uwezo wa kuandaa harusi ninao?
Nikamwomba awe mvumilivu,nikijua kuwa ukweli kuwa ,huo ndio
ulikuwa mwisho wake.
Tuliendelea kuwasiliana na Krisi alikuwa anafanya kazi Tanga katika kiwanda cha simenti,akaniahidi kukutana naye wakati wa likizo yake.
Tuliendelea kuwasiliana na Krisi alikuwa anafanya kazi Tanga katika kiwanda cha simenti,akaniahidi kukutana naye wakati wa likizo yake.
Huku nako nilijitahidi kumukwepa Kelvin aliyetaka kila sehemu
twende naye,kwa visingizio vya ugonjwa ,uchovu na ushauri wa kutunza pesa kwa
ajiri ya maisha ya baadaye.
Tabia hii ilipokuwa endelevu aliwauliza marafiki
zangu,wakamwambia ukweli kuwa tayari nilikuwa nimeshapata Krisi.
Aliniarika kwenye chakula cha mchana,nikaenda.Akaniambia kuwa
tayari alikuwa ameshajua kwanini nimekuwa sitaki kwenda naye kama ambavyo
amekuwa akiniomba,na mimi nikamweleza ukweli tu.Alijitahidi kunibembeleza nibadili
maamuzi yangu,nikumbuke kuwa tayari alishanipeleka kwa wazazi wake atawaambia
nini? Na alikuwa ananipenda sana.Aliongea kwa hisia kubwa,kiasi cha kwamba
macho yalinilenga ,nikamuhurumia sana lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kuamua
kama nilivyokuwa nimeamua.Si kosa langu mimi kwenda kwao ,yeye ndiye
aliyenilazimisha, mimi nilikuwa sitaki.
Nilipoendelea na msimamo wangu alinipa muda wa kwenda
kufikiria zaidi.
Niliendelea kuongea na Krisi akaniahidi kuwa akija atafanya
mipango ya kufunga ndoa.Hii ikafanya mawazo yangu kwa Kelvin kutokomea katika
vyumba vya moyo wangu.
Kelvin alimaliza chuo ,yeye alikuwa amenitangulia mwaka mmoja
akaenda kwao,Shinyanga.Aliondoka bila hata kuniaga,kwa kuwa nilikuwa kama nimemsariti.Mimi
niliendelea na chuo,nikamaliza.
Krisi alikuja Mwanza,nikampokea katika stendi ya
Nyegezi,tukaenda kwao akanitambulisha.Baadaye tulifunga ndoa tukawa mme na mke.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni